Kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Tanzania limekanusha uvumi wa ujumbe mfupi wa maneno
unaoendelea kusambazwa kwenye simu na mitandao ya kijamii kuhusiana na Papa kumtaka Rais
Barack Obama wa Marekani kupitisha sheria ya kuabudu siku ya jumapili mwezi huu.
Akizungumza katika kipindi cha Kanisani jumahili kupitia Morning Star Radio ambacho huwapatia nafasi Viongozi mbalimbali wa Kanisa hilo kutoa mada na kuulizwa maswali na wasikilizaji Katibu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato katika Unioni ya Kusini mwa Tanzania Mchungaji James Machage amesema kuwa ujumbe huo ni uvumi na wa uongo ambao hauhusiana na kanisa hilo,kwani kanisa lina utaratibu maalum wa kutoa matamko yanayolihusu na sio katika ujumbe wa maneno katika simu ama kwenye mitandao ya kijamii.
Toka jumatano iliyopita blog hii imekuwa ikitumiwa na kushuhudia ujumbe huo ambao mwanzoni ulikuwa kwa lugha ya kiingereza na ijumaa ukawa umetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili hali ambayo imeleta sintofahamu miongoni mwa waumini wa kanisa la Waadventista Wa Sabato
Ujumbe wenyewe wa kiingereza "Doreen
Emmau: The Pope urging US President Barrack Obama to pass the National
Sunday Law this month,SDA President Ted Wilson is appealing to
all SDA members around the world to pray and have a personal
consecration and revival and reformation of Godliness for 7 days either 7
am or 7 pm for the outcome of the Holy Spirit in the form of the latter
rain.Plse send to all SDA members.Many will be cold in faith,a prophecy
that will go back to the fold of the Beast the pope itself.Be Watchful
my friend,Jesus is at the Door....He is coming be Ready....Harry Coombs"
Wa kiswahili "Papa amwomba rais wa marekani Barack Obama atangaze sheria ya taifa ya
jumapil mwisho wa mwezi huu, rais wa wasabato Ted wilson anawaomba
waadventista wasabato duniani kote kufanya maombi na matengenezo kwa
siku saba kwa ajili ya utauwa wa kweli muda wa maombi ni saa 1 asbh au 1
jioni kwa kumwagwa roho mtakatifu kwa namna ya mvua.Tafadhali tuma sms
kwa waadventista wasabato.Rafiki yangu kesha na uwe tayari YESU anakuja
yuko mlangoni"
Naye Katibu Mkuu wa Konferensi ya Mashariki mwa Tanzania Mchungaji Sadock Butoke amesema jana kuwa kanisa hilo halina taarifa hizo na ujumbe huo unapaswa kupuuzwa.
Saturday, October 18, 2014
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...