Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) kupitia Mkurugenzi wake Mkuu Profesa John Nkoma imesema namba za simu zilizosajiliwa nchini humo ni asilimia 93 na asilimia 7 hazijasajiliwa na kwamba asilimia iliyobaki inatakiwa kuondoka.
Akizungumza na wadau wa mawasiliano jijini Dar es salaam jana Mkurungenzi huyo amesema kuwa namba za simu lazima zisajiliwe kwa mujibu wa sheria ya Mawasiliano ya Elekroniki na Posta (EPOCA) ya mwaka 2010.
Amesema kisheria mtu anayetumia simu isiyosajiliwa akikamatwa anaweza kutozwa faini ya shilingi 50,000 za kitanzania ama kwenda jela miezi sita.
Katika vikao vya pamoja vilivyofanyika Aprili 4 na Aprili 11 mwaka huu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na kampuni zinazotoa huduma za simu za mkononi,zimekubaliana kuchukua hatua za kumaliza tatizo la usajili wa namba za simu na utaratibu wa kufungia namba zote ambazo hazikusajiliwa.
Profesa Nkoma amesema kuwa kwa kushirikiana na kampuni za simu na vyombo vya usalama imeanza kampeni endelevu ili kuwabaini wanaohusika na uvunjifu wa sheria kwa lengo la kuwalinda watumiaji wema.
Popular Posts
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya ...
-
Watu wanne huko nchini Marekani wameushitaki mtandao wa kijamii wa LinkedIn unaowaunganisha wanataaluma kuwa umekuwa ukii...
-
Facebook imekuwa kama Google ya mitandao ya kijamii. kama sasa hivi hauposti status yako basi unapandisha picha au unajibu quiz ...
-
Kwa watumiaji wa Facebook na mitandao jamii mingine jaribuni kuwa makini na kile mnachokiweka ama kutoa maoni katika suala lolote kwenye kur...
-
Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa Wizara ya Sheria nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kwa kile kinachosemekana ni ufichuaj...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
Akaunti ya Twitter ya kundi la wanamgambo wa Al Shabaab imesitishwa kwa mara nyingine. Ujumbe kutoka kwa Twitter katika akaunti yake ...