Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam wamezungumzia utapeli unaofanywa kwa kutumia simu za mkononi na kusema wengi wanaofanya hivyo husajili laini kwa majina ya uongo.
Kamishna Msaidizi wa Polisi na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es salaam,Ahmed Msangi amehadharisha wananchi kwa kutaka kuwa makini katika kutuma fedha kwa njia ya simu.
Alikuwa akizungumza na mwandishi wa habari wa gazeti la Habari Leo juu ya utapeli uliohusisha kampuni ya ndege ya kimataifa ya Qatar ambao baadhi ya watu wameibiwa pesa zao baada ya kuzituma kwa watu waliojifanya ni maofisa wa kampuni hiyo kwa ahadi ya kupatiwa kazi.
Kaimu meneja Mawasiliano Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA,Semu Mkwakanjala anasema alisema wanafanya mikutano kadhaa na kampuni za simu za mikononi kukumbusha kufuata utaratibu wa usajili wa namba unaozingatia sheria ili kuepusha kuendelea kutokea kwa uhalifu kupitia simu za mkononi.
Popular Posts
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome akizungumza kabla ya kuzindua rasmi maonesho ya Tehama yanayoend...
-
Yusuph Kileo baada ya kukabidhiwa tuzo Mtaalamu wa masuala ya usalama mtandaoni Yusu ph Kileo hivi karibuni alipata Tunzo ya ...
-
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia imesema gharama za kupiga simu kutoka mtandao wa kampuni moja ya s...
-
Kampuni ya magari ya Fiat Chrysler kutoka Marekani imeyarudisha magari yake yapatayo milioni 1.4 baada ya watafiti wa usalama kuony...
-
Watumiaji wa programu ya komputa iitwayo Window XP wamepewa tahadhari na kampuni ya Microsoft ambayo ndiyo iliyotengeneza program hiyo ...
-
Na Brown Nyanza Wanasayansi wawili katika nchi ya Ujerumani wamegundua kalamu inayotoa alama pindi mwandishi anapokosea heruf...
-
Mkuu Kituo cha Teknohama cha Ushirikiano wa India na Tanzania (DIT), Dr. Amos Nungu akiwakaribisha wafanyakazi wa Shirika la Umoja w...