Thursday, August 6, 2015

ZAIDI YA WATU MILIONI MBILI WAJIANDIKISHA KUPIGA KURA KWA MFUMO WA BVR JIJINI DAR ES SALAAM



Wapiga kura 2,845,256 wameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa mfumo wa kielektroniki wa utambuzi wa mwili wa binadamu wa Biometric Voters Registration (BVR), mkoani Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, wapiga kura hao ni sawa na asilimia 101.2.

 Dar es salaam inaelezwa kuwa na wakazi wapatao 4,364,541 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012.


 Jaji Lubuva ametaja idadi ya walioandikishwa katika wilaya za jiji hilo hadi Agosti 04 mwaka huu na idadi yao kuwa ni Kinondoni 1,157,142 sawa na asilimia 105 wakati makadirio yalikuwa ni watu 1,101,565,Temeke lengo lilikuwa watu 896,142, lakini walioandikishwa ni 886,564 sawa na asilimia 98.9 wakati Ilala lengo lilikuwa 811,716, lakini  walioandikishwa ni 886,564 sawa na asilimia 98.9.


Kwa mujibu wa Jaji Lubuva, uwekajiwazi wa daftari la kudumu la wapigakura kwa mikoa iliyokwishapokea daftari utaanza Agosti saba na utadumu kwa siku tano.


Amesema lengo la uwekaji wazi huo ni kutoa fursa kwa wale wote waliojiandikisha kusahihisha taarifa zao, kuhamisha taarifa za wapiga kura waliohama toka kata au jimbo kwenda kata  au jimbo jingine kutoa kadi kwa wapiga kura waliopoteza kadi zao, kuangalia iwapo taarifa za mpiga kura aliyejiandikisha zipo kwenye daftari na kuweka pingamizi kwa jina au taarifa za mpiga kura asiye na sifa ya kuwamo katika daftari.

Popular Posts

Labels