Simu za Android kwa sasa zimekuwa na watumiaji wengi na inawezekana
ndio zinaongoza kwa kuwavutia wezi. Lakini bila kujali kuwa simu yako
imeibiwa au umeisahau sehemu kuna umuhimu wa kuhakikisha unachukua
tahadhari ili inapotokea tukio linalokufanya usijue simu yako iko wapi
uweze kuifatilia. Hizi ni baadhi ya software ambazo unaweza kuweka
kwenye simu yako na kukusaidia pale inapopotea au kuibiwa:
1. Anti Theft Droid
Hii ni App inayokuwezesha kufuatilia simu yako pale inapokuwa
imepotea au kuibiwa. Unapoiweka katika simu yako unakuwa na uwezo wa
kuifuatilia kupitia browser ya internet kama Mozilla au google chrome na
inaweza kukutumia email pale inapotokea simcard ya simu yako
kubadilishwa na kuwekwa nyingine. Pia inakuwezesha kuona picha ambazo
zimepigwa kwenye simu yako pale unapokuwa umeipoteza.
2. Snuko – Android Anti Theft Security
Snuko ni App inayokuwezesha kuifuatilia simu yako ya android kwa
kutumia GPS, Wi-Fi na mnara wa simu inayotumia. Snuko pia inaweza
kuizima simu yako pale unapogundua kuwa imeibiwa na uwezekano wa kuipata
haupo na inaweza kukupa taarifa pale simcard inapobadilishwa.
3. Total Equipment Protection App
Hii inafanya kazi kama nyingine zilizotajwa hapo juu ikikuwezesha
kujua simu yako iko maeneo gani lakini ikiwa na kitu cha ziada ambacho
ni uwezo wa kufuta data zako zote zilizokuwa kwenye simu inapotokea
ukashindwa kuipata simu yako..
4. Cerberus Anti Theft
Cerberus Anti Theft inaweza kutumika kuzilinda simu hadi 5 kwa wakati
mmoja, pia inakutumia taarifa kupitia ujumbe mfupi “SMS”. Kitu kingine
kizuri kuhusu App hii ni kuwa inaweza kufuatilia simu yako iko maeneo
gani kwa kusikiliza mazungumzo kupitia microphone ya simu yako hata kama
alieichukua haitumii kupiga simu.
5. Lost Droid
Lost Droid ni App ambayo inakusaidia kuitafuta simu yako iliyopotea
kwa kutumia computer yako. Inaweza kukutumia taarifa ya mahali simu yako
ilipo kupitia SMS bila kusahau kuizima simu yako kwa kutumia SMS.
Chanzo:tanganyikanblog
Popular Posts
-
Wanasayansi wa maabara ya Bristol Robotics Uingereza wamegundua njia ya kutumia mkojo kama chanzo cha kuzalisha umeme wa kuchaji bet...
-
Wakulima nchini Nigeria wamepewa bure simu za mikononi,Ingawa vyama vya upinzani vinakandia hali hiyo wananchi wengi wanaamini huo ni...
-
Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa M...
-
Maelfu ya tarakirishi (kompyuta) za mitandao ya mashirika makubwa kadhaa duniani yamedukuliwa na kutekwa na watekaji wanadai malipo ...
-
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaanza kutumia tiketi za elektroniki kwenye uwanja wa Azam uliopo Chamazi,Dar es salaam w...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetoa viwango vipya vya bei elekezi ya gharama za kupiga simu kwa mwingiliano wa mitandao ya ma...
-
Shirika la kujiolea la nchini Marekani linalojihusisha na utabibu na masuala ya haki za binadamu (PHR) limetengeneza program tumishi mp...
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
Kampuni ya Microsft Corporation imeanzisha programu mpya ambayo itawawezesha wanafunzi kufanya mazoezi yote wanayopewa shuleni kupitia tek...