Friday, July 3, 2015
TTCL YAJA NA HUDUMA YA INTANET YA SATELAITI
Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), imeendelea kukuza matumizi ya mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) nchini Tanzania ambapo kupitia kipindi cha msimu wa Sabasaba imeleta teknolojia ambayo itasaidia kampuni, taasisi na ofisi za Serikali ambazo ziko mbali na njia ya Mkongo wa Taifa kupatiwa mawasiliano ya intaneti kwa njia ya satelaiti.
Akizungumza na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam kwenye Maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa, katika viwanja vya Sabasaba, Ofisa kutoka TTCL, Fredrick Benard amesema teknolojia hiyo ni muhimu kwa kampuni na kwamba ina ubora, uhakika na kwa bei nafuu.
Benald amesema ili kupata huduma ya intaneti kwa njia ya setelaiti, mteja atapaswa kupeleka maombi rasmi ya huduma anayoitaka na baadaye atapelekewa tathmini ya gharama ya kuunganishiwa.
Aidha amesema, kampuni iliamua kupeleka huduma hiyo kutokana na mahitaji makubwa ya matumizi ya intaneti kwa shughuli za maendeleo.
Popular Posts
-
Mwishoni mwa juma lililopita pamegundulika hali mbaya ya kiusalama mtandao itakayo waathiri watumiaji wa kivinjari kijulikanacho kama...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU KUVURUGA PROGRAMU YA WINXP 1 – PROGRAMU YA WIN XP KUVURUGIKA Sio ukweli kwamba programu ya win xp itavuruguka...
-
Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi akitoa zawadi kwa washindi wa tweet bora kwa mwezi wa nane Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ardhi Lilian Wils...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ,Bw Charles Kitwanga ameyashawishi mataifa ambayo tayari yamejiunga na mfumo wa Digitali katika haraka...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kuzingatia kifungu 5 (b) na (e) cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya 2003 inatoa t...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Tokea LAPTOP zimeanza kuingia sokoni zimekua sehemu ya maisha yetu ya kila siku . Mwanzoni hazikua zinapendeza sana , Kubwa na Gha...