Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania imeamua kusitisha awamu ya pili ya kuzima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali,ili kufanya tathimini yaliyojiri katika awamu ya kwanza.
Kwa mujibu wa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa amesema hatua hiyo ni ya muda ili kupisha tathimini hiyo.
Profesa Mbarawa alisema serikali haina mpango wa kusitisha kuwasha mitambo ya dijitali na kuzima ya analojia bali inachofanya sasa ni kuhakikisha mchakato mzima wa dijitali unafanikiwa nchini.
Awamu ya kwanza ya uzimaji wa mitambo ya analojia ilihusisha mikoa saba ikiwemo mikoa ya Dar es salaam,Tanga,Dodoma,Mwanza,Arusha na Mbeya inayotarajiwa kuzimwa rasmi mitambo yake mwishoni mwa mwezi huu.
Awamu ya pili inayotarajiwa kuanza wakati wowote na kuhusisha mikoa zaidi ya 14,wizara hiyo kwa kushirikiana na wadau na kamati za Bunge ya Miundombinu walikubaliana kwa kuda hadi tathmini ya kina itakapofanyika katika mikoa saba iliyoanza kutumia mfumo mpya wa dijitali.
Waziri huyo amesema kuwa msimamo wa serikali kuhusu suala hilo la matumizi ya dijitali ni kuhakikisha kuwa hadi ifikapo juni 17,2015 dunia nzima itazima mitambo ya analojia na kuwasha dijitali na hivyo Tanzania nzima itakuwa tayali inatumia mfumo huo mpya.
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Unapomblock mtu kwenye viber inamaana umezuia kuwasiliana na mtu yoyote kwa njia yoyote katika mtandao wa kijamii wa viber,huta...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya ...