Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania imeamua kusitisha awamu ya pili ya kuzima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali,ili kufanya tathimini yaliyojiri katika awamu ya kwanza.
Kwa mujibu wa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa amesema hatua hiyo ni ya muda ili kupisha tathimini hiyo.
Profesa Mbarawa alisema serikali haina mpango wa kusitisha kuwasha mitambo ya dijitali na kuzima ya analojia bali inachofanya sasa ni kuhakikisha mchakato mzima wa dijitali unafanikiwa nchini.
Awamu ya kwanza ya uzimaji wa mitambo ya analojia ilihusisha mikoa saba ikiwemo mikoa ya Dar es salaam,Tanga,Dodoma,Mwanza,Arusha na Mbeya inayotarajiwa kuzimwa rasmi mitambo yake mwishoni mwa mwezi huu.
Awamu ya pili inayotarajiwa kuanza wakati wowote na kuhusisha mikoa zaidi ya 14,wizara hiyo kwa kushirikiana na wadau na kamati za Bunge ya Miundombinu walikubaliana kwa kuda hadi tathmini ya kina itakapofanyika katika mikoa saba iliyoanza kutumia mfumo mpya wa dijitali.
Waziri huyo amesema kuwa msimamo wa serikali kuhusu suala hilo la matumizi ya dijitali ni kuhakikisha kuwa hadi ifikapo juni 17,2015 dunia nzima itazima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali na hivyo Tanzania nzima itakuwa tayali inatumia mfumo huo mpya.
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...