Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kutokana na kushamiri kwa wizi katika mifumo ya malipo kwa njia ya kielekroniki kwenye simu za kiganjani na miamala ya fedha ya benki.
Wakizungumzia bungeni jana wakati wakichangia muswada huo,wamesema kampuni za simu zinawakata wananchi fedha katika simu zao za kiganjani bila ridhaa yao na hakuna sehemu yoyote wanayoweza kufikisha malalamiko yao ili warejeshewe fedha hizo.
Katika muswada huo uliowasilishwa na Waziri wa Fedha,Saada Mkuya Salum,Serikali imependekeza kuboresha usimamizi na kuongeza udhibiti,kuimarisha mifumo ya malipo,pia kuzuia na kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza katika mifumo hiyo na kuongeza faini kwa kampuni za simu na benki zitakazokiuka sheria na utaratibu.
Popular Posts
-
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania itafanya sherehe maalumu za kutimiza miaka 50 ya Uhuru katika Wiki ya Sayansi ...
-
Wakulima nchini Nigeria wamepewa bure simu za mikononi,Ingawa vyama vya upinzani vinakandia hali hiyo wananchi wengi wanaamini huo ni...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...
-
Baadhi ya Wataalamu wa Teknohama wa Taasis za Kanisa la Waadventista Wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Kanisa l...