Saturday, August 1, 2015

POSTA NCHINI YAELEZA UMUHIMU WA MATUMIZI YA TEKNOHAMA



Imeelezwa kwamba kadri teknolojia inavyoongezeka, inatengeneza fursa ya kukua kwa Shirika la Posta Duniani.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Shirika la Posta nchini, Fortunatus Kapinga wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ukuaji wa Teknolojia.

Kapinga amesema  kuwa teknolojia inaleta fursa na sio tishio ila inategemea imetumiwaje katika eneo husika na kuongeza kuwa biashara ya mtandao imeimarisha biashara ya shirika hilo ikiwa ni pamoja na kutoa teknolojia mpya.

Aidha amesema kutokana na kuongezeka kwa biashara ya mtandao barani Ulaya, mapato yamekuwa kwa asilimia 1.4, Asia na Amerika ya Kaskazini asilimia 3.9 na ameongeza kwa kusema kuwa shirika limefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(Teknohama) ili kuongeza ubora wa huduma zake.

Popular Posts

Labels