Thursday, August 20, 2015
GOOGLE WAZINDUA SIMU YA KISASA YA BEI RAHISI KWA AJILI YA AFRIKA
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika.
Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupatikana katika nchi sita za Afrika.
Itagharimu kati ya dola 85 na 100. Licha ya kuwa si watu wengi watakuwa na uwezo wa kuinunua, lakini ni bei rahisi kulinganisha na iPhone ambayo inauzwa hadi dola 1,000.
Uzinduzi huu ni juhudi za Google kujaribu kulikamata soko linalokua kwa kasi la simu za kisasa, ambapo watumiaji wengi bado hawana uwezo wa kuwa na vifaa vinavyoweza kuuganishwa kwenye mtandao wa internet.
Hot 2 imeshaanza kuuzwa na baadhi ya wafanyabiashara wa Nigeria na pia inapatikana kwa kununua kwenye mtandao kwa kiasi cha Pesa za Nigeria Naira 17,500 sawa na dola 88 na itapatikana pia hivi karibuni katika nchi za Ghana, Ivory Coast, Kenya,Misri na Morocco.
Kwa mujibu wa Google takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya wanaigeria milioni 50 wanaotumia intaneti asilimia 95 kati yao wanatumia simu za mikononi.
Simu hiyo ambayo ipo katika rangi nyeusi,,nyekundu,nyeupe,dhahabu na blue ina prosesa ya quad-core MediaTek yenye memory ya 16GB na inauwezo wa kutumiwa na sim card mbili,ikiwa imeundwa kwa program endeshi ya Android 6.0 Marshmallow
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Huduma ya ujumbe Whatsapp imetangaza kuwa itayalinda mawasiliano ya wateja wake kuanzia hapo siku ya Jumanne April 5,mwaka huu Huk...
-
Watafiti toka kampuni ya utafiti ya Zscalar wamegundua kuwa,tovuti za kichina zenye picha za ngono zimekuwa zikisamb...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Kuwa na Akaunti ya Facebook ni kwa manufaa yako na manufaa ya Facebook Facebook ambayo kwa sasa inapatikana katika lugha 70 ul...
-
Maofisa wa WAMOJA ICT Consulting Limited Mtangazaji Maduhu na WAMOJA ICT Consulting Limited Kampuni ya WAMOJA ICT Consulting Li...
-
Utafiti uliofanywa mwaka jana na Kampuni ya Utengenezaji wa simu ya Nokia kabla haijabadilishwa na kuwa Microsoft kuhusu biashara ya m...
-
UDUKUZI NI NINI ? Ni uchukuaji wa taarifa za mwingine kwa njia ambazo sio halali kwa kutumia vyombo vya mawasiliano anavyotumia mtu hu...