Thursday, August 27, 2015

MAWASILIANO YA INTANETI KWA SIMU YAZUIWA KATIKA MJI WA AHMEDABAD NCHINI INDIA

A slice of Ahmedabad. Gujarat is home to India's current Prime Minister Narendra Modi
Sehemu ya mji wa Gujarat  ambako anatoka Waziri Mkuu wa sasa wa  India Narendra Mod
Huduma za mawasiliano ya intaneti kwa njia ya simu zimezuiwa katika jimbo la Gujarat lenye wakazi karibu milioni 63  nchini India kutokana na ghasia za  wapinzani wa jumuia ya Patel baada ya mmoja wa wafuasi wake kukamatwa na polisi katika mji wa Ahmedabad wenye wakazi wapatao milioni 3.5 kwa mujibu wa sensa ya umoja wa mataifa ya mwaka 2001

Jamii ya Patel walituma ujumbe mfupi wa maneno kwa raia kupitia mtandao wa kijamii wa WhatsApp kutosababisha machafuko katika eneo hilo.
Ujumbe huo umekuwa ukiambatanishwa na  picha za video na sauti kupitia mtandao huo

Afisa mmoja wa Polisi amesema kuwa walikuwa wakifuatilia taarifa kuwa watu wamekuwa wakiwasiliana kuhusu suala hilo kupitia mtandao wa kijamii wa Whatsapp ingawa ametoa taarifa kuwa huduma za intaneti zitarejea baada ya kuwa wamejiridhisha na hali ya utulivu kama kawaida katika eneo hilo.
Taarifa zingine zinaeleza kuwa mawasiliano ya intaneti kwa njia ya simu yamezuiwa katika jimbo lote la Gujarat.

Popular Posts

Labels