Monday, January 5, 2015

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI NCHINI TANZANIA YAKIRI MASHINE ZA BVR ZILIZOTUMIKA KWA MAJARIBIO HAZIFAI



Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania (NEC) imekiri kuwa mashine 250 zilizotumika katika zoezi la majaribio la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa kielektroniki (BVR) lililofanyika mwezi uliopita katika majimbo matatu nchini, hazifai.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu tathimini ya utekelezaji wa majaribio ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia mfumo wa BVR.

Jaji Lubuva amesema changamoto zilizojitokeza katika majaribio hayo ambayo yalihusisha watu 41,721 ni pamoja na matatizo ya programu za mifumo ya kompyuta na hali ya hewa ya joto ambayo iliharibu urahisi wa utendaji kazi wa mashine hizo.

Amesema kompyuta mpakato zilizokuwa zikitumika katika kazi hiyo ziliwekewa bati la kuzuia zisiibiwe kwa urahisi lakini iligundulika baadaye kuwa bati hilo lilikuwa likizuia mzunguko wa hewa ndani ya mashine hizo.

Lubuva amesema Zoezi hilo linatarajia kugharimu Shilingi bilioni 293 za kitanzania  ambapo  vitambulisho hivyo ndivyo vitakavyotumika katika upigaji wa kura ya maoni ya Katiba mpya mwezi Machi pamoja na Uchaguzi Mkuu Oktoba.

Katika hotuba yake ya salamu za mwaka mpya wa 2015  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete amesema

Moja ya mambo muhimu ambayo Tume ya Uchaguzi inafanya kwa sasa ni kuandikisha wapiga kura katika Daftari la Mpiga Kura. Tume imeamua kutumia mfumo mpya wa Biometric Voters Register. Uandikishaji wa majaribio umefanyika katika baadhi ya Kata katika Majimbo ya Mlele, Kawe na Kilombero. Matatizo yaliyojitokeza yatasaidia kuboresha mfumo huo kabla ya uandikishaji wa watu wote wenye sifa stahiki kuanza.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win
Moja ya mambo muhimu ambayo Tume ya Uchaguzi inafanya kwa sasa ni kuandikisha wapiga kura katika Daftari la Mpiga Kura. Tume imeamua kutumia mfumo mpya wa Biometric Voters Register. Uandikishaji wa majaribio umefanyika katika baadhi ya Kata katika Majimbo ya Mlele, Kawe na Kilombero. Matatizo yaliyojitokeza yatasaidia kuboresha mfumo huo kabla ya uandikishaji wa watu wote wenye sifa stahiki kuanza.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win
Tume imeamua kutumia mfumo mpya wa Biometric Voters Register. Uandikishaji wa majaribio umefanyika katika baadhi ya Kata katika Majimbo ya Mlele, Kawe na Kilombero. Matatizo yaliyojitokeza yatasaidia kuboresha mfumo huo kabla ya uandikishaji wa watu wote wenye sifa stahiki kuanza.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_wi


Tume imeamua kutumia mfumo mpya wa Biometric Voters Register na uandikishajiwa majaribio umefanyika katika baadhi ya Kata katika Majimbo ya Mlele, Kawe na Kilombero na kuleeza kuwa matatizo yaliyojitokeza yatasaidia kuboresha mfumo huo kabla ya uandikishaji wa watu wote wenye sifa stahiki kuanza.
Napenda kutumia nafasi hii kuwafahamisha Watanzania wenzangu wote kuwa mfumo mpya unatengeneza Daftari Jipya la Mpiga Kura ingawaje lugha inayotumika ni uboreshaji wa Daftari la sasa. Uboreshaji huu wa Daftari la Mpiga Kura ni tofauti na ule tuliouzoea ambapo walikuwa wanaandikishwa wapiga kura wapya na wale waliopoteza vitambulisho vyao. Safari hii wanaandikishwa wote wapya na wa zamani na wote watapata vitambulisho vipya. Hivyo basi, sisi wenye vitambulisho vya kupiga kura vya zamani tusifanye ajizi, tujitokeze kujiandikisha wakati ukifika.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_wi




Wednesday, December 31, 2014

TUUFUNGE MWAKA NA KUANZA MWAKA KWA KUJIHADHARI NA UHALIFU MTANDAO

 
Mwaka 2014 Umekua wenye changamoto nyingi sana kwenye upande wa mitandao ambapo wahalifu mtandao walifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuitikisa anga ya usalama mitandao duniani kote ambapo walifikia kutamba kuwa wameshinda mapambano na wanausalama mitandao.

Kubwa zaidi ni uelewa mdogo wa watumiaji mtandao juu ya kujiweka salama kimtandao iliyoambatana na wana usalama mitandao kuwa wachache sana katika ngazi ya kidunia huku baadhi ya mataifa kutotoa kipaumbele katika maswala ya usalama mitandao.

Aidha, Mengi katika jitihada yameweza kufikiwa ikiwa ni pamoja na Kikao cha funga mwaka cha tathmini ya hali ilivyokuwa kwa mwaka 2014 ambapo iliweza kutabiri hali ya uhalifu mwaka 2015 na kuweka mikakati ya dhati ya kukabiliana na hali hiyo kwa mwaka 2015 inayotegemewa kuwa na matokeo chanya. Kwenye hili unaweza kulisoma kwenye  “TAARIFA FUPI INAYOSOMEKA HAPA"

Wamarekani nao kupitia “US department of Justice” wameamua kuazisha kitengo maalum kitakachotoa msaada kwa mataifa yote duniani katika upande wa maswala ya usalama mitandao ikisisitiza itaangazia zaidi katika kuzuia matatizo kabla hayajatokea.

Tanzania nayo haikubaki nyumba kwenye hili, Tumeshuhudia warsha, semina, kongamano na mikutano mingine yenye malengo thabiti ya kukuza na kuongezea uwezo wa uelewa wa matumizi salama ya mitandao paoja kukuza uwezo wa kukabiliana na hali ya uhalifu mtandao nchini.


Sheria za usalama mitandao zimeweza kupaziwa sauti na kutoa matumaini makubwa kwa mwaka ujao, Huku vyombo vya habari kuw na jitihada ya dhati katika kampeni ya kutoa elimu na kuhabarisha jamii kuhusiana na janga la uhalifu mtandao linaloweza kuleta athari zaidi kwa taifa.

Nikumbushe tu, Uhalifu Mtandao umeendelea kuja kwa kasi ya juu na njia ambazo watanzania wengi wameweza kuwa waathirika. Kubwa nililoliona ambalo kueleke mwisho wa mwaka limeweza kukamata kasi ni pamoja na uhalifu aina ya “Phishing kama unavyo onekana kwenye picha nilizo tumiwa na baadhi ya raia wema ambapo wengi wameendelea kuathiriwa na uhalifu huu wa kimtandao.
Umakini zaidi unahitajika na tumalize mwaka kwa kuwa salama kimtandao.
Na:Yusuph Kileo

Wednesday, December 24, 2014

SEMINA YA USALAMA KATIKA MITANDAO YAFANYIKA DIT



Mtaalaam wa Masuala ya Usalama kwenye Mitandao Yusuph Kileo akitoa mada





Mshiriki akiuliza swali

Mshiriki wa Semina akiwa ameshikilia zawadi yake baada ya kujibu maswali

Washiriki wakiuliza maswali

Desemba 23 mwaka huu mtalaamu wa masuala ya usalama kwenye mitandao Yusuph Kileo aliendesha semina ya usalama mtandaoni iliyofanyika Dar es salaam Institute of Technology (DIT) na kuhudhuriwa na wanafunzi mbalimbali wa teknolojia ya habari na mawasiliano toka miongoni mwa vyuo vikuu vya jijini Dar es salaam,ikiratibiwa na DIT.

Katika semina hiyo Kileo alielezea ukuaji wa uhalifu kwenye mtandao unavyoendelea kushamili kwa kasi duniani na unavyoleta athali mbalimbali za kiuchumi,kiusalama na kisiasa huku nchi mbalimbali zikiathilika ikiwemo Tanzania huku ikionekana kuwa nchi zinazoendelea bado hajijajidhatiti barabara katika kujilinda na wahalifu wa kwenye mitandao.

Kileo amewataka wanafunzi waliohudhuria semina hiyo kujifunza zaidi masuala ya usalama kwenye mitandao kwani kuna watalaam wachache katika suala  hilo na amesema kuna haja ya vyuo vinavyotoa elimu ya teknohama nchini kuweka somo la usalama kwenye mtandao katika mitaala yao ambapo amesema wamekubaliana na DIT kuipitia mitaala ya taasis hiyo ili mapema mwakani somo hilo lianze kufundishwa kwenye taasis hiyo.

Friday, December 19, 2014

KASISI AWEKA KIFAA KANISANI KUBANA MAWASILIANO YA SIMU KWA WAUMINI



 

Kasisi mmoja nchini Italia, ameweka kifaa kanisani mwake kinachoweza kubana mawasiliano ya simu baada ya kuchoka kuwaomba waumini kuzima simu zao kila wakati alipokuwa anahubiri.

Alilazimika kuomba idhini ya polisi kuweka kifaa hicho baada ya kuchoka kusikia milio ya simu zikipokea ujumbe.

Mpango huo umesifiwa sana na waumini ingawa imewaudhi wenye maduka katika mji wa Naples wanaosema kifaa hicho kinatatiza masafa na mawasiliano yao na pia kifaa hicho kimeathiri mashine za kutoa pesa.

Wanasema kifaa hicho pia kinatatiza shughuli zao ambapo wateja huagiza bidhaa kupitia simu zao za mkononi.

Kasisi Don alikasirishwa sana na waumini wake kujibu simu zao wakiwa kanisani

Lakini kasisi Don Michele Madonna, anakana kwamba kifaa chake kinatatiza shughuli za wenye maduka akisema kinaathiri tu mawasiliano kwa simu kwa waumini walio kanisani peke yake.

'Nilinunua kifaa hicho kutoka kwa duka la vifaa vya elektroniki, na kuwauliza polisi ikiwa ilikuwa sawa kuweka kifaa hiicho kanisani mwangu. Ni kifaa kizuri sana kwa sababu kimemaliza tatizo la watu kupigiwa simu na kuzipokea wakiwa kanisani.

Mmiliki mmoja wa maduka alisema: 'Tangu kasisi Madonna kuweka kifaa hicho ndani ya kanisa , nimepata matatizo sana kutumia kadi yangu katika biashara yangu. ''


Kasisi Michele Madonna aliamua kuchukua msimamo huo kwa sababu waumini walikuwa na mazoea ya kutumia simu zao kanisani wakati kasisi huyo akihubiri. Kilichomuudhi zaidi kasisi huyo ni watu kupokea simu kanisani na hata wakati wa mazishi.

Kasisi Don alinunua kifaa hicho kwa dola sitini.

Kabla ya kukinunua kifaa hicho alianza kwa kuwasihi waumini kutotumia simu zao kanisani kwa sababu zilitatiza shughuli zake.

 Alianza kwa kuweka mabango kanisani humo lakini ujumbe huo wengi hawakuuzingatia na hapo ndipo akalazimika kuweka kifaa hicho ambacho kinazuia watu kupokea au hata kutumia simu zao kanisani.

Popular Posts

Labels