Friday, April 12, 2013

TAARIFA YA TCRA KUHUSU UUZAJI, USAJILI NA MATUMIZI YA LAINI ZA SIMU ZA MIKONONI


MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
 
TAARIFA KWA UMMA
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha Serikali
kinachosimamia masuala ya mawasiiliano Tanzania. Mamlaka ilianzishwa kwasheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta.
 
Mwaka 2010, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Sheria la Mawasiliano ya Elektroniki na Posta (EPOCA) kusimamia, pamoja na mambo mengine, uuzaji, usajili na matumizi ya laini za simu za mkononi, ambazo kwa kiingereza zinaitwa “
Subscriber Identification Module”, na kwa kifupi SIM, katika Jamhuri ya Muungano waTanzania. 
 
Mamlaka inapenda kuwakumbusha wananchi kwa ujumla kwamba sheria hiyo imeainisha makosa yanayotokana na kukiuka vipengele vya sheria iliyotajwa hapo juu. 
 
Makosa hayo ni kama ifuatavyo:
a)Kuuza au kusambaza laini ya simu bila kibali cha mtoa huduma za simu
ambaye ana leseni kutoka TCRA;
b)Kutumia laini ya simu ambayo haikusajiliwa;
c)Kutoandikisha taarifa za laini husika kabla ya kuitoa au kuiuza;
d)Kutoa taarifa ya uwongo au maelezo yasiyo sahihi wakati wa kusajili laini
ya simu;
e)Kuchakachua simu ya mkononi au laini ya simu;
Mamlaka inawakumbusha watoa huduma wote na wakala wao kwamba ni wajibu 
 
wao kuzingatia yafuatayo:
a)Kuweka kumbukumbu na taarifa kuhusu wakala
wao wanaouza laini zao za simu;
b)Kuandikisha watumiaji wanaonunua au kupatiwa
laini za simu;
c)Kuhakiki taarifa zinazotolewa waka
ti wa usajili wa laini za simu;
d)Kuhifadhi nakala ya vitambulisho au nyaraka zozote zilizotumika wakati wa
kusajili laini husika ya simu;
e)Kutokutoa taarifa za wateja bila idhini ya Mamlaka husika;
f)Wauzaji wa laini za simu walioidhinishwa wana wajibu wa kuwasilisha
taarifa za wateja kwa watoa huduma;
g)Wauzaji wa laini za simu walioidhinishwa wana wajibu pia wa kutokuuza
laini za simu bila idhini ya Mtoa Huduma;
Kama ilivyoanishwa kwenye sheria ya EPOCA ya mwaka 2010 na Kanuni za
Sheria hiyo za mwaka 2011,masharti ya usajili wa laini za simu ni kama
ifuatavyo: 
 
1.Mtoa huduma au wakala analazimika kujaza fomu ya usajili;
2.Mteja Mtarajiwa anatakiwa kuonyesha mojawapo ya vitambulisho halisi
vyenye picha yake;
•Pasipoti
•Kitambulisho cha kazini
•Leseni ya udereva
•Kadi ya usajili wa Mpiga Kura
•Barua ya utambulisho kutoka Se
rikali za Mitaa ikiwa na picha
•Kitambulisho cha Taifa
•Kitambulisho cha SACCOs
•Kadi ya benki yenye picha
3.Watoa huduma wanatakiwa kuhifadhi ukurasa wa kwanza wa fomu ya usajili;
4.Mteja anatakiwa kupatiwa nakala ya fomu au hati itakayothibitisha kwamba amejisajili;
5.Mtoa huduma au Wakala atabakia na nakala ya kitambulisho 
 
Wateja waliojiandik isha wanaweza kuhakiki usajili wao kwa kupiga *106#.
Mtu yeyote ambaye atakiuka vipengele vya Sheria ya EPOCA ya mwaka 2010 na
kupatikana na hatia kwa mujibu wa vifungu vya Sheria hiyo ataadhibiwa kwa
kutozwa faini au kufungwa jela au vyote kwa pamoja. 
 
Imetolewa na
Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
Mawasiliano Towers
Namba 20, Barabara ya Sam Nujoma Road
S.L.P. 474
14414 Dar es Salaam

Popular Posts

Labels