Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaandaa utaratibu wa kuanzisha mfumo mpya wa kuhama mtandao bila ya kubadili namba ya simu(MNP) na kuhamia mtandao mwingine.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,Prof.John Nkoma anasema mfumo huo utawasaidia watu wote wanaotumia simu nchini humo waliokuwa wanashindwa kuhamia mtandao mwingine kwa hofu ya kubadili namba ya simu,lakini baada ya kuzindua mfumo huu watu watahama mitandao kwa urahisi bila kubadili namba za simu.
Anafafanua kuwa mfumo huo utasaidia kuleta ushindani kwa makampuni ya simu na kuleta faida kwa wateja,pia makampuni hayo yataweza kuongeza ubora wahuduma kwa wateja wao.
TCRA imeandaa makutano wa kimataifa ambao utahudhuriwa na watu zaidi
ya 100 wa kuzungumzia suala hilo ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa
Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania,Prof.Makame
Mbarawa.
Mkutano huo wa siku mbili unaotarajiwa kuanza kesho
umeandaliwa kwa ushirikiano na Umoja wa Mawasiliano Duniani (ITU) na
utahudhuriwa na wawakilishi mbalimbali kutoka duniani kote zikiwemo nchi
za Afrika Mashariki
Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo aliwataka wananchi kununua vinga'amuzi mapema ili kuondokana na usumbufu ambao unaweza kujitokeza baada ya kuhamia katika mfumo wa digital Disemba 31 mwaka huu.
Popular Posts
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...