Wakati matukio ya wizi wa fedha katika mashine maalumu za kutolea fedha katika benki maarufu kwa jina la ATM yakiendelea kuripotiwa na vyombo vya usalama nchini Tanzania,Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imesema kuwa licha ya kuwepo kwa wizi huo kamwe haitazuia huduma hiyo kwani ni mkombozi mkubwa kwa wateja.
Gavana wa BOT Profesa Benno Ndulu amekaririwa na Gazeti la Jambo leo akieleza kuwa huduma hiyo haiwezi kufutwa badala yake wataendelea kutafiti njia za kuwabana wahalifu hao.
Kauli hiyo ya gavana Ndulu imekuja siku moja baada ya jeshi la polisi
wilayani Rungwe, mkoani Mbeya,kuwanasa watu wanne akiwamo mwanafunzi
aliyemaliza kidato cha nne mwaka jana, wilayani Bunda, mkoani Mara,
baada ya kukutwa wakiiba fedha Benki ya NMB tawi la Tukuyu kupitia
mashine za kutolea fedha (ATM).
Watuhumiwa walikutwa
wakiwa na kadi bandia za ATM 150 za watu tofautitofauti na kwamba, hadi
wanatiwa mbaroni tayari walikuwa na Sh20.5 milioni mkononi,
kadi zote ni za NMB na kwamba, zilikuwa zinaonyesha wateja wote ni
walimu kutoka wilayani Mbozi.
Popular Posts
-
Facebook wametangaza kitu kipya kwa simu za Android walichokipa jina la Home. Kwa muda mrefu kulikuwa na uvumi kuwa Facebook wana...
-
Semina kuhusu mfumo wa utunzaji wa taarifa za washiriki katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato (ACMS) imemalizika jijini Arusha Septem...
-
Baadhi ya Wataalamu wa Teknohama wa Taasis za Kanisa la Waadventista Wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Kanisa l...
-
Mwezeshaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama cha Morning Star Radio,Johnson Mziray akichangia jambo kwenye warsha hiyo,pembeni yake mweny...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU KUVURUGA PROGRAMU YA WINXP 1 – PROGRAMU YA WIN XP KUVURUGIKA Sio ukweli kwamba programu ya win xp itavuruguka...
-
Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi akitoa zawadi kwa washindi wa tweet bora kwa mwezi wa nane Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ardhi Lilian Wils...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ,Bw Charles Kitwanga ameyashawishi mataifa ambayo tayari yamejiunga na mfumo wa Digitali katika haraka...