Friday, October 10, 2014

TEKNOLOJIA YA HABARI YAOKOA GHARAMA ZA KANISA



Idara ya uwakili ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani imesema kuwa Utoaji wa semina na makongamano kupitia mtandao wa intaneti unaweza kuwafikia watu wengi kwa gharama ndogo kuliko njia za kawaida zinazotumika sasa.

Hatua hiyo inakuja baada ya hivi karibuni kufanyika mkutano wa uwakili kwa njia ya mtandao uliowezeshwa na idara ya mawasiliano ya kanisa hilo duniani na kuwashirikisha watu 2000 toka nchi 83 uliohusisha masaa 12 ya mafunzo yaliyowezeshwa na watoa mada 15 wakiwemo Mwenyekiti wa Kanisa hilo ulimwenguni Mch Teddy Wilson,Makamu wake Mchungaji Pardon Mwansa, Benjamin Shoun ,Mwenyekiti wa Divisheni ya Amerika ya Kati  Israel Leitona Daniel Jackson toka Divisheni ya Kaskazini mwabara la Amerika.

Taarifa zinaeleza kuwa mkutano huo ulitumia dola za kimarekani 20,000 tofauti na utaratibu wa kawaida  ya kuwa kutanisha watu katika eneo moja ambapo zingetumika dola za kimarekani  1,168,000  jambo ambalo limewapa shauku viongozi wa kanisa hilo duniani kufanya mkutano mwingine kwa njia ya mtandao.

Mkutano huo ulioendeshwa kwa lugha ya Kiingereza, Kifaransa, Kireno na kihispaniola ulihusisha video za masaa 48,masaa 12 ya uwasilishaji ambao umesambazwa kwenye vituo vya televisheni vya kanisa hilo.

Popular Posts

Labels