Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaandaa utaratibu wa kuanzisha mfumo mpya wa kuhama mtandao bila ya kubadili namba ya simu(MNP) na kuhamia mtandao mwingine.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,Prof.John Nkoma anasema mfumo huo utawasaidia watu wote wanaotumia simu nchini humo waliokuwa wanashindwa kuhamia mtandao mwingine kwa hofu ya kubadili namba ya simu,lakini baada ya kuzindua mfumo huu watu watahama mitandao kwa urahisi bila kubadili namba za simu.
Anafafanua kuwa mfumo huo utasaidia kuleta ushindani kwa makampuni ya simu na kuleta faida kwa wateja,pia makampuni hayo yataweza kuongeza ubora wahuduma kwa wateja wao.
TCRA imeandaa makutano wa kimataifa ambao utahudhuriwa na watu zaidi
ya 100 wa kuzungumzia suala hilo ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa
Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania,Prof.Makame
Mbarawa.
Mkutano huo wa siku mbili unaotarajiwa kuanza kesho
umeandaliwa kwa ushirikiano na Umoja wa Mawasiliano Duniani (ITU) na
utahudhuriwa na wawakilishi mbalimbali kutoka duniani kote zikiwemo nchi
za Afrika Mashariki
Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo aliwataka wananchi kununua vinga'amuzi mapema ili kuondokana na usumbufu ambao unaweza kujitokeza baada ya kuhamia katika mfumo wa digital Disemba 31 mwaka huu.
Popular Posts
-
Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya iOS 12.2 kwa ajili ya iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivy...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Kuna Utapeli umeanza kusambaa saa chache zilizopita kupitia CRDB INTERNET BANKING . Anayefanya utapeli huu ametengeneza majina band...
-
Facebook is developing a new smartphone app to track the location of users in an effort to target them with localised adverts, acc...
-
Tokea LAPTOP zimeanza kuingia sokoni zimekua sehemu ya maisha yetu ya kila siku . Mwanzoni hazikua zinapendeza sana , Kubwa na Gha...
-
Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani mkoani Dar es salaam limeanzisha kanuni ya tozo la papo kwa hapo kwa njia ya kiel...
-
Shirika la Ugavi wa Umeme nchini Tanzania (TANESCO) limeibuka mshindi wa jumla wa kero kwa wateja wa huduma mbalimbali na bidhaa hapa nc...
-
Wadau kutoka kampuni na mashirika mbalimbali nchini Tanzania wameshauri kutolewa elimu zaidi kuhusu matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari ...