Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania imeamua kusitisha awamu ya pili ya kuzima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali,ili kufanya tathimini yaliyojiri katika awamu ya kwanza.
Kwa mujibu wa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa amesema hatua hiyo ni ya muda ili kupisha tathimini hiyo.
Profesa Mbarawa alisema serikali haina mpango wa kusitisha kuwasha mitambo ya dijitali na kuzima ya analojia bali inachofanya sasa ni kuhakikisha mchakato mzima wa dijitali unafanikiwa nchini.
Awamu ya kwanza ya uzimaji wa mitambo ya analojia ilihusisha mikoa saba ikiwemo mikoa ya Dar es salaam,Tanga,Dodoma,Mwanza,Arusha na Mbeya inayotarajiwa kuzimwa rasmi mitambo yake mwishoni mwa mwezi huu.
Awamu ya pili inayotarajiwa kuanza wakati wowote na kuhusisha mikoa zaidi ya 14,wizara hiyo kwa kushirikiana na wadau na kamati za Bunge ya Miundombinu walikubaliana kwa kuda hadi tathmini ya kina itakapofanyika katika mikoa saba iliyoanza kutumia mfumo mpya wa dijitali.
Waziri huyo amesema kuwa msimamo wa serikali kuhusu suala hilo la matumizi ya dijitali ni kuhakikisha kuwa hadi ifikapo juni 17,2015 dunia nzima itazima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali na hivyo Tanzania nzima itakuwa tayali inatumia mfumo huo mpya.
Popular Posts
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya ...
-
Watu wanne huko nchini Marekani wameushitaki mtandao wa kijamii wa LinkedIn unaowaunganisha wanataaluma kuwa umekuwa ukii...
-
Facebook imekuwa kama Google ya mitandao ya kijamii. kama sasa hivi hauposti status yako basi unapandisha picha au unajibu quiz ...
-
Kwa watumiaji wa Facebook na mitandao jamii mingine jaribuni kuwa makini na kile mnachokiweka ama kutoa maoni katika suala lolote kwenye kur...
-
Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa Wizara ya Sheria nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kwa kile kinachosemekana ni ufichuaj...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
Akaunti ya Twitter ya kundi la wanamgambo wa Al Shabaab imesitishwa kwa mara nyingine. Ujumbe kutoka kwa Twitter katika akaunti yake ...