Friday, November 1, 2013

KARIBIA NUSU YA MAPATO YA MATANGAZO YA BIASHARA YA FACEBOOK YANATOKA KATIKA SIMU ZA MIKONONI


Facebook imeeleza juma hili kuwa ilipata mapato ya jumla ya dola za kimarekani bilioni 1.8 kutokana na matangazo ya biashara, ambapo asilimia 44 kati ya asilimia 49 ya matangazo yanatoka katika simu za mikononi katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2013.

Katika robo ya tatu mwaka 2012 facebook ilipata asilimia 14 tu kutokana na matangazo ya kwenye simu za mikononi.

Takwimu zinaonesha kuwa watu milioni 874 wenye simu za mkononi wanatumia mtandao wa facebook kwa mwezi,na kuna ongezeko la asilimia 45 mwaka hadi mwaka na kubaki kuwa mtandao wa kijamii unaotumiwa na watu wengi ambapo kila mwezi hutumiwa na zaidi ya watu milioni 1.19 duniani.


Popular Posts

Labels