Friday, April 12, 2013

WATUMIAJI WA SIMU NA INTANETI WAONGEZEKA DUNIANI

Takwimu zilizotolewa na Taasis inayosimamia masuala ya mawasiliano ya Shirika la Umoja wa Mataifa Duniani (ITU) 
Februari ,2013 iliyopo Geneva,Uswisi kupitia kituo chache cha kukusanya takwimu za mawasilliano ya teknolojia ya habari na mawasiliano duniani zinaonesha kuwa watu wanaotumia wa mawasiliano ya simu wamefikia bilioni 6.8 kati ya watu bilioni 7.1 waliopo duniani.

Takwimu hizo zinaonesha kuwa matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa asilimia 96 duniani ambapo asilimia 128 katika nchi zilizoendelea na kwa nchi zinazoendelea ni asilimia 89.

Kwa upande wa mawasiliano ya intaneti watu bilioni 2.7 duniani ambao ni karibia asilimia 40 ndio waliounganishwa katika matumizi ya mawasiliano hayo ambapo wanawake ni asilimia 16 tu.

Katika nchi zinazoendelea asilimia 31 wameunganishwa kwenye mitandao ya komputa ukilinganisha na asilimia 77 ya watu wanaotoka katika nchi zilizoendelea.Ambapo matumizi ya interneti barani Ulaya ni asilimia 75 na nchi za bara la Amerika ni asilimia 65,wakati barani Afrika ni asilimia 16 tu.

Takwimu hizi zinaonesha kuwa kumekuwa na kiwango kikubwa cha matumizi ya intaneti kwa wanaume kuliko wanawake duniani  kwani ni asilimia 37 tu ya wanawake wanaweza kuwa katika mitandao ambapo wanaume ni asilimia 41.

Katika nchi zinazoendelea kuna wanawake milioni 826 wanaotumia intaneti na wanaume ni milioni  980 na katika nchi zilizoendelea wanawake wanaotumia inteneti ni milioni  475 ambapo wanaume ni milioni 483.Ambapo inaonekana kuna tofauti ya asilimia 16 kati ya wanaume na wanawake katika matumizi ya teknolojia hiyo ya mawasiliano katika nchi zinazoendelea na katika nchi zilizoendelea ni tofauti ya asilimia 2 tu.

Takwimu hizo pia zinaonesha kuwa inakadiliwa kuwa  kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 jumla ya kaya 750 ambazo ni sawa na asilimia 41 duniani ndizo ambazo zitakuwa zimeunganishwa na mawasiliano ya intaneti.

Popular Posts

Labels