Thursday, July 17, 2014

ARUSHA:MIKAKATI YA KUKABILIANA NA UDUKUZI YAPANGWA NA CHUO KIKUU CHA NELSON MANDELA



Chuo Kikuu cha Nelson Mandela cha jijini Arusha kimeanza utaratibu kuwashirikisha watafiti na wabunifu kutoka makundi mbalimbali katika jamii ilikukabiliana na tatizo la Udukuzi wa taarifa za watu kwa vifaa vya mawasiliano vinavyotumia teknolojia mpya ya habari na mawasiliano.

Mkrugenzi wa chuo hicho Bwana Balton Mwamila amesema kuwa ilikufanikisha maadhimio hayo wameamuakuandaa maonesho ya ubuni fu na ugunduziwa teknolojia inayohusu masuala ya kisayansi.

Amesema kuwa bado yapo matatizo yanayo ikabili jamii hasa pale kunako tokea mabadiliko ya kisayansi huku kukiwa hakuna sheria zinazotoa miongozo inayombana mtumiaji wateknolojia mpya hali inayosababisha mtu kuangalia au kudukua taarifazawatu.

Ameeleza kuwakupitia mtandao watu hufahamu undani wa mtu hasa kupitia taarifa zilizohifadhiwa hali aliyoeleza kuwa si sahihi nani hatari kiusalama hasa kwa mwenye taarifa za mtu binafsi.

Aidha swala udukuaji wa taarifa au mawasiliano ya mtu bila ridhaa yamekuwa yakilalamikiwa katika nchi mbalimbali ambapo hivi karibuni nchi ya Uingereza na Ujerumani ziliilalamikia nchi ya Marekani kupitia kikosi chake cha kijasusi kwa kile walichodai kuwa wamedukuliwa taarifa mbalimbali za kimtandao huku nchi nyingi hasa zinazoendelea zikiwa hazina sheria za kuwabana baadhi ya watu wanaotekeleza vitendohivyo.

Popular Posts

Labels