Wednesday, November 4, 2015
SERIKALI YA TANZANIA YAKANUSHA TAARIFA ZA UZUSHI KUHUSU RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA
Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Assah Mwambene amekanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa kuwa amefariki Dunia.
Akizungunza na waandishi wa habari Hii leo katika ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Mwambene amesema Rais Mkapa yupo salama na mzima wa afya na hakuna maradhi yoyote yanayomsumbua.
Mwambene amewaasa watumiaji wa mitandao mbalimbali hasa Blogs kuacha kuitumia mitandao hiyo kwa kupotosha umma na kuandika mambo yasiyo na ukweli ili kuepusha mifumuko ya habari za upotishaji.
Aidha amesema Serikali italishughulikia hili na tayari imeshaanza kukamata baadhi ya watu mbalimbali ambao wanatoa taarifa za uongo zinazopelekea umma kupotoka.
Amesema kuwa vyombo vya habari vifanye kazi kwa uweredi ili kazi ya uandishi wao iwe ya usawa na kufuata misingi ya uandishi, jambo ambalo wengi hukiuka kutokana kutofuata weredi wa kazi zao.
Popular Posts
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...
-
Facebook is developing a new smartphone app to track the location of users in an effort to target them with localised adverts, acc...