Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kutokana na kushamiri kwa wizi katika mifumo ya malipo kwa njia ya kielekroniki kwenye simu za kiganjani na miamala ya fedha ya benki.
Wakizungumzia bungeni jana wakati wakichangia muswada huo,wamesema kampuni za simu zinawakata wananchi fedha katika simu zao za kiganjani bila ridhaa yao na hakuna sehemu yoyote wanayoweza kufikisha malalamiko yao ili warejeshewe fedha hizo.
Katika muswada huo uliowasilishwa na Waziri wa Fedha,Saada Mkuya Salum,Serikali imependekeza kuboresha usimamizi na kuongeza udhibiti,kuimarisha mifumo ya malipo,pia kuzuia na kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza katika mifumo hiyo na kuongeza faini kwa kampuni za simu na benki zitakazokiuka sheria na utaratibu.
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Blogger katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa Ubalozi wa Marekani Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania kupitia kitengo chake cha M...
-
Tokea LAPTOP zimeanza kuingia sokoni zimekua sehemu ya maisha yetu ya kila siku . Mwanzoni hazikua zinapendeza sana , Kubwa na Gha...
-
Watumiaji wa Gmail takribani bilioni moja duniani wako hatarini kudhuriwa na uhalifu mtandao aina ya Phishing ambao umelenga programu tum...
-
Kwa mara ya kwanza, wanafunzi Tanzania wanaweza kujipatia nyenzo za kujifunzia masomo ya sekondari bila gharama yoyote kupiti...
-
Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues na Mkurugenzi wa Samsung Electronics nchini Tanzania, Bw. Mike Seo...
-
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo nchini Tanzania Assah Mwambene Mhandisi wa TCRA,Andrew Kisaka akiwasilisha Mada kuhusu ma...
-
Watu sita wanaosadikiwa kuwa ni matapeli kwa njia ya mtandao wa simu wamekamatwa jijini mwanza baada ya kufanya utapeli kwa watu mbali ...
-
Serikali nchini Tanzania imetakiwa kuimarisha kitengo cha upelelezi na ufatiliaji wa makosa jinai yanayofanywa kupitia mitandao ya sim...