Jeshi la Polisi Tanzania limeanza kunasa watu wanaodaiwa kutuma ujumbe wa matusi na wengine kupiga simu kwa spika wa Bunge la nchi hiyo Anne Makinda na Naibu wake,Job Ndugai.
Hatua ya jeshi hilo imekuja siku chache,baada ya ofisi ya Bunge kudai kuwa namba zilizohusika kutuma au kupiga simu na kutoa matusi wanazo na kwamba,tayari wameziwasilisha kwenye mamlaka husika kwa hatua za kisheria.
Akizungumza Dar es salaam juzi Msemaji wa Polisi,Advera Senso alisema hivi sasa wanakusanya taarifa kutoa mikoa tofauti ili kujua takwimu halisi za watu waliokamatwa.
Advera alisema kutokana na hali hiyo wananchi wanapaswa kuwa makini na matumizi ya simu,ili kuondoa matatizo yaliyojitokeza ikiwemo kutumia ujumbe ama kupiga simu za matusi zinazoweza kuwasababisha kufikishwakwenye vyombo vya sheria
Wednesday, February 20, 2013
Popular Posts
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...