Vyombo vya habari vinapasha kuwa, Maafisa nchini Ujerumani
wanawashikilia Wajerumani wawili wanaoshukiwa kuifanyia ujasusi na
kufanikisha kupenyeza taarifa za siri kwa maafisa wa Marekani, kwa
hiyari yao wenyewe.
Steffen Seibert, Msemaji wa Chancellor Angela Merkel, amekiri
kutaarifiwa kuhusu suala hilo lililotokea Jumatano ya wiki hii na kusema
kuwa Chancellor Merkel alizungumza na Rais wa Marekani, Barack Obama
siku ya Alhamisi (ijapokuwa
hakusema ni kipi kilikuwa kiini cha mazungumzo hayo).
Uhusiano baina ya mataifa haya mawili makubwa kiuchumi Duniani
umetikiswa kutokana na kuvuja kwa siri za shirika (NSA) lililokuwa
likidukua taarifa za mawasiliano nyeti duniani ikiwepo ya Wajerumani na
kiongozi wao, Merkel.
Inasadikiwa kuwa mmoja wa waliotiwa mbaroni ni kijana wa umri wa miaka
31, mwajiriwa wa idara ya kiitelijensia ya mambo ya nje ya Ujerumani,
aliyenyakua nyaraka za siri 218, ambazo aliziuza kwa $34,000 na kutuma
taarifa za Bunge la Ujerumani (Bundestag) kuhusu udadisi wa aina ya
maswali yanayokusudiwa kuulizwa ili kupata majibu kuhusu udukuzi wa
NSA/Marekani kwa Ujerumani.
Awali, mtuhumiwa huyo alikamatwa kwa kuhisiwa kuwa anafanyia ujasusi
nchi ya Urusi lakini baadaye alikaririwa na chombo kimoja cha habari cha
nchini Ujerumani kuwa alikiri kufanyia Marekani ujasusi.
Mtuhumiwa alifikishwa katika korti kuu huko Ujerumani na kuamuriwa
kushikiliwa kwa dharura kwa kuwa na nyaraka za kiitelijensia bila ruhusa
maalumu.
Chanzo:http://www.wavuti.com
Popular Posts
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya iOS 12.2 kwa ajili ya iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivy...
-
Baraza la Sanaa la Taifa nchini Tanzania (BASATA) limetoa siku saba kwa wasanii,vituo vya radio,runinga wamiliki wa tovuti na wa...
-
Facebook is developing a new smartphone app to track the location of users in an effort to target them with localised adverts, acc...
-
Tokea LAPTOP zimeanza kuingia sokoni zimekua sehemu ya maisha yetu ya kila siku . Mwanzoni hazikua zinapendeza sana , Kubwa na Gha...
-
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yussuf Mwenda akibofya kompyuta kuzindua huduma ya WiFi ya bure kwenye Kituo cha Mabasi cha Sinza, wi...
-
Wakati ugonjwa wa Ebola ukiendelea kuwa tishio katika baadhi ya nchi za Afrika magharibi, Wataalam wa afya nao wameendelea kuweka jitih...
-
Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Tekinolojia nchini Tanzania imeahidi kutoa msaada kwa shirika la posta nchini humo ili liweze kuwa shi...