Takwimu zilizotolewa na Taasis inayosimamia masuala ya mawasiliano ya Shirika la Umoja wa Mataifa Duniani (ITU)
Februari
,2013 iliyopo Geneva,Uswisi kupitia kituo chache cha kukusanya
takwimu za mawasilliano ya teknolojia ya habari na mawasiliano duniani zinaonesha kuwa watu wanaotumia wa
mawasiliano ya simu wamefikia bilioni 6.8 kati ya watu bilioni 7.1
waliopo duniani.
Takwimu
hizo zinaonesha kuwa matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa
asilimia 96 duniani ambapo asilimia 128 katika nchi zilizoendelea na kwa
nchi zinazoendelea ni asilimia 89.
Kwa
upande wa mawasiliano ya intaneti watu bilioni 2.7 duniani ambao ni
karibia asilimia 40 ndio waliounganishwa katika matumizi ya mawasiliano
hayo ambapo wanawake ni asilimia 16 tu.
Katika
nchi zinazoendelea asilimia 31 wameunganishwa kwenye mitandao ya
komputa ukilinganisha na asilimia 77 ya watu wanaotoka katika nchi
zilizoendelea.Ambapo matumizi ya interneti barani Ulaya ni asilimia 75
na nchi za bara la Amerika ni asilimia 65,wakati barani Afrika ni
asilimia 16 tu.
Takwimu
hizi zinaonesha kuwa kumekuwa na kiwango kikubwa cha matumizi ya
intaneti kwa wanaume kuliko wanawake duniani kwani ni asilimia 37 tu ya
wanawake wanaweza kuwa katika mitandao ambapo wanaume ni asilimia 41.
Katika
nchi zinazoendelea kuna wanawake milioni 826 wanaotumia intaneti na
wanaume ni milioni 980 na katika nchi zilizoendelea wanawake wanaotumia
inteneti ni milioni 475 ambapo wanaume ni milioni 483.Ambapo
inaonekana kuna tofauti ya asilimia 16 kati ya wanaume na wanawake
katika matumizi ya teknolojia hiyo ya mawasiliano katika nchi
zinazoendelea na katika nchi zilizoendelea ni tofauti ya asilimia 2 tu.
Takwimu
hizo pia zinaonesha kuwa inakadiliwa kuwa kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 jumla ya kaya
750 ambazo ni sawa na asilimia 41 duniani ndizo ambazo zitakuwa
zimeunganishwa na mawasiliano ya intaneti.
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakitoa elimu jinsi ya kut...
-
Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Simu katika Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Ndugu John Mwera akizungumza ...
-
Kanisa la Waadventista Wa Sabato mwaka huu litashiriki mkutano wa Waadventista watalaamu wa mawasilino ya Intaneti duniani (GAiN) kwa k...
-
If you've already bought a smart phone, you'll know the importance of choosing a good OS for it. With the versions of all the giant...
-
Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...
-
Wataalamu wa Teknolojia nchini Ghana wamebuni teknolojia ya kuhakiki ikiwa dawa ni bandia au ni halisi. Teknolojia hiyo iliyozindul...
-
New software which mines data from social networks to track people's movements and even predict future behaviour poses a 'very ...