Serikali ya Tanzania imeomba mkopo wa Dola za Marekani milioni 154 ambazo ni takribani shilingi za kitanzania bilioni 246 kwa India kuwezesha ujenzi wa minara ya mawasiliano ya simu katika maeneo yasiyo na huduma hiyo,ambapo sh.bilioni 320 zinatarajiwa kutumika.
Tayari Serikali imeorodhesha maeneo yanayotakiwa kuwekewa minara na gharama zake ikiwa ni hatua ya kuwezesha kuanza utekelezaji wa ujenzi huo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia,January Makamba amesema bungeni jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Bukene,Selemani Zedi (CCM) aliyetaka kujua juhudi za Serikali kujenga minara katika sehemu zisizo na mawasiliano,hususani yasiyo na mvuto wa kibiashara.
Makamba pia amesema kupitia mfuko wa mawasiliano kwa wote ulioanzishwa na Wizara hiyo utasaidia kuharakisha kazi hiyo ya upelekaji huduma za mawasiliano.
Takwimu zilizotolewa na jana na Kampuni ya Simu ya Vodacom zinaonesha kwamba Kenya inaongoza kwa mawasiliano ya mawasiliano ya simu na intaneti kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ikifuatiwa na Tanzania,Uganda,Rwanda na Burundi.
Takwimu hizo zinaeleza kuwa julai mwaka jana Kenya yenye wakazi milioni 44,inawatumiaji wa simu za mkononi milioni 34.4 huku intaneti wakiwa ni milioni 16.3 sawa na asilimia 41.
Tanzania inafuata kwa kuwa na wakazi wapatao milioni 48.3 na watumiaji wa simu za mkononi ni milioni 27.4 na wanaotumia intaneti ni milioni 5.31 sawa na asilimia 11 tu
Friday, May 23, 2014
Popular Posts
-
Kikundi cha kihalifu mtandao cha # Anonymous kimetekeleza mashambulizi mtandao dhidi ya Nchi ya Angola na kufanikiwa kudukua na kua...
-
Huu ni mfululizo wa vipindi vya Serikali Mtandao hapa utaona kwa namna gani TANAPA inavyotumia TEHAMA katika utoaji huduma kwa umma.
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Watu wengi wameshaona filamu ambazo wahalifu wakidukua simu za mikononi hata kama zimezimwa. Kama ili...
-
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dr Ally Simba Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevitaka vituo vya redio na televi...
-
Na Yusuph Kileo Nchi ya Tanzania yabahatika tena kwa mara ya tatu kuwa mwenyeji wa mkutano wa “Connect 2 Connect” ambapo kauli mbiu ya...
-
Rais Barak Obama wa Marekani Serikali ya Marekani imekumbwa na udukuzi wa mtandao wa komputa ambapo taarifa bina...
-
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU KUVURUGA PROGRAMU YA WINXP 1 – PROGRAMU YA WIN XP KUVURUGIKA Sio ukweli kwamba programu ya win xp itavuruguka...
-
Imeelezwa kuwa wananachi wengi bado hawana uelewa wa kutosha juu ya haki zao za msingi katika huduma za mawasiliano wanazotumia, hali ambayo...
-
Recording video has become easier than ever with the growing number of smart phones and the recording function of digital still cameras. Fo...