Tuesday, February 12, 2013
MADAKTARI NCHINI TANZANIA KUWASILIANA BURE KUPITIA VODACOM
Waatalamu wa afya nchini Tanzania wakiwamo madaktari, wataanza kupata huduma ya kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maneno bila malipo yoyote kwa wataalam wenzao popote nchini humo na kupokea taarifa, maelekezo na ushauri unaohitajika kupitia mtandao wa mawasiliano ya simu za mkononi wa Vodacom.
Mtandao kwa ajili ya mawasiliano ya wanataaluma wa afya Health Network Programme, umeanzishwa kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi wa madaktari na kuboresha kiwango cha mawasiliano ya wenyewe kwa wenyewe.
Usajili wa mtandao huo kuanzia sasa unatarajia kuhusisha wataalam wa afya wapatao 9,000 nchi nzima, wakiwamo madaktari wa meno na wasaidizi wao, tabibu na tabibu wasaidizi popote alipo, serikalini na binafsi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Vodacom Foundation, Yessaya Mwakifulefule, kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, ili mtaalam wa afya ajiunge kwenye programu hiyo, atatakiwa kutumia simu yake ya mkononi ambayo itakuwa na kadi ya simu (simcard) ya Vodacom.
Akizungumza katika uzinduzi wa huduma hiyo jijini Dar es Salaam, Mwakifulefule, alisema huduma hiyo muhimu na yenye tija siyo tu itawanufaisha madaktari na sekta ya afya, bali pia Watanzania wote mijini na vijijini.
Alisema mbali ya kupiga simu bure, wanachama wa mtandao huo kwa kushiriki katika programu hiyo watakuwa na uwezo wa kutuma ujumbe mfupi wa maneno 50 bure kila mwezi kuwasiliana na wenzao waliojisajili ndani ya programu hiyo.
Awali, Taasisi ya Kimataifa inayoshughulika na huduma za mawasiliano (Switchboard) kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari, imewasihi madaktari kujumuika katika program hiyo ili kutathmini mafanikio ya utendaji wao kama wadau na wataalamu ndani ya sekta ya afya.
Alisema suala la upungufu wa madaktari na wataalam wa afya katika mataifa mengi limesababisha daktari au muuguzi mmoja kujikuta akihudumia wagonjwa kati ya 5,000 hadi 150,000.
Programu hiyo inadhaminiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Switchboard na Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom.
Popular Posts
-
Some tips on keeping your online financial and personal information safe. ...
-
Moja ya sehemu iliyofanikiwa kufanya mapinduzi makubwa ya teknolojia ya sayansi ni teknolojia ya habari na mawasiliano. Katika mapin...
-
Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 inakadiliwa kuwa jumla ya program tumishi kwenye simu zitakazo kuwa zimepakuliwa duniani zitakuwa ni bi...
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Serikali ya Tanzania imesema shilingi trioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao,endapo Sheria za...
-
Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto ya kuhifadhi vitu sehemu ambayo mtu anaweza kutumia akiwa popote duniani akiwa ame...
-
Jumuia ya watumiaji wa huduma mbalimbali nchini Tanzania kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter imezindua rasmi shindano...
-
Kwa muda sasa Korea ya Kusini imeonekana kuwa na asilimia kubwa ya uwezo wa kasi ya intaneti duniani. Katika robo ya pili ya mwaka 20...