Friday, January 31, 2014
MAKAMPUNI YA MITANDAO YA SIMU NCHINI MAREKANI KUFANYA UTAFITI WA NAMBA ZA SIMU KUWA IP
Natumaini umeshawahi kusikia ama unafahamu kuhusu teknolojia ya kusafirisha mawimbi ya sauti kwa njia ya intaneti ( VoIP) ambayo si teknolojia mpya.
Kamisheni ya Shirikisho la Mawasiliano (FCC) ambayo ni wakala wa serikali ya Marekani inayahimiza makampuni ya mitando ya simu kufanya utafiti iwapo namba za simu zinaweza kuwa IP ambapo hata katika namba za dhalula ambazo hutumiwa bure kwa huduma za haraka zitumike kuwasiliana kwa kutumia tovuti.
IP ni namba ya pekee ambayo hutumika katika utambuzi wa komputa ama kifaa cha mawasiliano kilichopo katika mtandao ili kiweze kuwasiliana na komputa ama kifaa kingine.
Tovuti ya engadget na shirika la habari la Reuters zimeikariri FCC karibuni ikieleza kuwa makampuni ya mitandao ya simu ambayo yanataka kushiriki kwenye utafiti huyo yanapaswa kuwasilisha mawazo yao kuhusu jambo hilo mwishoni mwa mwezi februari mwaka huu na maamuzi ya jambo hilo yanatarajiwa kutolewa mwezi machi mwaka huu.
Popular Posts
-
Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) kupitia Mkurugenzi wake Mkuu Profesa John Nkoma imesema namba za simu zilizosajiliwa nchini hu...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...