Serikali ya Tanzania
inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa hivi karibuni kumezuka
kundi la Watu wadanganyifu ambao wamekuwa wakitumia majina ya viongozi
waandamizi wa serikali na Taasisi nyeti ikiwemo Usalama wa Taifa
kujipatia fedha kwa madai ya kutumwa na viongozi hao.
Watu
hao wamekuwa wakituma ujumbe mfupi wa simu (SMS) kwa maofisa mbalimbali
wa wizara, mashirika ya umma na Idara za Serikali zinazojitegemea
kuomba pesa ili wawafanye mipango ya kupandishwa vyeo.
Utapeli
huo umekuwepo nchini kwa kipindi kirefu sasa, ambapo watu huwapigia
simu viongozi wa Taasisi za fedha, Mifuko ya Taasisi za Jamii na watu
binafisi wakiomba fedha kwa madai ya kutumwa na viongozi waandamizi
Serikalini wakati si kweli.
Watu
hao wamekuwa wakiwatapeli maofisa mbalimbali kuwa wanaweza kuwafanyia
mipango ya kupandishwa vyeo endapo watawapatia kiasi cha fedha jambo
ambalo halipo katika taratibu za utumishi wa umma.
Utumishi
wa umma unazo taratibu zake za kuwapandisha vyeo watumishi wake
kulingana na sifa za kada zao na wala haiwezekani kwa viongozi
waandamizi kuwachangisha fedha kwa ajili ya kuwapandisha vyeo. Serikali
inawataka wananchi kuwapuuza matapeli hao na watoe taarifa katika vyombo
vya dola na usalama mara wapatapo ujumbe wa aina hiyo ili hatua
zichukuliwe dhidi yao.
IMETOLEWA NA:
IDARA YA HABARI (MAELEZO)
DAR ES SALAAM.
12.02.2013
Chanzo:wanabidii googlegroups.com
Popular Posts
-
Moja ya sehemu iliyofanikiwa kufanya mapinduzi makubwa ya teknolojia ya sayansi ni teknolojia ya habari na mawasiliano. Katika mapin...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kuzingatia kifungu 5 (b) na (e) cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya 2003 inatoa t...
-
Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 inakadiliwa kuwa jumla ya program tumishi kwenye simu zitakazo kuwa zimepakuliwa duniani zitakuwa ni bi...
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Serikali ya Tanzania imesema shilingi trioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao,endapo Sheria za...
-
Kumekuwa na changamoto ya kujilinda na watu ambao wanaweza kukuwekea maelezo ama kukutagg picha usiyoihitaji kwenye timeline ...
-
Habari si nzuri kwa wanaume wanaopenda kutumia wireless internet kwenye laptop zao wakiwa wameziweka laptop zao mapajani au karibu na viun...