Mtu mmoja ambaye alijitambulisha kwa cheo cha Katibu wa Usaili Idara ya Uhamiaji Dr Mawazo Kaburugu anatafutwa na idara hiyo kwa tuhuma za kutoza watu sh 10,000 kwa njia za udanganyifu.
Mtu huyo ambaye alifanikiwa kutuma ujumbe kwa watu zaidi ya 900,wanaotaka kufanyiwa usaili kwenye idara ya Uhamiaji,anadaiwa kupata kiasi kikubwa cha fedha kutokana na ujumbe aliokuwa akutuma kwa watu hao.
Ujumbe huo ulisomeka "Habari ndugu,pongezi kwa kuitwa kwenye usaili kuanzia tar 9/6.Idara ya uhamiaji inakufahamisha kuwa unatakiwa kulipa sh 10,000 na haitarejeshwa kama gharama za usaili vikiwamo vitambulisho pekee ndio wataruhusiwa kuingia ukumbini,malipo yote yatumwe kwa tigo pesa kwenye namba 0715 54 62 81 kuanzia tarehe 26 hadi 30,kisha tuma sms yenye code za Tigopesa na jina lako kamili,imetolewa na Kamishna Dr Mawazo Kaburugu Katibu wa Usaili".
Mwandishi wa gazeri la Raia Tanzania aliwasiliana na mtu huyo ambapo alieleza kuwa wote ambao wameitwa kwenye usaili watume fedha hiyo kama ujumbe ulivyotolewa na kuongeza kuwa pesa hiyo inahitajika haraka sana ili iweze kufanyakazi iliyokusudiwa kwa ajili ya usaili.
Kaimu Mtendaji wa Idara ya Uhamiaji,Tatu Bruani amesema mtu huyo ni tapeli na ambao wametumiwa ujumbe wasitume pesa hizo.
Chanzo:Gazeti la RaiaTanzania
Popular Posts
-
Watafiti toka kampuni ya utafiti ya Zscalar wamegundua kuwa,tovuti za kichina zenye picha za ngono zimekuwa zikisamb...
-
Over the years, Safer Internet Day (SID) has become a landmark event in the online safety calendar. Starting as an initiative of the EU ...
-
Mbunge wa Moshi vijijini,Philemon Ndesambulo (CHADEMA) amezushiwa kifo kutokana na baadhi ya watu kusambaza habari hizo kupitia ujumbe mfup...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Serikali kusambaza tabiti za kufundishia sekondari Yaanza kazi hiyo kwa kushirikiana na taasisi ya Marekani ya Opportunity Education Tr...
-
Wakati bado mafanikio mbali mbali yakijadiliwa wahalifu mtandao wamegundulika kuja na uhalifu unaotafsiriwa kuwa ni wa kihistoria na uliof...
-
Intaneti ni bahari kubwa yenye taarifa nyingi,kwa hiyo kupata taarifa unayoitafuta ni lazima uuelekeze utaratibu wa intaneti unaotafuta ma...
-
Katika ukurasa wake wa twitter Mhe Zitto Kabwe ametweet "Asanteni sana Wauza Mawese # TeamMawese leo kwenye uzinduzi wetu Kigoma Mj...