Serikali ya Tanzania imesema itawachukulia hatua kali za kisheria kwa mtu yeyote atakayebainika kutumia vibaya simu za mikononi na mitandao ya kijamii kuleta uchochezi au kwenda kinyume na maadili ya nchi hiyo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mwishoni mwa juma Waziri wa Sayansi na Teknolojia,Makame Mbarawa amesema lengo la kufanya hivyo ni kukomesha vitendo vya hatarai vinavyoonekana kukua siku hadi siku nchini Tanzania.
Amesema hatua zitachukuliwa dhidi ya kampuni au mtu yeyote atakayetumia njia hizo za mawasiliano kutoa kashfa ama kuitukana serikali,viongozi wa serikali,dini,siasa na watu binafsi kwa kuwa vitendo hivyo vinakiuka sheria za nchini.
Hatua hizo za serikali pia zitawahusu watu wote wanaojihusisha na uonyeshaji kwenye mitandao hiyo picha za ngono,unyanyasaji wa watoto na ukiukwaji wa maadili na kutoa taarifa zenye lengo la kuvunja utulivu na amani.
Teknolojia ya habari na mawasiliano katika miaka ya hivi karibuni imechangia kuleta maendeleo nchini Tanzania lakini baadhi ya watu wanaitumia kwa mambo yasiyofaa ikiwa ni pamoja na wizi,ujambazi,ubakaji,biashara ya dawa za kulevya, ukahaba na kusambaza siri za watu binafsi bila idhini ya wahusika.
Popular Posts
-
Bwana. Keriako Tobiko Mkurugenzi wa Mashtaka ya umma ya nchini Kenya Bwana. Keriako Tobiko ametangaza kuanzishwa kwa kitengo maalum...
-
Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya iOS 12.2 kwa ajili ya iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivy...
-
Kuna Utapeli umeanza kusambaa saa chache zilizopita kupitia CRDB INTERNET BANKING . Anayefanya utapeli huu ametengeneza majina band...
-
Kitabu hiki kipo tayari. Wasiliana kwa namba 0713 309 314 au 0763 309 314 na Mushi Richard, Mpesa: 0755872462, Tigopesa: 0713643703 ...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginev...
-
Mtandao wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha. Nia...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA UMMA Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha...