Serikali ya Tanzania imesema shilingi trioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao,endapo Sheria za Mitandao na Miamala ya fedha haitatumika.
Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa ametoa hadhali hiyo wakati akifungua mafunzo ya viongozi wa Jeshi la Polisi yaliyolenga kuwapa elimu kuhusu utekelezaji wa sheria hizo kabla ya kuanza kutumika Septemba Mosi mwaka huu.
Amesema fedha hizo sawa na trioni 4.4 kila mwezi ,watu wanahifadhi na kutumia kupitia miamala mbalimbali ya mitandao ya simu za mikononi.
Profesa Mbarawa amesema fedha hizo lazima zilindwe kwa kuwekewa sheria zenye kuzuia na kutoa adhabu kwa watu watakaoingilia mihamala ya fedha.
Saturday, August 15, 2015
Popular Posts
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...