Takwimu zilizotolewa na Taasis inayosimamia masuala ya mawasiliano ya Shirika la Umoja wa Mataifa Duniani (ITU)
Februari
,2013 iliyopo Geneva,Uswisi kupitia kituo chache cha kukusanya
takwimu za mawasilliano ya teknolojia ya habari na mawasiliano duniani zinaonesha kuwa watu wanaotumia wa
mawasiliano ya simu wamefikia bilioni 6.8 kati ya watu bilioni 7.1
waliopo duniani.
Takwimu
hizo zinaonesha kuwa matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa
asilimia 96 duniani ambapo asilimia 128 katika nchi zilizoendelea na kwa
nchi zinazoendelea ni asilimia 89.
Kwa
upande wa mawasiliano ya intaneti watu bilioni 2.7 duniani ambao ni
karibia asilimia 40 ndio waliounganishwa katika matumizi ya mawasiliano
hayo ambapo wanawake ni asilimia 16 tu.
Katika
nchi zinazoendelea asilimia 31 wameunganishwa kwenye mitandao ya
komputa ukilinganisha na asilimia 77 ya watu wanaotoka katika nchi
zilizoendelea.Ambapo matumizi ya interneti barani Ulaya ni asilimia 75
na nchi za bara la Amerika ni asilimia 65,wakati barani Afrika ni
asilimia 16 tu.
Takwimu
hizi zinaonesha kuwa kumekuwa na kiwango kikubwa cha matumizi ya
intaneti kwa wanaume kuliko wanawake duniani kwani ni asilimia 37 tu ya
wanawake wanaweza kuwa katika mitandao ambapo wanaume ni asilimia 41.
Katika
nchi zinazoendelea kuna wanawake milioni 826 wanaotumia intaneti na
wanaume ni milioni 980 na katika nchi zilizoendelea wanawake wanaotumia
inteneti ni milioni 475 ambapo wanaume ni milioni 483.Ambapo
inaonekana kuna tofauti ya asilimia 16 kati ya wanaume na wanawake
katika matumizi ya teknolojia hiyo ya mawasiliano katika nchi
zinazoendelea na katika nchi zilizoendelea ni tofauti ya asilimia 2 tu.
Takwimu
hizo pia zinaonesha kuwa inakadiliwa kuwa kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 jumla ya kaya
750 ambazo ni sawa na asilimia 41 duniani ndizo ambazo zitakuwa
zimeunganishwa na mawasiliano ya intaneti.
Popular Posts
-
Kitabu hiki kipo tayari. Wasiliana kwa namba 0713 309 314 au 0763 309 314 na Mushi Richard, Mpesa: 0755872462, Tigopesa: 0713643703 ...
-
Katika wiki chache zilizopita kulikuwa na msuguano kati ya serikali ya Marekani na China , Serikali ya Marekani inailaumu china kwa kufany...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginev...
-
Mtandao wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha. Nia...
-
Bwana. Keriako Tobiko Mkurugenzi wa Mashtaka ya umma ya nchini Kenya Bwana. Keriako Tobiko ametangaza kuanzishwa kwa kitengo maalum...
-
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA UMMA Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha...
-
Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya iOS 12.2 kwa ajili ya iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivy...
-
Kuna Utapeli umeanza kusambaa saa chache zilizopita kupitia CRDB INTERNET BANKING . Anayefanya utapeli huu ametengeneza majina band...
-
Waziri na waziri wa uchukuzi Dr Harrison mwakyembe amesema kuwa Teknolojia ya kisasa inayotumika katika uwanja wa ndege wa kimataifa...
-
Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani mkoani Dar es salaam limeanzisha kanuni ya tozo la papo kwa hapo kwa njia ya kiel...