Friday, July 3, 2015
TTCL YAJA NA HUDUMA YA INTANET YA SATELAITI
Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), imeendelea kukuza matumizi ya mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) nchini Tanzania ambapo kupitia kipindi cha msimu wa Sabasaba imeleta teknolojia ambayo itasaidia kampuni, taasisi na ofisi za Serikali ambazo ziko mbali na njia ya Mkongo wa Taifa kupatiwa mawasiliano ya intaneti kwa njia ya satelaiti.
Akizungumza na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam kwenye Maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa, katika viwanja vya Sabasaba, Ofisa kutoka TTCL, Fredrick Benard amesema teknolojia hiyo ni muhimu kwa kampuni na kwamba ina ubora, uhakika na kwa bei nafuu.
Benald amesema ili kupata huduma ya intaneti kwa njia ya setelaiti, mteja atapaswa kupeleka maombi rasmi ya huduma anayoitaka na baadaye atapelekewa tathmini ya gharama ya kuunganishiwa.
Aidha amesema, kampuni iliamua kupeleka huduma hiyo kutokana na mahitaji makubwa ya matumizi ya intaneti kwa shughuli za maendeleo.
Popular Posts
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...