Friday, January 31, 2014
MAKAMPUNI YA MITANDAO YA SIMU NCHINI MAREKANI KUFANYA UTAFITI WA NAMBA ZA SIMU KUWA IP
Natumaini umeshawahi kusikia ama unafahamu kuhusu teknolojia ya kusafirisha mawimbi ya sauti kwa njia ya intaneti ( VoIP) ambayo si teknolojia mpya.
Kamisheni ya Shirikisho la Mawasiliano (FCC) ambayo ni wakala wa serikali ya Marekani inayahimiza makampuni ya mitando ya simu kufanya utafiti iwapo namba za simu zinaweza kuwa IP ambapo hata katika namba za dhalula ambazo hutumiwa bure kwa huduma za haraka zitumike kuwasiliana kwa kutumia tovuti.
IP ni namba ya pekee ambayo hutumika katika utambuzi wa komputa ama kifaa cha mawasiliano kilichopo katika mtandao ili kiweze kuwasiliana na komputa ama kifaa kingine.
Tovuti ya engadget na shirika la habari la Reuters zimeikariri FCC karibuni ikieleza kuwa makampuni ya mitandao ya simu ambayo yanataka kushiriki kwenye utafiti huyo yanapaswa kuwasilisha mawazo yao kuhusu jambo hilo mwishoni mwa mwezi februari mwaka huu na maamuzi ya jambo hilo yanatarajiwa kutolewa mwezi machi mwaka huu.
Popular Posts
-
Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Simu katika Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Ndugu John Mwera akizungumza ...
-
Kanisa la Waadventista Wa Sabato mwaka huu litashiriki mkutano wa Waadventista watalaamu wa mawasilino ya Intaneti duniani (GAiN) kwa k...
-
Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam...
-
Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ-Kanali Ngemela Lubingo (Chanzo:Mwananchi) Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lime...
-
Wanasayansi wa maabara ya Bristol Robotics Uingereza wamegundua njia ya kutumia mkojo kama chanzo cha kuzalisha umeme wa kuchaji bet...
-
Kampuni ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya Huawei Tanzania na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) zimeungana na kuzindua mtandao wa ...
-
Serikali ya Tanzania imesema shilingi trioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao,endapo Sheria za...
-
Shule ya Msingi ya Mlimani iliyopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia wiki hii itaanza kunufaika na huduma ya intaneti bure inayofung...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Imeelezwa kwamba kadri teknolojia inavyoongezeka, inatengeneza fursa ya kukua kwa Shirika la Posta Duniani. Hayo yamesemwa na Kai...