Kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Tanzania limekanusha uvumi wa ujumbe mfupi wa maneno
unaoendelea kusambazwa kwenye simu na mitandao ya kijamii kuhusiana na Papa kumtaka Rais
Barack Obama wa Marekani kupitisha sheria ya kuabudu siku ya jumapili mwezi huu.
Akizungumza katika kipindi cha Kanisani jumahili kupitia Morning Star Radio ambacho huwapatia nafasi Viongozi mbalimbali wa Kanisa hilo kutoa mada na kuulizwa maswali na wasikilizaji Katibu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato katika Unioni ya Kusini mwa Tanzania Mchungaji James Machage amesema kuwa ujumbe huo ni uvumi na wa uongo ambao hauhusiana na kanisa hilo,kwani kanisa lina utaratibu maalum wa kutoa matamko yanayolihusu na sio katika ujumbe wa maneno katika simu ama kwenye mitandao ya kijamii.
Toka jumatano iliyopita blog hii imekuwa ikitumiwa na kushuhudia ujumbe huo ambao mwanzoni ulikuwa kwa lugha ya kiingereza na ijumaa ukawa umetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili hali ambayo imeleta sintofahamu miongoni mwa waumini wa kanisa la Waadventista Wa Sabato
Ujumbe wenyewe wa kiingereza "Doreen
Emmau: The Pope urging US President Barrack Obama to pass the National
Sunday Law this month,SDA President Ted Wilson is appealing to
all SDA members around the world to pray and have a personal
consecration and revival and reformation of Godliness for 7 days either 7
am or 7 pm for the outcome of the Holy Spirit in the form of the latter
rain.Plse send to all SDA members.Many will be cold in faith,a prophecy
that will go back to the fold of the Beast the pope itself.Be Watchful
my friend,Jesus is at the Door....He is coming be Ready....Harry Coombs"
Wa kiswahili "Papa amwomba rais wa marekani Barack Obama atangaze sheria ya taifa ya
jumapil mwisho wa mwezi huu, rais wa wasabato Ted wilson anawaomba
waadventista wasabato duniani kote kufanya maombi na matengenezo kwa
siku saba kwa ajili ya utauwa wa kweli muda wa maombi ni saa 1 asbh au 1
jioni kwa kumwagwa roho mtakatifu kwa namna ya mvua.Tafadhali tuma sms
kwa waadventista wasabato.Rafiki yangu kesha na uwe tayari YESU anakuja
yuko mlangoni"
Naye Katibu Mkuu wa Konferensi ya Mashariki mwa Tanzania Mchungaji Sadock Butoke amesema jana kuwa kanisa hilo halina taarifa hizo na ujumbe huo unapaswa kupuuzwa.
Saturday, October 18, 2014
Popular Posts
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
China imezifungia tovuti 110 ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuzuia masuala ya ngono kwenye mitandao.Imeeleza taarifa ya serikal...
-
Bunduki ya plastiki iliyotengenezwa kwa mashine ya 3D ikifyatua risasi wakati wa majaribio Photo credits: Screenshot from ATF Video Kam...
-
Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa M...
-
Program Tumishi maarufu ya mawasiliano ya ujumbe wa papo kwa papo katika simu za BlackBerry inayojulikana kwa jina la BlackBerry Mes...
-
Mtandao wa kijamii wa Facebook umenunua programu tumishi ya huduma za ujumbe mfupi wa maneno ya WhatsApp kwa dola za marekani bilioni ...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya kati imewataka watangazaji wa radio, luninga na mitandao ya kijamii kuwa makini na hab...
-
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) jana imekabidhi mradi wa mawasiliano utaotumiwa katika mikoa 12 ya Tanzania kwa ofisi ya Mkaguzi na ...
-
Kampuni ya Google kupitia huduma yake ya kutafuta jambo sasa imeanzisha utaratibu wa kutoa majibu ya moja kwa moja kwa maswali kuhus...