Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imeleza kuwa imenufaika na utaratibu mpya wa utaratibu wa ulipaji wa kodi kwa kutumia huduma ya simu za
mkononi na Max-malipo.
Taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Kinondoni Sebastian Modestus Mhowera imeeleza kuwa huduma hiyo mpya inayotolewa kupitia mfumo unaojulikana kama “e–payment system”,ambao unamwezesha mwananchi kulipa kodi yake muda wowote, kwa haraka na urahisi na mahali popote.
Huduma
hii inatolewa na Manispaa kwa kushirikiana na wakala anayetambulika
kama “Max-malipo” ambaye kupitia huduma zake mitaa 171 iliyopo katika
Kata 34 imeunganishwa katika mifumo hiyo ya ulipaji kodi.
Mfumo huu
wa ukusanyaji wa kodi ndani ya Manispaa ni hatua ya utekelezaji
unaozingatia maelekezo ya waraka wa Serikali Na. 5 wa mwaka 2009
unaohamasisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA)
kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa Umma, kwa ufanisi na kwa
wakati.
Taarifa inaeleza kuwa manispaa hiyo iliona ni vema ikaingia katika utaratibu huu ili mwananchi aweze kulipia kodi popote
kwa kutumia Max-malipo au wakala wa simu za mkononi yaani Tigo pesa Na.
212888 na M-Pesa Na. 212888.
Katika
kipindi kifupi cha muda wa miezi 3, tangu mfumo huu mpya ulipoanzishwa
rasmi kumekuwa na
• Ongezeko la ada ya kuchangia huduma za Afya
(Cost sharing) imeongezeka kutoka Tshs. 45,000,000/= kwa wiki hadi
kufikia Tshs. 65,000,000/= kwa wiki, sawa na ongezeko la 69%
•
Chanzo cha kodi ya majengo hadi mwishoni mwa Machi zilikusanywa Tshs.
339,000,000/= tofauti na awali ambapo hadi kipindi kama mwaka 2013 zilikuwa kwa ongezeko la asilimia 269 hiki Tshs. 126,000,000/=
•
Maeneo mengine ongezeko la mapato limezidi bajeti ya mwaka iliyotakiwa
kukusanywa. Kwa mfano katika ushuru wa huduma za jiji (City Service
Kavy) ambapo tumezidi kwa 18%
• Ushuru wa Masoko umeongezeka kwa wastani wa asilimia 20 ya lengo la kila mwezi.
•
Lesseni za biashara hadi Machi zilikusanywa shs. 2.4 Bilioni sawa na
93% ya bajeti ya Manispaa ya chanzo hiki ya shilingi. 2.6 Bilioni kwa mwaka.
Saturday, May 3, 2014
Popular Posts
-
Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) kupitia Mkurugenzi wake Mkuu Profesa John Nkoma imesema namba za simu zilizosajiliwa nchini hu...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
Serikali kusambaza tabiti za kufundishia sekondari Yaanza kazi hiyo kwa kushirikiana na taasisi ya Marekani ya Opportunity Education Tr...
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...