Friday, July 3, 2015
TTCL YAJA NA HUDUMA YA INTANET YA SATELAITI
Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), imeendelea kukuza matumizi ya mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) nchini Tanzania ambapo kupitia kipindi cha msimu wa Sabasaba imeleta teknolojia ambayo itasaidia kampuni, taasisi na ofisi za Serikali ambazo ziko mbali na njia ya Mkongo wa Taifa kupatiwa mawasiliano ya intaneti kwa njia ya satelaiti.
Akizungumza na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam kwenye Maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa, katika viwanja vya Sabasaba, Ofisa kutoka TTCL, Fredrick Benard amesema teknolojia hiyo ni muhimu kwa kampuni na kwamba ina ubora, uhakika na kwa bei nafuu.
Benald amesema ili kupata huduma ya intaneti kwa njia ya setelaiti, mteja atapaswa kupeleka maombi rasmi ya huduma anayoitaka na baadaye atapelekewa tathmini ya gharama ya kuunganishiwa.
Aidha amesema, kampuni iliamua kupeleka huduma hiyo kutokana na mahitaji makubwa ya matumizi ya intaneti kwa shughuli za maendeleo.
Popular Posts
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya ...
-
Watu wanne huko nchini Marekani wameushitaki mtandao wa kijamii wa LinkedIn unaowaunganisha wanataaluma kuwa umekuwa ukii...
-
Facebook imekuwa kama Google ya mitandao ya kijamii. kama sasa hivi hauposti status yako basi unapandisha picha au unajibu quiz ...
-
Kwa watumiaji wa Facebook na mitandao jamii mingine jaribuni kuwa makini na kile mnachokiweka ama kutoa maoni katika suala lolote kwenye kur...
-
Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa Wizara ya Sheria nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kwa kile kinachosemekana ni ufichuaj...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
Akaunti ya Twitter ya kundi la wanamgambo wa Al Shabaab imesitishwa kwa mara nyingine. Ujumbe kutoka kwa Twitter katika akaunti yake ...