Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa Mawasiliano ya Simu, Februari 27,2014 jijini Dar es salaam,uzinnduzi uliofanyika yalipo makao makuu ya Mamlaka ya Mawasilino Tanzania (TCRA)
TCRA kupitia Mkurugenzi wake Profesa John Nkoma ameeleza mtambo huo utakuwa na faida zifuatazo;
1.Kuwa na uwezo wa kujua mapato yanayopatikana kwenye simu za kimataifa zinazoingia nchini.
2.Kuongeza mapato kwa sekta ya mawasiliano kutokana na wapigaji wa simu waliopo nje ya nchi ili kuweka uwiano ulio sawa kati ya makampuni ya hapa nchini na yale ya nje ya nchi.
3.Kuwa na utaalamu wa kuweza kuzuia matumizi ya simu zinazopigwa nchini na makampuni yasiyo na leseni kwa ajili ya kuunganisha simu za kimataifa na hivyo kuikosesha serikali ya Tanzania na Makampuni ya simu mapato halali.
4.Kuongeza uwazi na uwajibikaji katika sekta ya mawasiliano.
5.Kuipa serikali kwa kupitia TCRA uwezo wa kuweza kusimamia sekta ya mawasiliano vizuri,kwa kuwa sekta inakuwa kwa kasi na inatoa huduma nyingi sana zikiwemo za benki mtandao.
Makampuni yenye leseni za kutoa huduma za simu za kimataifa na nchini Tanzania ni Airtel,MIC (Tigo),Sixtelecoms,TTCL,Vodacom na Zantel
Thursday, February 27, 2014
FAIDA ZA MTAMBO WA USIMAMIZI NA UHAKIKI WA MAWASILIANO YA SIMU ULIOZINDULIWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...