Vyombo vya habari vinapasha kuwa, Maafisa nchini Ujerumani
wanawashikilia Wajerumani wawili wanaoshukiwa kuifanyia ujasusi na
kufanikisha kupenyeza taarifa za siri kwa maafisa wa Marekani, kwa
hiyari yao wenyewe.
Steffen Seibert, Msemaji wa Chancellor Angela Merkel, amekiri
kutaarifiwa kuhusu suala hilo lililotokea Jumatano ya wiki hii na kusema
kuwa Chancellor Merkel alizungumza na Rais wa Marekani, Barack Obama
siku ya Alhamisi (ijapokuwa
hakusema ni kipi kilikuwa kiini cha mazungumzo hayo).
Uhusiano baina ya mataifa haya mawili makubwa kiuchumi Duniani
umetikiswa kutokana na kuvuja kwa siri za shirika (NSA) lililokuwa
likidukua taarifa za mawasiliano nyeti duniani ikiwepo ya Wajerumani na
kiongozi wao, Merkel.
Inasadikiwa kuwa mmoja wa waliotiwa mbaroni ni kijana wa umri wa miaka
31, mwajiriwa wa idara ya kiitelijensia ya mambo ya nje ya Ujerumani,
aliyenyakua nyaraka za siri 218, ambazo aliziuza kwa $34,000 na kutuma
taarifa za Bunge la Ujerumani (Bundestag) kuhusu udadisi wa aina ya
maswali yanayokusudiwa kuulizwa ili kupata majibu kuhusu udukuzi wa
NSA/Marekani kwa Ujerumani.
Awali, mtuhumiwa huyo alikamatwa kwa kuhisiwa kuwa anafanyia ujasusi
nchi ya Urusi lakini baadaye alikaririwa na chombo kimoja cha habari cha
nchini Ujerumani kuwa alikiri kufanyia Marekani ujasusi.
Mtuhumiwa alifikishwa katika korti kuu huko Ujerumani na kuamuriwa
kushikiliwa kwa dharura kwa kuwa na nyaraka za kiitelijensia bila ruhusa
maalumu.
Chanzo:http://www.wavuti.com
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...