Saturday, October 11, 2014

BAADHI YA PICHA JINSI WAADVENTISTA WA SABATO WALIVYOUNGANA KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII KUOMBEA TATIZO LA EBOLA

 
 


 

 



Oktoba 11,2014 ilikuwa ni siku maalum kwa waumini wa  Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani kwa ajili ya kuombea waathirika  wa ugonjwa wa ebola,tukio hilo liliwashirikisha watu wote duniani kwa kushiriki kwa kutumia mitandao ya kijamii wa twitter na facebook kwa kutumia #UnitedinPrayer for #EbolaCrisis


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani Mchungaji Ted Wilson hivi karibuni  ambaye anaongoza kanisa hilo lenye waumini milioni 18 katika nchi 215 kutoka divisheni 13 za kanisa hilo duniani amesema ameguswa sana na tatizo la Ebola lililowakumba watu kutoka nchi za Afrika magharibi hasa nchi za Guinea,Siera Leone, Liberia ,Senegal na Nigeria.


Octoba mosi mwaka huu kanisa la waadventista wa sabato kupitia  chama cha wachungaji lilianzisha mkakati wa kufanya maombi duniani kote kwa kutumia mitandao ya kijamii kuombea tatizo la ugonjwa wa ebola  kwa watu waliokumbwa na ugonjwa huo,mkakati ambao umehitimishwa oktoba  11,2014 kwenye makao makuu ya kanisa hilo na viongozi wa ngazi za juu toka sehemu mbalimbali duniani waliokutana yalipo makao makuu ya kanisa hilo Maryland nchini Marekani


Popular Posts

Labels