Friday, January 31, 2014
MAKAMPUNI YA MITANDAO YA SIMU NCHINI MAREKANI KUFANYA UTAFITI WA NAMBA ZA SIMU KUWA IP
Natumaini umeshawahi kusikia ama unafahamu kuhusu teknolojia ya kusafirisha mawimbi ya sauti kwa njia ya intaneti ( VoIP) ambayo si teknolojia mpya.
Kamisheni ya Shirikisho la Mawasiliano (FCC) ambayo ni wakala wa serikali ya Marekani inayahimiza makampuni ya mitando ya simu kufanya utafiti iwapo namba za simu zinaweza kuwa IP ambapo hata katika namba za dhalula ambazo hutumiwa bure kwa huduma za haraka zitumike kuwasiliana kwa kutumia tovuti.
IP ni namba ya pekee ambayo hutumika katika utambuzi wa komputa ama kifaa cha mawasiliano kilichopo katika mtandao ili kiweze kuwasiliana na komputa ama kifaa kingine.
Tovuti ya engadget na shirika la habari la Reuters zimeikariri FCC karibuni ikieleza kuwa makampuni ya mitandao ya simu ambayo yanataka kushiriki kwenye utafiti huyo yanapaswa kuwasilisha mawazo yao kuhusu jambo hilo mwishoni mwa mwezi februari mwaka huu na maamuzi ya jambo hilo yanatarajiwa kutolewa mwezi machi mwaka huu.
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Unapomblock mtu kwenye viber inamaana umezuia kuwasiliana na mtu yoyote kwa njia yoyote katika mtandao wa kijamii wa viber,huta...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya ...