Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa Mawasiliano ya Simu, Februari 27,2014 jijini Dar es salaam,uzinnduzi uliofanyika yalipo makao makuu ya Mamlaka ya Mawasilino Tanzania (TCRA)
TCRA kupitia Mkurugenzi wake Profesa John Nkoma ameeleza mtambo huo utakuwa na faida zifuatazo;
1.Kuwa na uwezo wa kujua mapato yanayopatikana kwenye simu za kimataifa zinazoingia nchini.
2.Kuongeza mapato kwa sekta ya mawasiliano kutokana na wapigaji wa simu waliopo nje ya nchi ili kuweka uwiano ulio sawa kati ya makampuni ya hapa nchini na yale ya nje ya nchi.
3.Kuwa na utaalamu wa kuweza kuzuia matumizi ya simu zinazopigwa nchini na makampuni yasiyo na leseni kwa ajili ya kuunganisha simu za kimataifa na hivyo kuikosesha serikali ya Tanzania na Makampuni ya simu mapato halali.
4.Kuongeza uwazi na uwajibikaji katika sekta ya mawasiliano.
5.Kuipa serikali kwa kupitia TCRA uwezo wa kuweza kusimamia sekta ya mawasiliano vizuri,kwa kuwa sekta inakuwa kwa kasi na inatoa huduma nyingi sana zikiwemo za benki mtandao.
Makampuni yenye leseni za kutoa huduma za simu za kimataifa na nchini Tanzania ni Airtel,MIC (Tigo),Sixtelecoms,TTCL,Vodacom na Zantel
Thursday, February 27, 2014
FAIDA ZA MTAMBO WA USIMAMIZI NA UHAKIKI WA MAWASILIANO YA SIMU ULIOZINDULIWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.
Popular Posts
-
Katika ukurasa wake wa twitter Mhe Zitto Kabwe ametweet "Asanteni sana Wauza Mawese # TeamMawese leo kwenye uzinduzi wetu Kigoma Mj...
-
Wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakitoa elimu jinsi ya kut...
-
Wanasayansi wa maabara ya Bristol Robotics Uingereza wamegundua njia ya kutumia mkojo kama chanzo cha kuzalisha umeme wa kuchaji bet...
-
Maelfu ya tarakirishi (kompyuta) za mitandao ya mashirika makubwa kadhaa duniani yamedukuliwa na kutekwa na watekaji wanadai malipo ...
-
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaanza kutumia tiketi za elektroniki kwenye uwanja wa Azam uliopo Chamazi,Dar es salaam w...
-
Mwaka 2014 Umekua wenye changamoto nyingi sana kwenye upande wa mitandao ambapo wahalifu mtandao walifanikiwa kwa kiasi kikubwa san...
-
Afrika ni Bara la pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu ambapo inafikia takribani bilioni 1.2 (wengi wao wakiishi mijini) na inatarajiwa kon...
-
Maafisa wa utawala katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, wamebana matumizi ya ujumbe mfupi wa simu za mkononi baada ya kusema kuwa ni t...
-
Shirika la kujiolea la nchini Marekani linalojihusisha na utabibu na masuala ya haki za binadamu (PHR) limetengeneza program tumishi mp...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuanzia sasa itakamata mtu yoyote anayesajili laini za simu kwa kuchakachua au bila kuf...