Jeshi la Polisi Tanzania limeanza kunasa watu wanaodaiwa kutuma ujumbe wa matusi na wengine kupiga simu kwa spika wa Bunge la nchi hiyo Anne Makinda na Naibu wake,Job Ndugai.
Hatua ya jeshi hilo imekuja siku chache,baada ya ofisi ya Bunge kudai kuwa namba zilizohusika kutuma au kupiga simu na kutoa matusi wanazo na kwamba,tayari wameziwasilisha kwenye mamlaka husika kwa hatua za kisheria.
Akizungumza Dar es salaam juzi Msemaji wa Polisi,Advera Senso alisema hivi sasa wanakusanya taarifa kutoa mikoa tofauti ili kujua takwimu halisi za watu waliokamatwa.
Advera alisema kutokana na hali hiyo wananchi wanapaswa kuwa makini na matumizi ya simu,ili kuondoa matatizo yaliyojitokeza ikiwemo kutumia ujumbe ama kupiga simu za matusi zinazoweza kuwasababisha kufikishwakwenye vyombo vya sheria
Wednesday, February 20, 2013
Popular Posts
-
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) jana imekabidhi mradi wa mawasiliano utaotumiwa katika mikoa 12 ya Tanzania kwa ofisi ya Mkaguzi na ...
-
Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto ya kuhifadhi vitu sehemu ambayo mtu anaweza kutumia akiwa popote duniani akiwa ame...
-
Ofisa Biashara wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Thomas Lemunge akitoa ufafanuzi katika semina kwa wahariri juu ya mkongo wa taifa katika...