Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania jana ilianza kuendesha mkutano wa kimataifa kuhusu usimamizi na utekelezaji wa huduma ya simu za mkononi kwa kutumia kadi moja ya simu kwa mitandao yote bila kuwa na simu kadi nyingi za mitandao tofauti.
Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo wa siku mbili Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,Profesa John Nkoma, alisema kadi moja ya simu ya mkononi inaweza kutumika katika zaidi ya mtandao mmoja wa simu kama mteja atataka kuhama kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine bila kununua kadi nyingine ya simu kama ilivyozoeleka.
Alisema lengo la mkutano huo ni kutaka kujadili kwa kina utekelezaji na usimamizi wa huduma maalum ya mawasiliano ya simu ambapo mtumiaji wa simu ya mkononi anaweza kutumia kadi moja tu kama atataka kujiunga na mtandao mwingine.
Huduma hiyo inatarajiwa kuanza mapema mwakani baada ya maandalizi na michakato yote,Huduma hii imeshaanza kutumika nchini Kenya tangu Aprili mwaka jana
Friday, November 16, 2012
Popular Posts
-
Moja ya sehemu iliyofanikiwa kufanya mapinduzi makubwa ya teknolojia ya sayansi ni teknolojia ya habari na mawasiliano. Katika mapin...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kuzingatia kifungu 5 (b) na (e) cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya 2003 inatoa t...
-
Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 inakadiliwa kuwa jumla ya program tumishi kwenye simu zitakazo kuwa zimepakuliwa duniani zitakuwa ni bi...
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Serikali ya Tanzania imesema shilingi trioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao,endapo Sheria za...
-
Kumekuwa na changamoto ya kujilinda na watu ambao wanaweza kukuwekea maelezo ama kukutagg picha usiyoihitaji kwenye timeline ...
-
Habari si nzuri kwa wanaume wanaopenda kutumia wireless internet kwenye laptop zao wakiwa wameziweka laptop zao mapajani au karibu na viun...