Serikali ya Tanzania
inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa hivi karibuni kumezuka
kundi la Watu wadanganyifu ambao wamekuwa wakitumia majina ya viongozi
waandamizi wa serikali na Taasisi nyeti ikiwemo Usalama wa Taifa
kujipatia fedha kwa madai ya kutumwa na viongozi hao.
Watu
hao wamekuwa wakituma ujumbe mfupi wa simu (SMS) kwa maofisa mbalimbali
wa wizara, mashirika ya umma na Idara za Serikali zinazojitegemea
kuomba pesa ili wawafanye mipango ya kupandishwa vyeo.
Utapeli
huo umekuwepo nchini kwa kipindi kirefu sasa, ambapo watu huwapigia
simu viongozi wa Taasisi za fedha, Mifuko ya Taasisi za Jamii na watu
binafisi wakiomba fedha kwa madai ya kutumwa na viongozi waandamizi
Serikalini wakati si kweli.
Watu
hao wamekuwa wakiwatapeli maofisa mbalimbali kuwa wanaweza kuwafanyia
mipango ya kupandishwa vyeo endapo watawapatia kiasi cha fedha jambo
ambalo halipo katika taratibu za utumishi wa umma.
Utumishi
wa umma unazo taratibu zake za kuwapandisha vyeo watumishi wake
kulingana na sifa za kada zao na wala haiwezekani kwa viongozi
waandamizi kuwachangisha fedha kwa ajili ya kuwapandisha vyeo. Serikali
inawataka wananchi kuwapuuza matapeli hao na watoe taarifa katika vyombo
vya dola na usalama mara wapatapo ujumbe wa aina hiyo ili hatua
zichukuliwe dhidi yao.
IMETOLEWA NA:
IDARA YA HABARI (MAELEZO)
DAR ES SALAAM.
12.02.2013
Chanzo:wanabidii googlegroups.com
Popular Posts
-
Kitabu hiki kipo tayari. Wasiliana kwa namba 0713 309 314 au 0763 309 314 na Mushi Richard, Mpesa: 0755872462, Tigopesa: 0713643703 ...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginev...
-
Mtandao wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha. Nia...
-
Bwana. Keriako Tobiko Mkurugenzi wa Mashtaka ya umma ya nchini Kenya Bwana. Keriako Tobiko ametangaza kuanzishwa kwa kitengo maalum...
-
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA UMMA Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha...
-
Waziri na waziri wa uchukuzi Dr Harrison mwakyembe amesema kuwa Teknolojia ya kisasa inayotumika katika uwanja wa ndege wa kimataifa...
-
Polisi Wa kuzuia uhalifu Mtandao. Wakala unaofuatilia matumizi ya mitandao duniani (IAB) umebaini watumiaji wa intaneti nchini Ko...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania jana ilianza kuendesha mkutano wa kimataifa kuhusu usimamizi na utekelezaji wa huduma ya simu za mkononi kwa...
-
A failure in contingency planning and disaster recovery Today, on November 14, 2012 in Tanzania, the TIGO network was completely not...