Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesema kuwa Internet
ni zawadi kwa dunia nzima kutoka kwa Mungu lakini akaonya kuwa matamanio
ya kutaka kuwasiliana zaidi kutumia Intaneti kunawatenga watu kutoka
kwa familia na marafiki zao.
Amewataka waumuni wa kikatoliki kujiunga na mfumo wa dijitali.
"Intaneti... inatoa nafasi ya mafanikio mengi. Hiki ni kitu kizuri bila
shaka ni zawadi kutoka kwa Mungu,'' alisema Papa.
Katika ujumbe wake kwa dunia nzima ambao hutolewa kila mwaka, Papa
amesema kuwa mfumo wa dijitali, unapaswa kuwa mtandao wa watu wala sio
nyaya tupu.
Papa mwenyewe ana akaunti kwenye Twitter ambayo ina wafuasi zaidi ya milioni kumi.
Amehimiza kuwa mawasiliano yanapaswa kuhusisha hisia na mawazo, watu kukutana na kujuliana hali.
Kadhalika amewataka waumini wa kikatoliki
kutodhani kuwa ni mawazo yao na imani zao pekee ambazo ni muhimu wakati
wakiwasiliana na watu wa dini nyinginezo.
Chanzo:BBC
Popular Posts
-
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Afrika,Raia wa Afrika kutoka Congo-DRC Verone Mankou,amezindua simu aina ya smarthphone na k...
-
--> Mwenyekiti wa muda wa Chama cha Wamiliki wa Blog (TBN),Joachim Mushi akizungumza na waandishi wa habari Ofisa Uhusiano...
-
Wamiliki wa vituo vya utangazaji vya televisheni nchini, wamesema watasitisha kurusha matangazo ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa kutokan...
-
Explore more visuals like this one on the web's largest information design community - Visually .
-
Idara ya Uhamiaji nchini Tanzania imeeleza kujivunia mabadiliko ya utumiaji wa Teknohama katika utendaji wake wa kazi katika kipindi ...
-
Afrika ni Bara la pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu ambapo inafikia takribani bilioni 1.2 (wengi wao wakiishi mijini) na inatarajiwa kon...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inasheherekea maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwake huku yakiwemo mafanikio makubwa d...
-
Mitandao ya kijamii ni mingi sana,ingawa facebook umekuwa maarufu pengine kuliko hata baadhi ya vituo vya redio ama televisheni. K...