Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu za kibenki,jambo ambalo linahatarisha usalama wa fedha zao zinazohifadhiwa na benki hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB,Dr Charles Kimei amesema jijini Dar es salaam hivi karibuni kuwa kumeibuka mchezo kwa baadhi ya mitandao ya kijamii,ikijaribu kuwalaghai wateja kwa kuwaomba taarifa za akaunti zao ili kufanya uhalifu.
Amesema wananchi wanatakiwa kuwa makini na kundi hilo,wasikubali kudanganyika kwa kutoa taarifa zinazohusiana na nyaraka nyeti za benki zao na kusisitiza kuwa ni marufuku kutoa taarifa hizo kwa wafanyakazi wa benki.
Mkurugenzi huyo amesema pamoja na kwamba benki hiyo inawapigia simu wateja wao wakitaka kukamilisha usaili wao kuhusiana na kuingia katika mfumo wa uboreshaji wa huduma za benki hiyo kupitia simu za mkononi unaoitwa Simbaking watambue kuwa hawataulizwa kutoa taarifa zozote za akaunti.
Kuhusu mbinu zinazotumiwa na wahalifu,Mkurugenzi wa Idara Hatarishi James Mabula amesema huwapigia simu wakijifanya kuwa wakurugenzi ama wafanyakazi wa benki hiyo na kisha kuwaghilibu kwa kutaka kupatiwa namba za siri za akaunti husika.
Popular Posts
-
Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya iOS 12.2 kwa ajili ya iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivy...
-
Kuna Utapeli umeanza kusambaa saa chache zilizopita kupitia CRDB INTERNET BANKING . Anayefanya utapeli huu ametengeneza majina band...
-
Kitabu hiki kipo tayari. Wasiliana kwa namba 0713 309 314 au 0763 309 314 na Mushi Richard, Mpesa: 0755872462, Tigopesa: 0713643703 ...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginev...
-
Mtandao wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha. Nia...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
Bwana. Keriako Tobiko Mkurugenzi wa Mashtaka ya umma ya nchini Kenya Bwana. Keriako Tobiko ametangaza kuanzishwa kwa kitengo maalum...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA UMMA Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha...