Wadau kutoka kampuni na mashirika mbalimbali nchini Tanzania wameshauri kutolewa elimu zaidi kuhusu matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Teknohama) na ufanisi wake ili kuleta tija kwa watanzania wengi.
Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa warsha ya Teknohama iliyotolewa na ubalozi wa Marekani nchini Tanzania,wadau hao walisema ni muhimu kwa wadau wengine ikiwamo serikali kuandaa mafunzo kama hayo kwani kuna mambo mengi ya msingi ambayo bado yanasumbua katika matumizi sahihi na ufanisi wa Teknohama.
Mmoja wa maofisa wa ubalozi wa Marekani Jeffrey Shrader alisema waliandaa warsha hiyo kwa sababu ya kukua kwa kiasi kikubwa kwa Teknolojia ulimwenguni hivyo ni vyema kuwaelimisha wengine ambao hawafahamu.
Katika warsha hiyo wakufunzi mbalimbali walitoa mada zinazohusiana na Teknohama ikiwemo ulinzi wa mawasiliano kama vile komputa na simu,mfumo wa uendeshaji wa mambo ya kuchukua na kutumia taarifa katika mitandao.
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...