Wadau kutoka kampuni na mashirika mbalimbali nchini Tanzania wameshauri kutolewa elimu zaidi kuhusu matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Teknohama) na ufanisi wake ili kuleta tija kwa watanzania wengi.
Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa warsha ya Teknohama iliyotolewa na ubalozi wa Marekani nchini Tanzania,wadau hao walisema ni muhimu kwa wadau wengine ikiwamo serikali kuandaa mafunzo kama hayo kwani kuna mambo mengi ya msingi ambayo bado yanasumbua katika matumizi sahihi na ufanisi wa Teknohama.
Mmoja wa maofisa wa ubalozi wa Marekani Jeffrey Shrader alisema waliandaa warsha hiyo kwa sababu ya kukua kwa kiasi kikubwa kwa Teknolojia ulimwenguni hivyo ni vyema kuwaelimisha wengine ambao hawafahamu.
Katika warsha hiyo wakufunzi mbalimbali walitoa mada zinazohusiana na Teknohama ikiwemo ulinzi wa mawasiliano kama vile komputa na simu,mfumo wa uendeshaji wa mambo ya kuchukua na kutumia taarifa katika mitandao.
Popular Posts
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Watu wengi wameshaona filamu ambazo wahalifu wakidukua simu za mikononi hata kama zimezimwa. Kama ili...
-
Na Yusuph Kileo Nchi ya Tanzania yabahatika tena kwa mara ya tatu kuwa mwenyeji wa mkutano wa “Connect 2 Connect” ambapo kauli mbiu ya...
-
Kutoka Kushoto Gerald Masatu,Mtangazaji Maduhu,Brown Nyanza(IFM),Mama Kagize,Johnson Kuga Mzirai na Jonathan Mnyela Jonathan Mnyela ...
-
Imeelezwa kuwa wananachi wengi bado hawana uelewa wa kutosha juu ya haki zao za msingi katika huduma za mawasiliano wanazotumia, hali ambayo...
-
Wakati bado mafanikio mbali mbali yakijadiliwa wahalifu mtandao wamegundulika kuja na uhalifu unaotafsiriwa kuwa ni wa kihistoria na uliof...
-
Jeshi la Polisi Tanzania limeanza kunasa watu wanaodaiwa kutuma ujumbe wa matusi na wengine kupiga simu kwa spika wa Bunge la nchi hiyo Anne...