Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania imeamua kusitisha awamu ya pili ya kuzima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali,ili kufanya tathimini yaliyojiri katika awamu ya kwanza.
Kwa mujibu wa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa amesema hatua hiyo ni ya muda ili kupisha tathimini hiyo.
Profesa Mbarawa alisema serikali haina mpango wa kusitisha kuwasha mitambo ya dijitali na kuzima ya analojia bali inachofanya sasa ni kuhakikisha mchakato mzima wa dijitali unafanikiwa nchini.
Awamu ya kwanza ya uzimaji wa mitambo ya analojia ilihusisha mikoa saba ikiwemo mikoa ya Dar es salaam,Tanga,Dodoma,Mwanza,Arusha na Mbeya inayotarajiwa kuzimwa rasmi mitambo yake mwishoni mwa mwezi huu.
Awamu ya pili inayotarajiwa kuanza wakati wowote na kuhusisha mikoa zaidi ya 14,wizara hiyo kwa kushirikiana na wadau na kamati za Bunge ya Miundombinu walikubaliana kwa kuda hadi tathmini ya kina itakapofanyika katika mikoa saba iliyoanza kutumia mfumo mpya wa dijitali.
Waziri huyo amesema kuwa msimamo wa serikali kuhusu suala hilo la matumizi ya dijitali ni kuhakikisha kuwa hadi ifikapo juni 17,2015 dunia nzima itazima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali na hivyo Tanzania nzima itakuwa tayali inatumia mfumo huo mpya.
Popular Posts
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
China imezifungia tovuti 110 ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuzuia masuala ya ngono kwenye mitandao.Imeeleza taarifa ya serikal...
-
Bunduki ya plastiki iliyotengenezwa kwa mashine ya 3D ikifyatua risasi wakati wa majaribio Photo credits: Screenshot from ATF Video Kam...
-
Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa M...
-
Program Tumishi maarufu ya mawasiliano ya ujumbe wa papo kwa papo katika simu za BlackBerry inayojulikana kwa jina la BlackBerry Mes...
-
Mtandao wa kijamii wa Facebook umenunua programu tumishi ya huduma za ujumbe mfupi wa maneno ya WhatsApp kwa dola za marekani bilioni ...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya kati imewataka watangazaji wa radio, luninga na mitandao ya kijamii kuwa makini na hab...
-
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) jana imekabidhi mradi wa mawasiliano utaotumiwa katika mikoa 12 ya Tanzania kwa ofisi ya Mkaguzi na ...
-
Kampuni ya Google kupitia huduma yake ya kutafuta jambo sasa imeanzisha utaratibu wa kutoa majibu ya moja kwa moja kwa maswali kuhus...