Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imeleza kuwa imenufaika na utaratibu mpya wa utaratibu wa ulipaji wa kodi kwa kutumia huduma ya simu za
mkononi na Max-malipo.
Taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Kinondoni Sebastian Modestus Mhowera imeeleza kuwa huduma hiyo mpya inayotolewa kupitia mfumo unaojulikana kama “e–payment system”,ambao unamwezesha mwananchi kulipa kodi yake muda wowote, kwa haraka na urahisi na mahali popote.
Huduma
hii inatolewa na Manispaa kwa kushirikiana na wakala anayetambulika
kama “Max-malipo” ambaye kupitia huduma zake mitaa 171 iliyopo katika
Kata 34 imeunganishwa katika mifumo hiyo ya ulipaji kodi.
Mfumo huu
wa ukusanyaji wa kodi ndani ya Manispaa ni hatua ya utekelezaji
unaozingatia maelekezo ya waraka wa Serikali Na. 5 wa mwaka 2009
unaohamasisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA)
kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa Umma, kwa ufanisi na kwa
wakati.
Taarifa inaeleza kuwa manispaa hiyo iliona ni vema ikaingia katika utaratibu huu ili mwananchi aweze kulipia kodi popote
kwa kutumia Max-malipo au wakala wa simu za mkononi yaani Tigo pesa Na.
212888 na M-Pesa Na. 212888.
Katika
kipindi kifupi cha muda wa miezi 3, tangu mfumo huu mpya ulipoanzishwa
rasmi kumekuwa na
• Ongezeko la ada ya kuchangia huduma za Afya
(Cost sharing) imeongezeka kutoka Tshs. 45,000,000/= kwa wiki hadi
kufikia Tshs. 65,000,000/= kwa wiki, sawa na ongezeko la 69%
•
Chanzo cha kodi ya majengo hadi mwishoni mwa Machi zilikusanywa Tshs.
339,000,000/= tofauti na awali ambapo hadi kipindi kama mwaka 2013 zilikuwa kwa ongezeko la asilimia 269 hiki Tshs. 126,000,000/=
•
Maeneo mengine ongezeko la mapato limezidi bajeti ya mwaka iliyotakiwa
kukusanywa. Kwa mfano katika ushuru wa huduma za jiji (City Service
Kavy) ambapo tumezidi kwa 18%
• Ushuru wa Masoko umeongezeka kwa wastani wa asilimia 20 ya lengo la kila mwezi.
•
Lesseni za biashara hadi Machi zilikusanywa shs. 2.4 Bilioni sawa na
93% ya bajeti ya Manispaa ya chanzo hiki ya shilingi. 2.6 Bilioni kwa mwaka.
Saturday, May 3, 2014
Popular Posts
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya ...
-
Watu wanne huko nchini Marekani wameushitaki mtandao wa kijamii wa LinkedIn unaowaunganisha wanataaluma kuwa umekuwa ukii...
-
Facebook imekuwa kama Google ya mitandao ya kijamii. kama sasa hivi hauposti status yako basi unapandisha picha au unajibu quiz ...
-
Kwa watumiaji wa Facebook na mitandao jamii mingine jaribuni kuwa makini na kile mnachokiweka ama kutoa maoni katika suala lolote kwenye kur...
-
Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa Wizara ya Sheria nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kwa kile kinachosemekana ni ufichuaj...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
Akaunti ya Twitter ya kundi la wanamgambo wa Al Shabaab imesitishwa kwa mara nyingine. Ujumbe kutoka kwa Twitter katika akaunti yake ...