Thursday, October 9, 2014

DAR ES SALAAM:WIZARA YAAHIDI KUSAIDIA UBORESHAJI WA HUDUMA ZA POSTA NCHINI



Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Tekinolojia nchini Tanzania imeahidi kutoa msaada kwa shirika la posta nchini humo ili liweze kuwa shirika bora na la kisasa zaidi.



Akizungumza katika warsha maalumu ya kuadhimisha siku ya posta duniani iliyofanyika jijini Dar es salaam  Katibu mkuu wa wizara ya mawasiliano sayansi ya tekinolojia Profesa Partick Makungu amesema kuwa wizara yake ipo tayari  kuliboresha shirika hilo ambalo ndilo lililo na uwezo mkubwa wa kumfikia kila mwananchi katika sehemu tofauti.



 Profesa Makungu amewataka viongozi wa shirika hilo pamoja na wadau wengine kutambua kuwa idadi kubwa ya watanzania wanaishi katika maeneo ya vijijini, hivyo wanawajibu wa kuhakikisha wanaboresha miundo mbinu ambayo itasaidia kuwezesha shughuli za utumaji wa vifurushi kuwa wa rahisi na wa haraka zaidi.



Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Shirika hilo Deusi Mndeme amesema lengo lao kubwa  kama viongozi wa shirika ni kuliboresha ili liwe la kisasa liweze kuhudumia idadi kubwa zaidi ya watanzania  kwani pamoja na uwepo wa  tekinolojia mpya za mawasiliano bado lipo hitaji kubwa kwa wananchi kutuma  vifurushi kwa njia ya posta,



 Siku ya posta duniani huadhimishwa kila tarehe 9 Oktoba kila mwaka ambapo mwaka huu siku hiyo imeadhimishwa hii leo Jijini DSM ikiwa na kauli mbiu  isemayo “ posta katika mageuzi ya sekta ya mawasiliano”.

Popular Posts

Labels