Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaandaa utaratibu wa kuanzisha mfumo mpya wa kuhama mtandao bila ya kubadili namba ya simu(MNP) na kuhamia mtandao mwingine.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,Prof.John Nkoma anasema mfumo huo utawasaidia watu wote wanaotumia simu nchini humo waliokuwa wanashindwa kuhamia mtandao mwingine kwa hofu ya kubadili namba ya simu,lakini baada ya kuzindua mfumo huu watu watahama mitandao kwa urahisi bila kubadili namba za simu.
Anafafanua kuwa mfumo huo utasaidia kuleta ushindani kwa makampuni ya simu na kuleta faida kwa wateja,pia makampuni hayo yataweza kuongeza ubora wahuduma kwa wateja wao.
TCRA imeandaa makutano wa kimataifa ambao utahudhuriwa na watu zaidi
ya 100 wa kuzungumzia suala hilo ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa
Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania,Prof.Makame
Mbarawa.
Mkutano huo wa siku mbili unaotarajiwa kuanza kesho
umeandaliwa kwa ushirikiano na Umoja wa Mawasiliano Duniani (ITU) na
utahudhuriwa na wawakilishi mbalimbali kutoka duniani kote zikiwemo nchi
za Afrika Mashariki
Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo aliwataka wananchi kununua vinga'amuzi mapema ili kuondokana na usumbufu ambao unaweza kujitokeza baada ya kuhamia katika mfumo wa digital Disemba 31 mwaka huu.
Popular Posts
-
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania itafanya sherehe maalumu za kutimiza miaka 50 ya Uhuru katika Wiki ya Sayansi ...
-
Wakulima nchini Nigeria wamepewa bure simu za mikononi,Ingawa vyama vya upinzani vinakandia hali hiyo wananchi wengi wanaamini huo ni...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Makubaliano ambayo yangeiruhusu kampuni kubwa ya simu ya Marekani, AT&T kuinunua kampuni ya T-mobile tawi la Marekani la kampuni ya Uj...
-
Baadhi ya Wataalamu wa Teknohama wa Taasis za Kanisa la Waadventista Wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Kanisa l...