Serikali ya Tanzania imesema itawachukulia hatua kali za kisheria kwa mtu yeyote atakayebainika kutumia vibaya simu za mikononi na mitandao ya kijamii kuleta uchochezi au kwenda kinyume na maadili ya nchi hiyo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mwishoni mwa juma Waziri wa Sayansi na Teknolojia,Makame Mbarawa amesema lengo la kufanya hivyo ni kukomesha vitendo vya hatarai vinavyoonekana kukua siku hadi siku nchini Tanzania.
Amesema hatua zitachukuliwa dhidi ya kampuni au mtu yeyote atakayetumia njia hizo za mawasiliano kutoa kashfa ama kuitukana serikali,viongozi wa serikali,dini,siasa na watu binafsi kwa kuwa vitendo hivyo vinakiuka sheria za nchini.
Hatua hizo za serikali pia zitawahusu watu wote wanaojihusisha na uonyeshaji kwenye mitandao hiyo picha za ngono,unyanyasaji wa watoto na ukiukwaji wa maadili na kutoa taarifa zenye lengo la kuvunja utulivu na amani.
Teknolojia ya habari na mawasiliano katika miaka ya hivi karibuni imechangia kuleta maendeleo nchini Tanzania lakini baadhi ya watu wanaitumia kwa mambo yasiyofaa ikiwa ni pamoja na wizi,ujambazi,ubakaji,biashara ya dawa za kulevya, ukahaba na kusambaza siri za watu binafsi bila idhini ya wahusika.
Popular Posts
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya ...
-
Watu wanne huko nchini Marekani wameushitaki mtandao wa kijamii wa LinkedIn unaowaunganisha wanataaluma kuwa umekuwa ukii...
-
Facebook imekuwa kama Google ya mitandao ya kijamii. kama sasa hivi hauposti status yako basi unapandisha picha au unajibu quiz ...
-
Kwa watumiaji wa Facebook na mitandao jamii mingine jaribuni kuwa makini na kile mnachokiweka ama kutoa maoni katika suala lolote kwenye kur...
-
Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa Wizara ya Sheria nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kwa kile kinachosemekana ni ufichuaj...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
Akaunti ya Twitter ya kundi la wanamgambo wa Al Shabaab imesitishwa kwa mara nyingine. Ujumbe kutoka kwa Twitter katika akaunti yake ...