Serikali ya Tanzania imesema shilingi trioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao,endapo Sheria za Mitandao na Miamala ya fedha haitatumika.
Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa ametoa hadhali hiyo wakati akifungua mafunzo ya viongozi wa Jeshi la Polisi yaliyolenga kuwapa elimu kuhusu utekelezaji wa sheria hizo kabla ya kuanza kutumika Septemba Mosi mwaka huu.
Amesema fedha hizo sawa na trioni 4.4 kila mwezi ,watu wanahifadhi na kutumia kupitia miamala mbalimbali ya mitandao ya simu za mikononi.
Profesa Mbarawa amesema fedha hizo lazima zilindwe kwa kuwekewa sheria zenye kuzuia na kutoa adhabu kwa watu watakaoingilia mihamala ya fedha.
Saturday, August 15, 2015
Popular Posts
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania TCRA Imewataka wananchi wa mikoa ya Tabora na Singida kuepukana na dhana potofu ya matumizi ya televi...
-
Serikali ya Tanzania imeomba mkopo wa Dola za Marekani milioni 154 ambazo ni takribani shilingi za kitanzania bilioni 246 kwa India kuwezesh...