Vyombo vya habari vinapasha kuwa, Maafisa nchini Ujerumani
wanawashikilia Wajerumani wawili wanaoshukiwa kuifanyia ujasusi na
kufanikisha kupenyeza taarifa za siri kwa maafisa wa Marekani, kwa
hiyari yao wenyewe.
Steffen Seibert, Msemaji wa Chancellor Angela Merkel, amekiri
kutaarifiwa kuhusu suala hilo lililotokea Jumatano ya wiki hii na kusema
kuwa Chancellor Merkel alizungumza na Rais wa Marekani, Barack Obama
siku ya Alhamisi (ijapokuwa
hakusema ni kipi kilikuwa kiini cha mazungumzo hayo).
Uhusiano baina ya mataifa haya mawili makubwa kiuchumi Duniani
umetikiswa kutokana na kuvuja kwa siri za shirika (NSA) lililokuwa
likidukua taarifa za mawasiliano nyeti duniani ikiwepo ya Wajerumani na
kiongozi wao, Merkel.
Inasadikiwa kuwa mmoja wa waliotiwa mbaroni ni kijana wa umri wa miaka
31, mwajiriwa wa idara ya kiitelijensia ya mambo ya nje ya Ujerumani,
aliyenyakua nyaraka za siri 218, ambazo aliziuza kwa $34,000 na kutuma
taarifa za Bunge la Ujerumani (Bundestag) kuhusu udadisi wa aina ya
maswali yanayokusudiwa kuulizwa ili kupata majibu kuhusu udukuzi wa
NSA/Marekani kwa Ujerumani.
Awali, mtuhumiwa huyo alikamatwa kwa kuhisiwa kuwa anafanyia ujasusi
nchi ya Urusi lakini baadaye alikaririwa na chombo kimoja cha habari cha
nchini Ujerumani kuwa alikiri kufanyia Marekani ujasusi.
Mtuhumiwa alifikishwa katika korti kuu huko Ujerumani na kuamuriwa
kushikiliwa kwa dharura kwa kuwa na nyaraka za kiitelijensia bila ruhusa
maalumu.
Chanzo:http://www.wavuti.com
Popular Posts
-
Serikali ya Tanzania inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa hivi karibuni kumezuka kundi la Watu wadanganyifu ambao wamekuwa wakit...
-
Serikali ya Kenya imesema watu watakaopatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kingono kwa kutumia simu za kiganjani na intaneti watafungw...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Yusuph Kileo baada ya kukabidhiwa tuzo Mtaalamu wa masuala ya usalama mtandaoni Yusu ph Kileo hivi karibuni alipata Tunzo ya ...
-
Maofisa wa WAMOJA ICT Consulting Limited Mtangazaji Maduhu na WAMOJA ICT Consulting Limited Kampuni ya WAMOJA ICT Consulting Li...
-
Utafiti uliofanywa mwaka jana na Kampuni ya Utengenezaji wa simu ya Nokia kabla haijabadilishwa na kuwa Microsoft kuhusu biashara ya m...
-
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia imesema gharama za kupiga simu kutoka mtandao wa kampuni moja ya s...