Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kutokana na kushamiri kwa wizi katika mifumo ya malipo kwa njia ya kielekroniki kwenye simu za kiganjani na miamala ya fedha ya benki.
Wakizungumzia bungeni jana wakati wakichangia muswada huo,wamesema kampuni za simu zinawakata wananchi fedha katika simu zao za kiganjani bila ridhaa yao na hakuna sehemu yoyote wanayoweza kufikisha malalamiko yao ili warejeshewe fedha hizo.
Katika muswada huo uliowasilishwa na Waziri wa Fedha,Saada Mkuya Salum,Serikali imependekeza kuboresha usimamizi na kuongeza udhibiti,kuimarisha mifumo ya malipo,pia kuzuia na kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza katika mifumo hiyo na kuongeza faini kwa kampuni za simu na benki zitakazokiuka sheria na utaratibu.
Popular Posts
-
KAMPENI YA KUHAMASISHA MATUMIZI MAZURI YA MAWASILIANO Siku za hivi karibuni, ongezeko la huduma za mawasiliano nchini limekuwa kwa kas...
-
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Konferensi ya Mashariki mwa Tanzania Mchungaji Mark Warwa Marekana, Mchungaji L.Cooper ambaye ni Makam...
-
Wamiliki wa simu nchini kuanzia mwezi ujao wataanza kuingia gharama zaidi kwa asilimia 14.5 ili kuongeza mapato ya Serikali na kughar...
-
Mark Zuckerberg Facebook inasherehekea miaka kumi wiki hii tangu kuzinduliwa. Ina watumiaji bilioni 1.2. Lakini nani anatumia Face...
-
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Mch Musa Mika akizungumza na wanahabari kuhusu warsha ya Mawasiliano...