Tuesday, February 12, 2013
MADAKTARI NCHINI TANZANIA KUWASILIANA BURE KUPITIA VODACOM
Waatalamu wa afya nchini Tanzania wakiwamo madaktari, wataanza kupata huduma ya kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maneno bila malipo yoyote kwa wataalam wenzao popote nchini humo na kupokea taarifa, maelekezo na ushauri unaohitajika kupitia mtandao wa mawasiliano ya simu za mkononi wa Vodacom.
Mtandao kwa ajili ya mawasiliano ya wanataaluma wa afya Health Network Programme, umeanzishwa kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi wa madaktari na kuboresha kiwango cha mawasiliano ya wenyewe kwa wenyewe.
Usajili wa mtandao huo kuanzia sasa unatarajia kuhusisha wataalam wa afya wapatao 9,000 nchi nzima, wakiwamo madaktari wa meno na wasaidizi wao, tabibu na tabibu wasaidizi popote alipo, serikalini na binafsi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Vodacom Foundation, Yessaya Mwakifulefule, kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, ili mtaalam wa afya ajiunge kwenye programu hiyo, atatakiwa kutumia simu yake ya mkononi ambayo itakuwa na kadi ya simu (simcard) ya Vodacom.
Akizungumza katika uzinduzi wa huduma hiyo jijini Dar es Salaam, Mwakifulefule, alisema huduma hiyo muhimu na yenye tija siyo tu itawanufaisha madaktari na sekta ya afya, bali pia Watanzania wote mijini na vijijini.
Alisema mbali ya kupiga simu bure, wanachama wa mtandao huo kwa kushiriki katika programu hiyo watakuwa na uwezo wa kutuma ujumbe mfupi wa maneno 50 bure kila mwezi kuwasiliana na wenzao waliojisajili ndani ya programu hiyo.
Awali, Taasisi ya Kimataifa inayoshughulika na huduma za mawasiliano (Switchboard) kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari, imewasihi madaktari kujumuika katika program hiyo ili kutathmini mafanikio ya utendaji wao kama wadau na wataalamu ndani ya sekta ya afya.
Alisema suala la upungufu wa madaktari na wataalam wa afya katika mataifa mengi limesababisha daktari au muuguzi mmoja kujikuta akihudumia wagonjwa kati ya 5,000 hadi 150,000.
Programu hiyo inadhaminiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Switchboard na Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom.
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...