Serikali ya Tanzania imesema shilingi trioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao,endapo Sheria za Mitandao na Miamala ya fedha haitatumika.
Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa ametoa hadhali hiyo wakati akifungua mafunzo ya viongozi wa Jeshi la Polisi yaliyolenga kuwapa elimu kuhusu utekelezaji wa sheria hizo kabla ya kuanza kutumika Septemba Mosi mwaka huu.
Amesema fedha hizo sawa na trioni 4.4 kila mwezi ,watu wanahifadhi na kutumia kupitia miamala mbalimbali ya mitandao ya simu za mikononi.
Profesa Mbarawa amesema fedha hizo lazima zilindwe kwa kuwekewa sheria zenye kuzuia na kutoa adhabu kwa watu watakaoingilia mihamala ya fedha.
Saturday, August 15, 2015
Popular Posts
-
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) jana imekabidhi mradi wa mawasiliano utaotumiwa katika mikoa 12 ya Tanzania kwa ofisi ya Mkaguzi na ...
-
Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto ya kuhifadhi vitu sehemu ambayo mtu anaweza kutumia akiwa popote duniani akiwa ame...
-
Ofisa Biashara wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Thomas Lemunge akitoa ufafanuzi katika semina kwa wahariri juu ya mkongo wa taifa katika...