Tuesday, August 11, 2015

SHERIA YA MAKOSA YA UHALIFU WA MITANDAO NCHINI TANZANIA KUANZA KUTUMIKA SEPTEMBA MOSI MWAKA 2015



Wananchi wanaotumia vibaya mitandao huenda wakajikuta matatani hivi karibu kwani Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kuwa  ifikapo Septemba mosi, mwaka huu, Sheria ya Uhalifu wa Mitandao itaanza kutumika humo.

Akizungumza na   waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy amekiri kuwa pamoja na kwamba mamlaka hiyo imefanya kazi kubwa ya kuelimisha jamii juu ya utumiaji sahihi wa mitandao hiyo, bado matumizi yake si mazuri hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Aidha Mamlaka hiyo imebainisha kuwa kwa sasa Tanzania inaongoza kwa kuwa na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, jambo linalosababisha taarifa za mitandao mingi kutoaminika hadi nchi za nje kutokana na kujaa uzushi, uongo, lugha za uchochezi na picha za matusi.

Amesema kutokana na kukithiri kwa matumizi mabaya ya mitandao nchini, kwa sasa nchi nyingi haziamini tena taarifa za mitandao ya kijamii na wala hawazitumii hali inayopaswa kubadilishwa.

Mungy amesema mamlaka hiyo kazi yake kubwa ni kusimamia matumizi ya mitandao hivyo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola, itahakikisha inadhibiti kwa kuelimisha na kuwabaini wale wote wanaotumia vibaya mitandao hiyo.

Popular Posts

Labels