Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania jana ilianza kuendesha mkutano wa kimataifa kuhusu usimamizi na utekelezaji wa huduma ya simu za mkononi kwa kutumia kadi moja ya simu kwa mitandao yote bila kuwa na simu kadi nyingi za mitandao tofauti.
Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo wa siku mbili Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,Profesa John Nkoma, alisema kadi moja ya simu ya mkononi inaweza kutumika katika zaidi ya mtandao mmoja wa simu kama mteja atataka kuhama kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine bila kununua kadi nyingine ya simu kama ilivyozoeleka.
Alisema lengo la mkutano huo ni kutaka kujadili kwa kina utekelezaji na usimamizi wa huduma maalum ya mawasiliano ya simu ambapo mtumiaji wa simu ya mkononi anaweza kutumia kadi moja tu kama atataka kujiunga na mtandao mwingine.
Huduma hiyo inatarajiwa kuanza mapema mwakani baada ya maandalizi na michakato yote,Huduma hii imeshaanza kutumika nchini Kenya tangu Aprili mwaka jana
Friday, November 16, 2012
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...