Wednesday, September 3, 2014

WIZARA YASEMA MKONGO WA TAIFA UMESAIDIA KUPUNGUZA GHARAMA ZA MAWASILIANO TANZANIA



Wizara ya mawasiliano  sayansi na teknolojia imesema mkongo wa mawasiliano nchini Tanzania umefanikiwa kupunguza gharama za mawasiliano kwa watumiaji wachini ktk maeneo ambayo makampuni ya simu yameshindwa kuyafikia.

Akizungumza na waandishi wa habarI jijini Dar es salaam msemaji mkuu wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia Bi Prisca Ulomi amesema mkongo huo unasaidia jamii ambapo huduma zinazohitaji viwango vikubwa vya njia ya mawasiliano kama Elimu Mtandao, Biashara Mtandao, Afya mtandao, mikutano mtandao zinapatikana kupitia mkongo huo.

Bi Ulomi amesema mkongo huo umejengwa kwa viwango vya hali ya juu vya kimataifa na kuongeza kuwa kupitia kifaa hicho Tanzania imekuza mahusiano nanchi jirani za Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi ,Uganda na Kenya kwani makampuni ya simu nchini Tanzania yametumia mkongo huo kuunganisha nchi hizo.

Ameongeza kuwa mkongo huo wa kimataifa ulioenea ktk maeneo mengi hapa nchini pamoja na nchi jirani ktk awamu ya kwanzana ya pili utasaidia kufikisha huduma kwa wananchi kwa unafuu na kuhakikisha maendeleo ya taifa kwani wananchi watapata fursa ya kutumia Tehama ktk juhudi za kupambana na umasikini hapa nchini.

Popular Posts

Labels