Friday, January 31, 2014
MAKAMPUNI YA MITANDAO YA SIMU NCHINI MAREKANI KUFANYA UTAFITI WA NAMBA ZA SIMU KUWA IP
Natumaini umeshawahi kusikia ama unafahamu kuhusu teknolojia ya kusafirisha mawimbi ya sauti kwa njia ya intaneti ( VoIP) ambayo si teknolojia mpya.
Kamisheni ya Shirikisho la Mawasiliano (FCC) ambayo ni wakala wa serikali ya Marekani inayahimiza makampuni ya mitando ya simu kufanya utafiti iwapo namba za simu zinaweza kuwa IP ambapo hata katika namba za dhalula ambazo hutumiwa bure kwa huduma za haraka zitumike kuwasiliana kwa kutumia tovuti.
IP ni namba ya pekee ambayo hutumika katika utambuzi wa komputa ama kifaa cha mawasiliano kilichopo katika mtandao ili kiweze kuwasiliana na komputa ama kifaa kingine.
Tovuti ya engadget na shirika la habari la Reuters zimeikariri FCC karibuni ikieleza kuwa makampuni ya mitandao ya simu ambayo yanataka kushiriki kwenye utafiti huyo yanapaswa kuwasilisha mawazo yao kuhusu jambo hilo mwishoni mwa mwezi februari mwaka huu na maamuzi ya jambo hilo yanatarajiwa kutolewa mwezi machi mwaka huu.
Popular Posts
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
China imezifungia tovuti 110 ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuzuia masuala ya ngono kwenye mitandao.Imeeleza taarifa ya serikal...
-
Bunduki ya plastiki iliyotengenezwa kwa mashine ya 3D ikifyatua risasi wakati wa majaribio Photo credits: Screenshot from ATF Video Kam...
-
Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa M...
-
Program Tumishi maarufu ya mawasiliano ya ujumbe wa papo kwa papo katika simu za BlackBerry inayojulikana kwa jina la BlackBerry Mes...
-
Mtandao wa kijamii wa Facebook umenunua programu tumishi ya huduma za ujumbe mfupi wa maneno ya WhatsApp kwa dola za marekani bilioni ...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya kati imewataka watangazaji wa radio, luninga na mitandao ya kijamii kuwa makini na hab...
-
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) jana imekabidhi mradi wa mawasiliano utaotumiwa katika mikoa 12 ya Tanzania kwa ofisi ya Mkaguzi na ...
-
Kampuni ya Google kupitia huduma yake ya kutafuta jambo sasa imeanzisha utaratibu wa kutoa majibu ya moja kwa moja kwa maswali kuhus...