Serikali ya Tanzania imesema itawachukulia hatua kali za kisheria kwa mtu yeyote atakayebainika kutumia vibaya simu za mikononi na mitandao ya kijamii kuleta uchochezi au kwenda kinyume na maadili ya nchi hiyo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mwishoni mwa juma Waziri wa Sayansi na Teknolojia,Makame Mbarawa amesema lengo la kufanya hivyo ni kukomesha vitendo vya hatarai vinavyoonekana kukua siku hadi siku nchini Tanzania.
Amesema hatua zitachukuliwa dhidi ya kampuni au mtu yeyote atakayetumia njia hizo za mawasiliano kutoa kashfa ama kuitukana serikali,viongozi wa serikali,dini,siasa na watu binafsi kwa kuwa vitendo hivyo vinakiuka sheria za nchini.
Hatua hizo za serikali pia zitawahusu watu wote wanaojihusisha na uonyeshaji kwenye mitandao hiyo picha za ngono,unyanyasaji wa watoto na ukiukwaji wa maadili na kutoa taarifa zenye lengo la kuvunja utulivu na amani.
Teknolojia ya habari na mawasiliano katika miaka ya hivi karibuni imechangia kuleta maendeleo nchini Tanzania lakini baadhi ya watu wanaitumia kwa mambo yasiyofaa ikiwa ni pamoja na wizi,ujambazi,ubakaji,biashara ya dawa za kulevya, ukahaba na kusambaza siri za watu binafsi bila idhini ya wahusika.
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wamiliki wa blog nchini humo inatarajia kuanzisha tuzo za umahiri kwa waandishi wa haba...
-
Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 25 ambaye alidukua komputa za Chuo Kikuu cha Birmingham na kuongeza alama za mtihani amefungwa...
-
Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) inatarajia kuzindua kituo kikubwa cha kuuzia intaneti Afrika Mashariki mwishoni mwa mwezi julai au Agosti mw...
-
Serikali ya Tanzania imesema inatoza kodi ya shilingi 1,000 kwa mwezi kwa kila laini yenye namba ya simu.Umoja wa Makampuni ya mi...
-
Facebook ni mtandao wa kijamii ambao unaendelea kuongoza kwa kuwa na watumiaji wengi duniani hata hiyo utafiti unaonesha kuwa vijana ...
-
Google I/O ni kongamano linalofanyika kila mwaka California kwa kuwakutanisha Developers wa bidhaa za Google kama Android , Chrome , Chrom...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini Tanzania imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu mili...