Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa Mawasiliano ya Simu, Februari 27,2014 jijini Dar es salaam,uzinnduzi uliofanyika yalipo makao makuu ya Mamlaka ya Mawasilino Tanzania (TCRA)
TCRA kupitia Mkurugenzi wake Profesa John Nkoma ameeleza mtambo huo utakuwa na faida zifuatazo;
1.Kuwa na uwezo wa kujua mapato yanayopatikana kwenye simu za kimataifa zinazoingia nchini.
2.Kuongeza mapato kwa sekta ya mawasiliano kutokana na wapigaji wa simu waliopo nje ya nchi ili kuweka uwiano ulio sawa kati ya makampuni ya hapa nchini na yale ya nje ya nchi.
3.Kuwa na utaalamu wa kuweza kuzuia matumizi ya simu zinazopigwa nchini na makampuni yasiyo na leseni kwa ajili ya kuunganisha simu za kimataifa na hivyo kuikosesha serikali ya Tanzania na Makampuni ya simu mapato halali.
4.Kuongeza uwazi na uwajibikaji katika sekta ya mawasiliano.
5.Kuipa serikali kwa kupitia TCRA uwezo wa kuweza kusimamia sekta ya mawasiliano vizuri,kwa kuwa sekta inakuwa kwa kasi na inatoa huduma nyingi sana zikiwemo za benki mtandao.
Makampuni yenye leseni za kutoa huduma za simu za kimataifa na nchini Tanzania ni Airtel,MIC (Tigo),Sixtelecoms,TTCL,Vodacom na Zantel
Thursday, February 27, 2014
FAIDA ZA MTAMBO WA USIMAMIZI NA UHAKIKI WA MAWASILIANO YA SIMU ULIOZINDULIWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Huduma ya ujumbe Whatsapp imetangaza kuwa itayalinda mawasiliano ya wateja wake kuanzia hapo siku ya Jumanne April 5,mwaka huu Huk...
-
Serikali ya Tanzania inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa hivi karibuni kumezuka kundi la Watu wadanganyifu ambao wamekuwa wakit...
-
Serikali ya Kenya imesema watu watakaopatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kingono kwa kutumia simu za kiganjani na intaneti watafungw...
-
Watafiti toka kampuni ya utafiti ya Zscalar wamegundua kuwa,tovuti za kichina zenye picha za ngono zimekuwa zikisamb...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Kuwa na Akaunti ya Facebook ni kwa manufaa yako na manufaa ya Facebook Facebook ambayo kwa sasa inapatikana katika lugha 70 ul...