Friday, September 19, 2014

DEREVA ATAKAYE KAMATWA AKIENDESHA GARI HUKU AKIONGEA NA SIMU KUFUTIWA LESENI

Picha kwa hisani yan http://www.sligotoday.ie
Jeshi la Polisi kikosi cha usalama Barabarani nchini Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya usafiri wa Nchi kavu na Majini SUMATRA limeanzisha mkakati wa kuwafungia leseni madereva watakaobanika kuendesha magari huku wakiwa manazungumza na simu za mkononi.

Zoezi hilo limekuja kufuatia kile kinachodaiwa kuwepo kwa ongezeko la ajali za barabarani ambazo zinasababishwa na uzembe ambao unasababishwa na unywaji wa pombe,kuchoka na kuzungumza na simu hizo.

Takwimu zinaonyesha kuwa kumekuwa na ongezeko la matukio 264 ya ajali barabarani kwa mwaka 2013 sawa na asilimia 1.1 tofauti na mwaka 2012 ambapo matukio yalikuwa 23,578.

Kwa mwaka huu kati ya januari hadi June idadi ya ajali zilizoripotiwa zilikiwa 8,405 zilizosababisha vifo 1743 na majeruhi 7,523 hali ambayo Kamanda Mpinga anasema ipo mikakati mbadala ya kukabiliana na hali hiyo.

Inatajwa kuwa madereva wengi hawana tabia ya kupima afya zao mara kwa mara,inaelezwa kuwa magonjwa ya macho,kisukari pamoja na shinikizo la damu pia linachangia ajali nyingi.

Popular Posts

Labels