Tuesday, February 12, 2013
MADAKTARI NCHINI TANZANIA KUWASILIANA BURE KUPITIA VODACOM
Waatalamu wa afya nchini Tanzania wakiwamo madaktari, wataanza kupata huduma ya kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maneno bila malipo yoyote kwa wataalam wenzao popote nchini humo na kupokea taarifa, maelekezo na ushauri unaohitajika kupitia mtandao wa mawasiliano ya simu za mkononi wa Vodacom.
Mtandao kwa ajili ya mawasiliano ya wanataaluma wa afya Health Network Programme, umeanzishwa kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi wa madaktari na kuboresha kiwango cha mawasiliano ya wenyewe kwa wenyewe.
Usajili wa mtandao huo kuanzia sasa unatarajia kuhusisha wataalam wa afya wapatao 9,000 nchi nzima, wakiwamo madaktari wa meno na wasaidizi wao, tabibu na tabibu wasaidizi popote alipo, serikalini na binafsi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Vodacom Foundation, Yessaya Mwakifulefule, kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, ili mtaalam wa afya ajiunge kwenye programu hiyo, atatakiwa kutumia simu yake ya mkononi ambayo itakuwa na kadi ya simu (simcard) ya Vodacom.
Akizungumza katika uzinduzi wa huduma hiyo jijini Dar es Salaam, Mwakifulefule, alisema huduma hiyo muhimu na yenye tija siyo tu itawanufaisha madaktari na sekta ya afya, bali pia Watanzania wote mijini na vijijini.
Alisema mbali ya kupiga simu bure, wanachama wa mtandao huo kwa kushiriki katika programu hiyo watakuwa na uwezo wa kutuma ujumbe mfupi wa maneno 50 bure kila mwezi kuwasiliana na wenzao waliojisajili ndani ya programu hiyo.
Awali, Taasisi ya Kimataifa inayoshughulika na huduma za mawasiliano (Switchboard) kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari, imewasihi madaktari kujumuika katika program hiyo ili kutathmini mafanikio ya utendaji wao kama wadau na wataalamu ndani ya sekta ya afya.
Alisema suala la upungufu wa madaktari na wataalam wa afya katika mataifa mengi limesababisha daktari au muuguzi mmoja kujikuta akihudumia wagonjwa kati ya 5,000 hadi 150,000.
Programu hiyo inadhaminiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Switchboard na Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom.
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Unapomblock mtu kwenye viber inamaana umezuia kuwasiliana na mtu yoyote kwa njia yoyote katika mtandao wa kijamii wa viber,huta...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya ...