Vyombo vya habari vinapasha kuwa, Maafisa nchini Ujerumani
wanawashikilia Wajerumani wawili wanaoshukiwa kuifanyia ujasusi na
kufanikisha kupenyeza taarifa za siri kwa maafisa wa Marekani, kwa
hiyari yao wenyewe.
Steffen Seibert, Msemaji wa Chancellor Angela Merkel, amekiri
kutaarifiwa kuhusu suala hilo lililotokea Jumatano ya wiki hii na kusema
kuwa Chancellor Merkel alizungumza na Rais wa Marekani, Barack Obama
siku ya Alhamisi (ijapokuwa
hakusema ni kipi kilikuwa kiini cha mazungumzo hayo).
Uhusiano baina ya mataifa haya mawili makubwa kiuchumi Duniani
umetikiswa kutokana na kuvuja kwa siri za shirika (NSA) lililokuwa
likidukua taarifa za mawasiliano nyeti duniani ikiwepo ya Wajerumani na
kiongozi wao, Merkel.
Inasadikiwa kuwa mmoja wa waliotiwa mbaroni ni kijana wa umri wa miaka
31, mwajiriwa wa idara ya kiitelijensia ya mambo ya nje ya Ujerumani,
aliyenyakua nyaraka za siri 218, ambazo aliziuza kwa $34,000 na kutuma
taarifa za Bunge la Ujerumani (Bundestag) kuhusu udadisi wa aina ya
maswali yanayokusudiwa kuulizwa ili kupata majibu kuhusu udukuzi wa
NSA/Marekani kwa Ujerumani.
Awali, mtuhumiwa huyo alikamatwa kwa kuhisiwa kuwa anafanyia ujasusi
nchi ya Urusi lakini baadaye alikaririwa na chombo kimoja cha habari cha
nchini Ujerumani kuwa alikiri kufanyia Marekani ujasusi.
Mtuhumiwa alifikishwa katika korti kuu huko Ujerumani na kuamuriwa
kushikiliwa kwa dharura kwa kuwa na nyaraka za kiitelijensia bila ruhusa
maalumu.
Chanzo:http://www.wavuti.com
Popular Posts
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya ...
-
Watu wanne huko nchini Marekani wameushitaki mtandao wa kijamii wa LinkedIn unaowaunganisha wanataaluma kuwa umekuwa ukii...
-
Facebook imekuwa kama Google ya mitandao ya kijamii. kama sasa hivi hauposti status yako basi unapandisha picha au unajibu quiz ...
-
Kwa watumiaji wa Facebook na mitandao jamii mingine jaribuni kuwa makini na kile mnachokiweka ama kutoa maoni katika suala lolote kwenye kur...
-
Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa Wizara ya Sheria nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kwa kile kinachosemekana ni ufichuaj...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
Akaunti ya Twitter ya kundi la wanamgambo wa Al Shabaab imesitishwa kwa mara nyingine. Ujumbe kutoka kwa Twitter katika akaunti yake ...