Friday, April 26, 2013
UNAVYOWEZA KUJILINDA NA PACHIKO AMA PICHA USIZOZIHITAJI KWENYE FACEBOOK ANGALIA HAPA
Kumekuwa na changamoto ya kujilinda na watu ambao wanaweza kukuwekea maelezo ama kukutagg picha usiyoihitaji kwenye timeline yako kwenye facebook iwe ni picha ama ni taarifa mbaya ama usizozihitaji.Na utagundua ya kwamba kuna watu ambao hata huwezi amini kama kweli wao wameweka picha zilizo kinyume na maadili na hii imekuwa ikiwakera wao ama watu wanaowasiliana nao kwenye mtandao wa facebook.
Kama inavyoonekana katika picha hapo juu ukifuata hatua hizo itakusaidia kujilinda kwanza ingia kwa timeline yako kulia mwa ukurasa ama timeline yako kuna kialama kinaonekana kama nyota ukishusha chini kasa yako ya mouse unaenda mahali pameandikwa privacy setting bofya hapo na utatokea ukurasa ambao kushoto kuna maelezo bofya palipo andika Timeline and Tagging.
Baada ya hapo utatokea ukurasa mwingine kulia kwake kuna maandishi meusi yameandikwa who can add things to my timeline hapo kuna mahali pa kuchagua Friends ama Only Me,kama ni friends ina maana rafiki yako yeyote anaweza kukuwekea jambo kwenye timeline yako maana hujaizuia,kama ni only me ina maana wewe tu ndo unayeweza kuweka jambo kwa hiyo utaamua angalia kielelezo namba tatu.
Pia kuna mahali pameandikwa Review Posts friends before they appear on your timeline hapo kuna Enable na Disable hapo utachagua enable maana yake uone kwanza wewe ndo itokea kwenye timeline yako vinginevyo utachagua disable kila rafiki yako aweza weka jambo kwenye timeline yako bila wewe kujua kama wewe huja login.
Hatua nyingine ni suala la kujilinda na picha usizozihitaji zitokee kwenye timeline yako kama mtu amekutagg hatua ni zile zile za mwanzo baada ya kuingia kwenye ukurasa wa privacy setting kuna mahali pameandika timeline and tagging angalia kielelezo namba nne hapo kuna Enable na Disable hiyo nayo inafanyakazi sawa sawa na pachiko hata kama hujalogin,fuatilia vilelezo vya picha kama zinavyoonekana juu.
Kumbuka baada ya kuweka setting hizi facebook watakuwa wanakutumia ujumbe kwa anuani yako ya barua pepe na kwenye timeline yako ukiwa na picha ama maelezo(jambo)ambalo limetumwa kuonekana kwenye timeline yako wewe utaliona kwanza ndo utaamua hiyo picha ama jambo lionekane kwanye timeline yako,pia unaweza hata kujiondoa kwenye hiyo tagg.
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wamiliki wa blog nchini humo inatarajia kuanzisha tuzo za umahiri kwa waandishi wa haba...
-
Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 25 ambaye alidukua komputa za Chuo Kikuu cha Birmingham na kuongeza alama za mtihani amefungwa...
-
Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) inatarajia kuzindua kituo kikubwa cha kuuzia intaneti Afrika Mashariki mwishoni mwa mwezi julai au Agosti mw...
-
Serikali ya Tanzania imesema inatoza kodi ya shilingi 1,000 kwa mwezi kwa kila laini yenye namba ya simu.Umoja wa Makampuni ya mi...
-
Facebook ni mtandao wa kijamii ambao unaendelea kuongoza kwa kuwa na watumiaji wengi duniani hata hiyo utafiti unaonesha kuwa vijana ...
-
Google I/O ni kongamano linalofanyika kila mwaka California kwa kuwakutanisha Developers wa bidhaa za Google kama Android , Chrome , Chrom...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini Tanzania imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu mili...