Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania TCRA Imewataka wananchi wa mikoa ya Tabora na Singida kuepukana na dhana potofu ya matumizi ya televisheni walizonazo kuwa hazitumiki katika matangazo ya kidijiti bali waendelee na televisheni zao kwani king’amuzi hakina luninga maalum.
Hayo yamebainishwa na Naibu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano na Utangazaji nchini Tanzania Bwana Fredrick Ntobi wakati akitoa taarifa ya kuzima mitambo ya analojia ifikapo tarehe 31 machi mwaka huu itakayohusisha maeneo ya mikoa hiyo.
Ntobi amesema kuwa utaratibu wa kuzima mitambo ya analojia utakuwa kwenye mitambo ya maeneo ya dijitali ambapo watoa huduma za kusambaza ving’amuzi walioko Tabora kuhakikisha kuwa kuna ving’amuzi vya kutosha.
Aidha wananchi wa mkoa Tabora wasizitupe tv zao za analojia bali wanunue ving’amuzi ili kupata matangazo ya kidijitali.
Hata hivyo wakizungumza na vyombo vya habari baadhi ya wananchi wa mkoa wa Tabora wameonesha wasiwasi wao kuhusu mfumo mpya wa kidijitali wa upataji wa matangazo ya televisheni kwa kuwa watu wengi bado hawajanunua ving’amuzi na ambao wamenunua wanalamika kuwa baadhi ya chaneli hawazipati.
Thursday, March 27, 2014
Popular Posts
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome akizungumza kabla ya kuzindua rasmi maonesho ya Tehama yanayoend...
-
Yusuph Kileo baada ya kukabidhiwa tuzo Mtaalamu wa masuala ya usalama mtandaoni Yusu ph Kileo hivi karibuni alipata Tunzo ya ...
-
Kampuni ya magari ya Fiat Chrysler kutoka Marekani imeyarudisha magari yake yapatayo milioni 1.4 baada ya watafiti wa usalama kuony...
-
Watumiaji wa programu ya komputa iitwayo Window XP wamepewa tahadhari na kampuni ya Microsoft ambayo ndiyo iliyotengeneza program hiyo ...
-
Na Brown Nyanza Wanasayansi wawili katika nchi ya Ujerumani wamegundua kalamu inayotoa alama pindi mwandishi anapokosea heruf...
-
Mkuu Kituo cha Teknohama cha Ushirikiano wa India na Tanzania (DIT), Dr. Amos Nungu akiwakaribisha wafanyakazi wa Shirika la Umoja w...