Raia watatu kutoka Pakstani wamehukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kulipa faini ya shilingi milioni 120 na iwapo watashindwa watatumikia kifungo cha mwaka mmoja jela kutokana na kosa la kula njama,kuingiza nchi Tanzania vifaa vya kielektroniki vya mawasiliano bila kuwa na leseni ya TCRA,kuvisimika,kuendesha huduma za mawasiliano ya simu za kimataifa bila kibali kutoka TCRA,kukwepa malipo na kusababishia serikali na mamlaka hiyo hasara ya shilingi milioni 140,049,000.
Raia hao wa Pakstani ni Hafeez Irfan (32),Mirza Baig (41) na Irfan Baig (46) na wakidaiwa kutenda makosa hayo katika Hoteli ya Butterfly iliyoko Kariakoo,Wilaya ya Ilala katika chumba namba 905.
Thursday, November 3, 2016
DAR ES SALAAM:RAIA WATATU WA PAKSTANI WAHUKUMIWA KWA KOSA LA KUMILIKI MITAMBO YA MAWASILIANO BILA LESENI
Popular Posts
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania TCRA Imewataka wananchi wa mikoa ya Tabora na Singida kuepukana na dhana potofu ya matumizi ya televi...
-
Serikali ya Tanzania imeomba mkopo wa Dola za Marekani milioni 154 ambazo ni takribani shilingi za kitanzania bilioni 246 kwa India kuwezesh...