Saturday, November 2, 2013

NAMNA UNAVYOWEZA KUFUTA TAARIFA ZAKO KWENYE MITANDAO NA TOVUTI MBALIMBALI

Huenda umekuwa ukitumia intaneti na hasa mitandao ya kijamii ya Facebook, Twitter, Google+,LinkedIn na mingine mingi na umeona unataka kujiondoa kabisa ama kuondoa kabisa taarifa zako zisiendelee kuonekana katika mitandao hiyo kuna njia chache za kuweza kufuata.
How to Erase Yourself From the Internet
Hii ni njia ya kufuta taarifa zako kwenye facebook

Facebook

Facebook imeweka njia ambayo iko wazi kuonekana kwa kila mtumiaji ambaye anataka kujiondoa kwenye mtandao huo nayo ni kusitisha yaani kudeactivate ambayo unaweza kuipata kwenye  Account Settings > Security > Deactivate your account. Usidanganyike siyo kwamba inaondoa taarifa zako bali inazitunza taarifa zako ili unapobadilisha uamuzi wa kurudi tena uzipate taarifa hizo. 

Kama unataka kweli kuondoa taarifa zako basi unahitaji kulogin kwenye wasifu wako kisha bofya  Delete My Account na baada ya hapo bofya kibox cha bluu hapo utakuwa umeondoa kila kitu kwenye mtandao wa kijamii wa facebook na huwezi kuzirudisha tena japo itabidi usubiri baada ya siku 40 zitakuwa zimeondolewa kabisa .

Japo kabla ya kufanya inakupasa uhamishe taarifa zako na mambo yote kwenye tarakirishi yako kwa kufanya hatua zifuatazo Account Settings > General > Download a copy of your Facebook Data > Start My Archive.

Twitter

Kama ilivyo kwenye facebook ,katika mtandao wa  Twitter deactivate ina maanisha ondoa ama futa,ni rahisi sana nenda  Account Settings > Deactivate my account > Okay, fine, deactivate account. na hapo weka neno lako la siri imemalizika.
Twitter nayo hutunza kumbukumbu zako kwa siku 30 ikiwa utabadilisha uamuzi utazikuta taarifa zako,usipofanya hivyo baada ya muda huo zitakuwa zimeondolewa 

 How to Erase Yourself From the Internet
 Hiyo ni baadhi ya mifano ya kuondoa taarifa zako katika tovuti ya accountkiller.com inatoa maelezo ya mbinu mbalimbali za kufuta taarifa zako katika mitandao mbalimbali ya kijamii 









Popular Posts

Labels