Saturday, May 2, 2015

TAHADHARI KWA WANAOANGALIA TOVUTI ZA PICHA ZA NGONO KATIKA SIMU ZAO


Watafiti toka kampuni ya utafiti ya  Zscalar  wamegundua kuwa,tovuti za kichina zenye picha za ngono zimekuwa zikisambaza virusi ambavyo vinasababisha simu za mikononi kushambuliwa na virusi vya komputa viitwavyo malware.
Utakapotembelea tovuti hizo na ukajaribu kuangalia video,tovuti itakuomba upakue sehemu ya program ya komputa ambayo kiuhalisia ni kirusi kiingine kiitwacho trojan.

Kirusi hicho cha Trojan kinajishajilisha chenyewe kwenye simu yako na kuifanya simu yako kuwa na uwezo wa kupokea matangazo yanayohusisha  ujumbe mfupi wa maneno (sms) ulioko kwenye simu yako.Jambo ambalo litasaidia wahalifu wa mtandao kudukua taarifa zako za kibenki kwenye simu iliyo na kirusi hicho kiurahisi.


Popular Posts

Labels