Wadau kutoka kampuni na mashirika mbalimbali nchini Tanzania wameshauri kutolewa elimu zaidi kuhusu matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Teknohama) na ufanisi wake ili kuleta tija kwa watanzania wengi.
Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa warsha ya Teknohama iliyotolewa na ubalozi wa Marekani nchini Tanzania,wadau hao walisema ni muhimu kwa wadau wengine ikiwamo serikali kuandaa mafunzo kama hayo kwani kuna mambo mengi ya msingi ambayo bado yanasumbua katika matumizi sahihi na ufanisi wa Teknohama.
Mmoja wa maofisa wa ubalozi wa Marekani Jeffrey Shrader alisema waliandaa warsha hiyo kwa sababu ya kukua kwa kiasi kikubwa kwa Teknolojia ulimwenguni hivyo ni vyema kuwaelimisha wengine ambao hawafahamu.
Katika warsha hiyo wakufunzi mbalimbali walitoa mada zinazohusiana na Teknohama ikiwemo ulinzi wa mawasiliano kama vile komputa na simu,mfumo wa uendeshaji wa mambo ya kuchukua na kutumia taarifa katika mitandao.
Popular Posts
-
Kitabu hiki kipo tayari. Wasiliana kwa namba 0713 309 314 au 0763 309 314 na Mushi Richard, Mpesa: 0755872462, Tigopesa: 0713643703 ...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginev...
-
Mtandao wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha. Nia...
-
Bwana. Keriako Tobiko Mkurugenzi wa Mashtaka ya umma ya nchini Kenya Bwana. Keriako Tobiko ametangaza kuanzishwa kwa kitengo maalum...
-
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA UMMA Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha...
-
Waziri na waziri wa uchukuzi Dr Harrison mwakyembe amesema kuwa Teknolojia ya kisasa inayotumika katika uwanja wa ndege wa kimataifa...
-
Polisi Wa kuzuia uhalifu Mtandao. Wakala unaofuatilia matumizi ya mitandao duniani (IAB) umebaini watumiaji wa intaneti nchini Ko...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania jana ilianza kuendesha mkutano wa kimataifa kuhusu usimamizi na utekelezaji wa huduma ya simu za mkononi kwa...
-
A failure in contingency planning and disaster recovery Today, on November 14, 2012 in Tanzania, the TIGO network was completely not...