Mtu mmoja ambaye alijitambulisha kwa cheo cha Katibu wa Usaili Idara ya Uhamiaji Dr Mawazo Kaburugu anatafutwa na idara hiyo kwa tuhuma za kutoza watu sh 10,000 kwa njia za udanganyifu.
Mtu huyo ambaye alifanikiwa kutuma ujumbe kwa watu zaidi ya 900,wanaotaka kufanyiwa usaili kwenye idara ya Uhamiaji,anadaiwa kupata kiasi kikubwa cha fedha kutokana na ujumbe aliokuwa akutuma kwa watu hao.
Ujumbe huo ulisomeka "Habari ndugu,pongezi kwa kuitwa kwenye usaili kuanzia tar 9/6.Idara ya uhamiaji inakufahamisha kuwa unatakiwa kulipa sh 10,000 na haitarejeshwa kama gharama za usaili vikiwamo vitambulisho pekee ndio wataruhusiwa kuingia ukumbini,malipo yote yatumwe kwa tigo pesa kwenye namba 0715 54 62 81 kuanzia tarehe 26 hadi 30,kisha tuma sms yenye code za Tigopesa na jina lako kamili,imetolewa na Kamishna Dr Mawazo Kaburugu Katibu wa Usaili".
Mwandishi wa gazeri la Raia Tanzania aliwasiliana na mtu huyo ambapo alieleza kuwa wote ambao wameitwa kwenye usaili watume fedha hiyo kama ujumbe ulivyotolewa na kuongeza kuwa pesa hiyo inahitajika haraka sana ili iweze kufanyakazi iliyokusudiwa kwa ajili ya usaili.
Kaimu Mtendaji wa Idara ya Uhamiaji,Tatu Bruani amesema mtu huyo ni tapeli na ambao wametumiwa ujumbe wasitume pesa hizo.
Chanzo:Gazeti la RaiaTanzania
Popular Posts
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome akizungumza kabla ya kuzindua rasmi maonesho ya Tehama yanayoend...
-
Yusuph Kileo baada ya kukabidhiwa tuzo Mtaalamu wa masuala ya usalama mtandaoni Yusu ph Kileo hivi karibuni alipata Tunzo ya ...
-
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia imesema gharama za kupiga simu kutoka mtandao wa kampuni moja ya s...
-
Kampuni ya magari ya Fiat Chrysler kutoka Marekani imeyarudisha magari yake yapatayo milioni 1.4 baada ya watafiti wa usalama kuony...
-
Watumiaji wa programu ya komputa iitwayo Window XP wamepewa tahadhari na kampuni ya Microsoft ambayo ndiyo iliyotengeneza program hiyo ...
-
Na Brown Nyanza Wanasayansi wawili katika nchi ya Ujerumani wamegundua kalamu inayotoa alama pindi mwandishi anapokosea heruf...
-
Mkuu Kituo cha Teknohama cha Ushirikiano wa India na Tanzania (DIT), Dr. Amos Nungu akiwakaribisha wafanyakazi wa Shirika la Umoja w...