Kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Tanzania limekanusha uvumi wa ujumbe mfupi wa maneno
unaoendelea kusambazwa kwenye simu na mitandao ya kijamii kuhusiana na Papa kumtaka Rais
Barack Obama wa Marekani kupitisha sheria ya kuabudu siku ya jumapili mwezi huu.
Akizungumza katika kipindi cha Kanisani jumahili kupitia Morning Star Radio ambacho huwapatia nafasi Viongozi mbalimbali wa Kanisa hilo kutoa mada na kuulizwa maswali na wasikilizaji Katibu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato katika Unioni ya Kusini mwa Tanzania Mchungaji James Machage amesema kuwa ujumbe huo ni uvumi na wa uongo ambao hauhusiana na kanisa hilo,kwani kanisa lina utaratibu maalum wa kutoa matamko yanayolihusu na sio katika ujumbe wa maneno katika simu ama kwenye mitandao ya kijamii.
Toka jumatano iliyopita blog hii imekuwa ikitumiwa na kushuhudia ujumbe huo ambao mwanzoni ulikuwa kwa lugha ya kiingereza na ijumaa ukawa umetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili hali ambayo imeleta sintofahamu miongoni mwa waumini wa kanisa la Waadventista Wa Sabato
Ujumbe wenyewe wa kiingereza "Doreen
Emmau: The Pope urging US President Barrack Obama to pass the National
Sunday Law this month,SDA President Ted Wilson is appealing to
all SDA members around the world to pray and have a personal
consecration and revival and reformation of Godliness for 7 days either 7
am or 7 pm for the outcome of the Holy Spirit in the form of the latter
rain.Plse send to all SDA members.Many will be cold in faith,a prophecy
that will go back to the fold of the Beast the pope itself.Be Watchful
my friend,Jesus is at the Door....He is coming be Ready....Harry Coombs"
Wa kiswahili "Papa amwomba rais wa marekani Barack Obama atangaze sheria ya taifa ya
jumapil mwisho wa mwezi huu, rais wa wasabato Ted wilson anawaomba
waadventista wasabato duniani kote kufanya maombi na matengenezo kwa
siku saba kwa ajili ya utauwa wa kweli muda wa maombi ni saa 1 asbh au 1
jioni kwa kumwagwa roho mtakatifu kwa namna ya mvua.Tafadhali tuma sms
kwa waadventista wasabato.Rafiki yangu kesha na uwe tayari YESU anakuja
yuko mlangoni"
Naye Katibu Mkuu wa Konferensi ya Mashariki mwa Tanzania Mchungaji Sadock Butoke amesema jana kuwa kanisa hilo halina taarifa hizo na ujumbe huo unapaswa kupuuzwa.
Saturday, October 18, 2014
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakitoa elimu jinsi ya kut...
-
Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Simu katika Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Ndugu John Mwera akizungumza ...
-
Kanisa la Waadventista Wa Sabato mwaka huu litashiriki mkutano wa Waadventista watalaamu wa mawasilino ya Intaneti duniani (GAiN) kwa k...
-
Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam...
-
If you've already bought a smart phone, you'll know the importance of choosing a good OS for it. With the versions of all the giant...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...
-
Wataalamu wa Teknolojia nchini Ghana wamebuni teknolojia ya kuhakiki ikiwa dawa ni bandia au ni halisi. Teknolojia hiyo iliyozindul...
-
New software which mines data from social networks to track people's movements and even predict future behaviour poses a 'very ...