Takwimu zilizotolewa na Taasis inayosimamia masuala ya mawasiliano ya Shirika la Umoja wa Mataifa Duniani (ITU)
Februari
,2013 iliyopo Geneva,Uswisi kupitia kituo chache cha kukusanya
takwimu za mawasilliano ya teknolojia ya habari na mawasiliano duniani zinaonesha kuwa watu wanaotumia wa
mawasiliano ya simu wamefikia bilioni 6.8 kati ya watu bilioni 7.1
waliopo duniani.
Takwimu
hizo zinaonesha kuwa matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa
asilimia 96 duniani ambapo asilimia 128 katika nchi zilizoendelea na kwa
nchi zinazoendelea ni asilimia 89.
Kwa
upande wa mawasiliano ya intaneti watu bilioni 2.7 duniani ambao ni
karibia asilimia 40 ndio waliounganishwa katika matumizi ya mawasiliano
hayo ambapo wanawake ni asilimia 16 tu.
Katika
nchi zinazoendelea asilimia 31 wameunganishwa kwenye mitandao ya
komputa ukilinganisha na asilimia 77 ya watu wanaotoka katika nchi
zilizoendelea.Ambapo matumizi ya interneti barani Ulaya ni asilimia 75
na nchi za bara la Amerika ni asilimia 65,wakati barani Afrika ni
asilimia 16 tu.
Takwimu
hizi zinaonesha kuwa kumekuwa na kiwango kikubwa cha matumizi ya
intaneti kwa wanaume kuliko wanawake duniani kwani ni asilimia 37 tu ya
wanawake wanaweza kuwa katika mitandao ambapo wanaume ni asilimia 41.
Katika
nchi zinazoendelea kuna wanawake milioni 826 wanaotumia intaneti na
wanaume ni milioni 980 na katika nchi zilizoendelea wanawake wanaotumia
inteneti ni milioni 475 ambapo wanaume ni milioni 483.Ambapo
inaonekana kuna tofauti ya asilimia 16 kati ya wanaume na wanawake
katika matumizi ya teknolojia hiyo ya mawasiliano katika nchi
zinazoendelea na katika nchi zilizoendelea ni tofauti ya asilimia 2 tu.
Takwimu
hizo pia zinaonesha kuwa inakadiliwa kuwa kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 jumla ya kaya
750 ambazo ni sawa na asilimia 41 duniani ndizo ambazo zitakuwa
zimeunganishwa na mawasiliano ya intaneti.
Popular Posts
-
Wanasayansi wa maabara ya Bristol Robotics Uingereza wamegundua njia ya kutumia mkojo kama chanzo cha kuzalisha umeme wa kuchaji bet...
-
Maelfu ya tarakirishi (kompyuta) za mitandao ya mashirika makubwa kadhaa duniani yamedukuliwa na kutekwa na watekaji wanadai malipo ...
-
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaanza kutumia tiketi za elektroniki kwenye uwanja wa Azam uliopo Chamazi,Dar es salaam w...
-
Wakulima nchini Nigeria wamepewa bure simu za mikononi,Ingawa vyama vya upinzani vinakandia hali hiyo wananchi wengi wanaamini huo ni...
-
Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa M...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetoa viwango vipya vya bei elekezi ya gharama za kupiga simu kwa mwingiliano wa mitandao ya ma...
-
Mwaka 2014 Umekua wenye changamoto nyingi sana kwenye upande wa mitandao ambapo wahalifu mtandao walifanikiwa kwa kiasi kikubwa san...
-
Maafisa wa utawala katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, wamebana matumizi ya ujumbe mfupi wa simu za mkononi baada ya kusema kuwa ni t...
-
Shirika la kujiolea la nchini Marekani linalojihusisha na utabibu na masuala ya haki za binadamu (PHR) limetengeneza program tumishi mp...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuanzia sasa itakamata mtu yoyote anayesajili laini za simu kwa kuchakachua au bila kuf...