Wakati matukio ya wizi wa fedha katika mashine maalumu za kutolea fedha katika benki maarufu kwa jina la ATM yakiendelea kuripotiwa na vyombo vya usalama nchini Tanzania,Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imesema kuwa licha ya kuwepo kwa wizi huo kamwe haitazuia huduma hiyo kwani ni mkombozi mkubwa kwa wateja.
Gavana wa BOT Profesa Benno Ndulu amekaririwa na Gazeti la Jambo leo akieleza kuwa huduma hiyo haiwezi kufutwa badala yake wataendelea kutafiti njia za kuwabana wahalifu hao.
Kauli hiyo ya gavana Ndulu imekuja siku moja baada ya jeshi la polisi
wilayani Rungwe, mkoani Mbeya,kuwanasa watu wanne akiwamo mwanafunzi
aliyemaliza kidato cha nne mwaka jana, wilayani Bunda, mkoani Mara,
baada ya kukutwa wakiiba fedha Benki ya NMB tawi la Tukuyu kupitia
mashine za kutolea fedha (ATM).
Watuhumiwa walikutwa
wakiwa na kadi bandia za ATM 150 za watu tofautitofauti na kwamba, hadi
wanatiwa mbaroni tayari walikuwa na Sh20.5 milioni mkononi,
kadi zote ni za NMB na kwamba, zilikuwa zinaonyesha wateja wote ni
walimu kutoka wilayani Mbozi.
Popular Posts
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...