Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imeleza kuwa imenufaika na utaratibu mpya wa utaratibu wa ulipaji wa kodi kwa kutumia huduma ya simu za
mkononi na Max-malipo.
Taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Kinondoni Sebastian Modestus Mhowera imeeleza kuwa huduma hiyo mpya inayotolewa kupitia mfumo unaojulikana kama “e–payment system”,ambao unamwezesha mwananchi kulipa kodi yake muda wowote, kwa haraka na urahisi na mahali popote.
Huduma
hii inatolewa na Manispaa kwa kushirikiana na wakala anayetambulika
kama “Max-malipo” ambaye kupitia huduma zake mitaa 171 iliyopo katika
Kata 34 imeunganishwa katika mifumo hiyo ya ulipaji kodi.
Mfumo huu
wa ukusanyaji wa kodi ndani ya Manispaa ni hatua ya utekelezaji
unaozingatia maelekezo ya waraka wa Serikali Na. 5 wa mwaka 2009
unaohamasisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA)
kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa Umma, kwa ufanisi na kwa
wakati.
Taarifa inaeleza kuwa manispaa hiyo iliona ni vema ikaingia katika utaratibu huu ili mwananchi aweze kulipia kodi popote
kwa kutumia Max-malipo au wakala wa simu za mkononi yaani Tigo pesa Na.
212888 na M-Pesa Na. 212888.
Katika
kipindi kifupi cha muda wa miezi 3, tangu mfumo huu mpya ulipoanzishwa
rasmi kumekuwa na
• Ongezeko la ada ya kuchangia huduma za Afya
(Cost sharing) imeongezeka kutoka Tshs. 45,000,000/= kwa wiki hadi
kufikia Tshs. 65,000,000/= kwa wiki, sawa na ongezeko la 69%
•
Chanzo cha kodi ya majengo hadi mwishoni mwa Machi zilikusanywa Tshs.
339,000,000/= tofauti na awali ambapo hadi kipindi kama mwaka 2013 zilikuwa kwa ongezeko la asilimia 269 hiki Tshs. 126,000,000/=
•
Maeneo mengine ongezeko la mapato limezidi bajeti ya mwaka iliyotakiwa
kukusanywa. Kwa mfano katika ushuru wa huduma za jiji (City Service
Kavy) ambapo tumezidi kwa 18%
• Ushuru wa Masoko umeongezeka kwa wastani wa asilimia 20 ya lengo la kila mwezi.
•
Lesseni za biashara hadi Machi zilikusanywa shs. 2.4 Bilioni sawa na
93% ya bajeti ya Manispaa ya chanzo hiki ya shilingi. 2.6 Bilioni kwa mwaka.
Saturday, May 3, 2014
Popular Posts
-
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU KUVURUGA PROGRAMU YA WINXP 1 – PROGRAMU YA WIN XP KUVURUGIKA Sio ukweli kwamba programu ya win xp itavuruguka...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Mwishoni mwa juma lililopita pamegundulika hali mbaya ya kiusalama mtandao itakayo waathiri watumiaji wa kivinjari kijulikanacho kama...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
Pr. T. G NG katibu mkuu wa kanisa la Waadventista duniani akifungua mkutano wa Adventist Church Management System, February 10, 2014...
-
Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi akitoa zawadi kwa washindi wa tweet bora kwa mwezi wa nane Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ardhi Lilian Wils...
-
Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ,Bw Charles Kitwanga ameyashawishi mataifa ambayo tayari yamejiunga na mfumo wa Digitali katika haraka...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kuzingatia kifungu 5 (b) na (e) cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya 2003 inatoa t...