Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania jana ilianza kuendesha mkutano wa kimataifa kuhusu usimamizi na utekelezaji wa huduma ya simu za mkononi kwa kutumia kadi moja ya simu kwa mitandao yote bila kuwa na simu kadi nyingi za mitandao tofauti.
Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo wa siku mbili Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,Profesa John Nkoma, alisema kadi moja ya simu ya mkononi inaweza kutumika katika zaidi ya mtandao mmoja wa simu kama mteja atataka kuhama kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine bila kununua kadi nyingine ya simu kama ilivyozoeleka.
Alisema lengo la mkutano huo ni kutaka kujadili kwa kina utekelezaji na usimamizi wa huduma maalum ya mawasiliano ya simu ambapo mtumiaji wa simu ya mkononi anaweza kutumia kadi moja tu kama atataka kujiunga na mtandao mwingine.
Huduma hiyo inatarajiwa kuanza mapema mwakani baada ya maandalizi na michakato yote,Huduma hii imeshaanza kutumika nchini Kenya tangu Aprili mwaka jana
Friday, November 16, 2012
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Wakulima nchini Nigeria wamepewa bure simu za mikononi,Ingawa vyama vya upinzani vinakandia hali hiyo wananchi wengi wanaamini huo ni...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Makubaliano ambayo yangeiruhusu kampuni kubwa ya simu ya Marekani, AT&T kuinunua kampuni ya T-mobile tawi la Marekani la kampuni ya Uj...
-
Baadhi ya Wataalamu wa Teknohama wa Taasis za Kanisa la Waadventista Wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Kanisa l...