Thursday, August 20, 2015
GOOGLE WAZINDUA SIMU YA KISASA YA BEI RAHISI KWA AJILI YA AFRIKA
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika.
Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupatikana katika nchi sita za Afrika.
Itagharimu kati ya dola 85 na 100. Licha ya kuwa si watu wengi watakuwa na uwezo wa kuinunua, lakini ni bei rahisi kulinganisha na iPhone ambayo inauzwa hadi dola 1,000.
Uzinduzi huu ni juhudi za Google kujaribu kulikamata soko linalokua kwa kasi la simu za kisasa, ambapo watumiaji wengi bado hawana uwezo wa kuwa na vifaa vinavyoweza kuuganishwa kwenye mtandao wa internet.
Hot 2 imeshaanza kuuzwa na baadhi ya wafanyabiashara wa Nigeria na pia inapatikana kwa kununua kwenye mtandao kwa kiasi cha Pesa za Nigeria Naira 17,500 sawa na dola 88 na itapatikana pia hivi karibuni katika nchi za Ghana, Ivory Coast, Kenya,Misri na Morocco.
Kwa mujibu wa Google takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya wanaigeria milioni 50 wanaotumia intaneti asilimia 95 kati yao wanatumia simu za mikononi.
Simu hiyo ambayo ipo katika rangi nyeusi,,nyekundu,nyeupe,dhahabu na blue ina prosesa ya quad-core MediaTek yenye memory ya 16GB na inauwezo wa kutumiwa na sim card mbili,ikiwa imeundwa kwa program endeshi ya Android 6.0 Marshmallow
Popular Posts
-
Baadhi ya watayarishaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama Masatu G.M,Johnson Kuga na Maduhu Emanueli Maisha na Teknohama ni kipindi kina...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya ...
-
Watu wanne huko nchini Marekani wameushitaki mtandao wa kijamii wa LinkedIn unaowaunganisha wanataaluma kuwa umekuwa ukii...
-
Facebook imekuwa kama Google ya mitandao ya kijamii. kama sasa hivi hauposti status yako basi unapandisha picha au unajibu quiz ...
-
Kwa watumiaji wa Facebook na mitandao jamii mingine jaribuni kuwa makini na kile mnachokiweka ama kutoa maoni katika suala lolote kwenye kur...
-
Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa Wizara ya Sheria nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kwa kile kinachosemekana ni ufichuaj...
-
Laini za simu za mitandao ya simu nchini Tanzania ambazo hazijasajiliwa zitazimwa rasmi Julai 10, mwaka huu. Naibu Waz...
-
Akaunti ya Twitter ya kundi la wanamgambo wa Al Shabaab imesitishwa kwa mara nyingine. Ujumbe kutoka kwa Twitter katika akaunti yake ...