Thursday, May 15, 2014

NCHINI KENYA:WANAOTUMA UJUMBE WA NGONO KWA SIMU NA MITANDAO KUFUNGWA JELA



Serikali ya Kenya imesema watu watakaopatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kingono kwa kutumia simu za kiganjani na intaneti watafungwa Jela.

Adhabu hiyo itawahusu wale wanaotuma ujumbe wenye picha za watu walio uchi na zenye mada ya ngono nchini humo.

Maafisa wakuu wa serikali wanasema kuwa yeyote atakayepatikana na hatia atafungwa jela kifungo cha miezi mitatu kwenda chini.

Afisa mkuu kutoka tume ya mawasiliano ya Kenya , Christopher Wambua, ameviambia vyombo vya habari nchini humo ,kwamba watu wenye tabia hiyo ya kutuma ujumbe wa kingono ,pamoja na picha zenye watu walio uchi ,watatozwa hadi shilingi elfu hamsini za Kenya au dola miatano na themanini na nane za kimarekani sawa na shilingi laki tisa arobaini elfu na mia nane za kitanzania kama faini au kufungwa jela.

Onyo hilo litawahusu hasa wale walio na uzoefu wa kutumiana ujumbe kama huo kupitia kwa simu ya kiganjani au kwenye intaneti.  

Kwa mujibu wa taarifa za serikali, kiwango ambacho watu hutumiana ujumbe wenye mada ya ngono pamoja na picha za watu walio uchi, zao wenyewe au za mtu mwingine kwa simu zao za kisasa ilipanda hadi asilimia sitini.
Chanzo:BBC

Popular Posts

Labels