Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kutokana na kushamiri kwa wizi katika mifumo ya malipo kwa njia ya kielekroniki kwenye simu za kiganjani na miamala ya fedha ya benki.
Wakizungumzia bungeni jana wakati wakichangia muswada huo,wamesema kampuni za simu zinawakata wananchi fedha katika simu zao za kiganjani bila ridhaa yao na hakuna sehemu yoyote wanayoweza kufikisha malalamiko yao ili warejeshewe fedha hizo.
Katika muswada huo uliowasilishwa na Waziri wa Fedha,Saada Mkuya Salum,Serikali imependekeza kuboresha usimamizi na kuongeza udhibiti,kuimarisha mifumo ya malipo,pia kuzuia na kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza katika mifumo hiyo na kuongeza faini kwa kampuni za simu na benki zitakazokiuka sheria na utaratibu.
Popular Posts
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
Serikali kusambaza tabiti za kufundishia sekondari Yaanza kazi hiyo kwa kushirikiana na taasisi ya Marekani ya Opportunity Education Tr...
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...