Simu za Android kwa sasa zimekuwa na watumiaji wengi na inawezekana
ndio zinaongoza kwa kuwavutia wezi. Lakini bila kujali kuwa simu yako
imeibiwa au umeisahau sehemu kuna umuhimu wa kuhakikisha unachukua
tahadhari ili inapotokea tukio linalokufanya usijue simu yako iko wapi
uweze kuifatilia. Hizi ni baadhi ya software ambazo unaweza kuweka
kwenye simu yako na kukusaidia pale inapopotea au kuibiwa:
1. Anti Theft Droid
Hii ni App inayokuwezesha kufuatilia simu yako pale inapokuwa
imepotea au kuibiwa. Unapoiweka katika simu yako unakuwa na uwezo wa
kuifuatilia kupitia browser ya internet kama Mozilla au google chrome na
inaweza kukutumia email pale inapotokea simcard ya simu yako
kubadilishwa na kuwekwa nyingine. Pia inakuwezesha kuona picha ambazo
zimepigwa kwenye simu yako pale unapokuwa umeipoteza.
2. Snuko – Android Anti Theft Security
Snuko ni App inayokuwezesha kuifuatilia simu yako ya android kwa
kutumia GPS, Wi-Fi na mnara wa simu inayotumia. Snuko pia inaweza
kuizima simu yako pale unapogundua kuwa imeibiwa na uwezekano wa kuipata
haupo na inaweza kukupa taarifa pale simcard inapobadilishwa.
3. Total Equipment Protection App
Hii inafanya kazi kama nyingine zilizotajwa hapo juu ikikuwezesha
kujua simu yako iko maeneo gani lakini ikiwa na kitu cha ziada ambacho
ni uwezo wa kufuta data zako zote zilizokuwa kwenye simu inapotokea
ukashindwa kuipata simu yako..
4. Cerberus Anti Theft
Cerberus Anti Theft inaweza kutumika kuzilinda simu hadi 5 kwa wakati
mmoja, pia inakutumia taarifa kupitia ujumbe mfupi “SMS”. Kitu kingine
kizuri kuhusu App hii ni kuwa inaweza kufuatilia simu yako iko maeneo
gani kwa kusikiliza mazungumzo kupitia microphone ya simu yako hata kama
alieichukua haitumii kupiga simu.
5. Lost Droid
Lost Droid ni App ambayo inakusaidia kuitafuta simu yako iliyopotea
kwa kutumia computer yako. Inaweza kukutumia taarifa ya mahali simu yako
ilipo kupitia SMS bila kusahau kuizima simu yako kwa kutumia SMS.
Chanzo:tanganyikanblog
Popular Posts
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome akizungumza kabla ya kuzindua rasmi maonesho ya Tehama yanayoend...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA Kufuatana na kifungu nambari 41 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki ...
-
Kampuni ya magari ya Fiat Chrysler kutoka Marekani imeyarudisha magari yake yapatayo milioni 1.4 baada ya watafiti wa usalama kuony...