Simu za Android kwa sasa zimekuwa na watumiaji wengi na inawezekana
ndio zinaongoza kwa kuwavutia wezi. Lakini bila kujali kuwa simu yako
imeibiwa au umeisahau sehemu kuna umuhimu wa kuhakikisha unachukua
tahadhari ili inapotokea tukio linalokufanya usijue simu yako iko wapi
uweze kuifatilia. Hizi ni baadhi ya software ambazo unaweza kuweka
kwenye simu yako na kukusaidia pale inapopotea au kuibiwa:
1. Anti Theft Droid
Hii ni App inayokuwezesha kufuatilia simu yako pale inapokuwa
imepotea au kuibiwa. Unapoiweka katika simu yako unakuwa na uwezo wa
kuifuatilia kupitia browser ya internet kama Mozilla au google chrome na
inaweza kukutumia email pale inapotokea simcard ya simu yako
kubadilishwa na kuwekwa nyingine. Pia inakuwezesha kuona picha ambazo
zimepigwa kwenye simu yako pale unapokuwa umeipoteza.
2. Snuko – Android Anti Theft Security
Snuko ni App inayokuwezesha kuifuatilia simu yako ya android kwa
kutumia GPS, Wi-Fi na mnara wa simu inayotumia. Snuko pia inaweza
kuizima simu yako pale unapogundua kuwa imeibiwa na uwezekano wa kuipata
haupo na inaweza kukupa taarifa pale simcard inapobadilishwa.
3. Total Equipment Protection App
Hii inafanya kazi kama nyingine zilizotajwa hapo juu ikikuwezesha
kujua simu yako iko maeneo gani lakini ikiwa na kitu cha ziada ambacho
ni uwezo wa kufuta data zako zote zilizokuwa kwenye simu inapotokea
ukashindwa kuipata simu yako..
4. Cerberus Anti Theft
Cerberus Anti Theft inaweza kutumika kuzilinda simu hadi 5 kwa wakati
mmoja, pia inakutumia taarifa kupitia ujumbe mfupi “SMS”. Kitu kingine
kizuri kuhusu App hii ni kuwa inaweza kufuatilia simu yako iko maeneo
gani kwa kusikiliza mazungumzo kupitia microphone ya simu yako hata kama
alieichukua haitumii kupiga simu.
5. Lost Droid
Lost Droid ni App ambayo inakusaidia kuitafuta simu yako iliyopotea
kwa kutumia computer yako. Inaweza kukutumia taarifa ya mahali simu yako
ilipo kupitia SMS bila kusahau kuizima simu yako kwa kutumia SMS.
Chanzo:tanganyikanblog
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakitoa elimu jinsi ya kut...
-
Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Simu katika Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Ndugu John Mwera akizungumza ...
-
Kanisa la Waadventista Wa Sabato mwaka huu litashiriki mkutano wa Waadventista watalaamu wa mawasilino ya Intaneti duniani (GAiN) kwa k...
-
Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
If you've already bought a smart phone, you'll know the importance of choosing a good OS for it. With the versions of all the giant...
-
Serikali Mtandao inarahisisha utendaji kazi na utoaji wa huduma kwa umma. Usikose kuangalia kipindi hiki cha Seikali Mtandao katika Mamlaka...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...