Saturday, April 13, 2013

UKWELI KUHUSU FACEBOOK HOME KATIKA SIMU ZA ANDROID

Facebook Home
 Facebook wametangaza kitu kipya kwa simu za Android walichokipa jina la Home. Kwa muda mrefu kulikuwa na uvumi kuwa Facebook wanajiandaa kuja na simu yao mpya na hata siku za karibuni ilipotangazwa kutakuwa na tamko toka Facebook uvumi ulisambaa kuwa wanatangaza simu yao mpya lakini haikuwa hivyo.

Mark Zuckerberg, CEO wa Facebook amesema lengo hasa ni kufanya unapowasha simu yako kitu cha kwanza kinachotokea ni watu ulionao Facebook ambapo utatokea ujumbe wa kukufahamisha ujumbe waliokuandikia, maoni na hata tags na utaweza kujibu bila kufungua application yoyote. Yote hii ni kwa ajili ya kuingia katika mfumo wa matangazo kupitia mobile web kwani ni sehemu pekee ambayo Facebook haijaweza kuweka ads zake. 
Android ambayo kwa siku za karibuni imekuwa na watumiaji wengi duniani inaonekana kuwa sehemu pekee ambayo Facebook inaweza kuanzisha utaratibu wa matangazo kwa gharama nafuu kulinganisha na kama wangeamua kuja na simu zao wenyewe.

Layers

Nini Utaweza Kufanya
Pamoja na kuwa na uwezo wa kusoma kila kinachoendelea kwenye account yako ya Facebook pale unapowasha simu, utaweza pia kutuma message wakati ukiendelea kutumia program tumishi nyingine kama Whatsapp au Keek kwa kutumia kitu kilichopewa jina la “Chat Heads”. Ikitokea ukapata message kwa mfano wakati unatumia Instagram, picha ya aliekuandikia itatokeza kwa juu na utaweza kujibu kwa kubofya bila kuacha ulichokuwa unakifanya.


App Launcher

Utaipataje?
App hii imeanza kupatika katika Google Play Store kuanzia April 12. Kama tayari unayo Facebook Messenger au Facebook tumishi yoyote utaombwa uijaribu Home. Ukishaiweka na kuanza kuitumia utagundua kitu kinachoitwa “Chat Heads” ambayo inachukua nafasi ya Facebook Messenger.
Simu Gani Zitakuwa Nayo:

Facebook Home on select phones

Simu zitakazoanza nayo ni HTC One, HTC One X, HTC One X+, Samsung Galaxy S3, Samsung Galaxy S4, na Samsung Galaxy Note II. Simu nyingine zitaongezwa baadae.
Ili kuondokana na usumbufu wa kuiweka kwa kuipakua kwenye Google Store, simu zitakazoanza kutengenezwa baadae zitakuwa zinayo Home moja kwa moja na kwa kuanza HTC watakuwa wa mwanzo kuiweka Home katika simu zao zinazotoka hivi karibuni.



Chanzo:Tanganyikanblog

Popular Posts

Labels