Kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu imependekeza kwa serikali iongeze adhabu ya faini kutoka shilingi milioni tatu na kifungo kisichopungua miezi sita na kuwa faini ya shilingi milioni tano na kifungo kisichopungua miezi sita kwa wale wote watakaotuma katika mtandao taarifa za uongo.
Aidha kamati hiyo ilipendekeza katika adhabu kwa watu wanaonyanyasa wenzao kupitia mtandaoni adhabu yao iongezwe kutoka kifungo cha cha mwaka mmoja na kuwa kifungo cha miaka mitano.
Awali akiwasilisha maelezo ya muswada huo,Waziri wa Mawasilino,Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa alisema kutokana na kukua kwa matumizi ya teknolojia ya Habari na Mawasiliano kumesababisha kuwepo kwa changamoto mbalimbali ikiwemo kuibuka kwa makosa ya mtandao.
Alitaja makosa ya mtandao yaliyokithiri kwa sasa kuwa ni makosa dhidi ya faragha,usalamana upatikanaji wa taarifa za kompyuta na mifumo ya kompyuta,makosa yanayohusu maudhui,makosa dhidi ya mifumo ya kompyuta na makosa ya kawaida yanayofanywa kwa kutumia mitandao.
Profesa Mbarawa alisema kuwa takwimu kutoka jeshi la polisi zinaonesha kuwa makosa ya uhalifu wa mtandao yaliyoripotiwa na kuchunguzwa kati ya mwaka 2012 hadi Agosti mwaka jana ni 400.
Alisema katika kipindi cha mwaka 2000 hadi mwaka 2013,makosa ya uhalifu wa mitandao yalisababisha hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 9.8 kwenye taasisi za fedha.
Thursday, April 2, 2015
Popular Posts
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Facebook is developing a new smartphone app to track the location of users in an effort to target them with localised adverts, acc...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Huenda umekuwa ukitumia intaneti na hasa mitandao ya kijamii ya Facebook, Twitter, Google+,LinkedIn na mingine mingi na umeona unataka kuji...
-
Huduma ya ujumbe Whatsapp imetangaza kuwa itayalinda mawasiliano ya wateja wake kuanzia hapo siku ya Jumanne April 5,mwaka huu Huk...
-
UDUKUZI NI NINI ? Ni uchukuaji wa taarifa za mwingine kwa njia ambazo sio halali kwa kutumia vyombo vya mawasiliano anavyotumia mtu hu...
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...