Nchi ya Kenya imechukua hatua ya kwanza katika ujenzi wa kile kinachotarajiwa utakuwa mradi mkubwa zaidi barani Afrika wa mji wa kiteknolojia (Silicon Valley) au unaotegemea sana vifaa vya electroniki katika kuendeleza teknolojia ya habari na mawasiliano.
Rais Mwai Kibaki alizindua rasmi mradi huo katika eneo la Konza,mtaa mdogo kusini mwa Nairobi,ambako mji huo mpya wa kiteknolojia utajengwa katika muda wa miaka 20 ijayo.Rais Kibaki ambaye alizindua mradi huo muda mfupi kabla ya kuondoka madarakani mwezi machi alieleza mji wa Konza utasaidia kubadili uchumi wa Kenya kwa kiasi kikubwa.
Mradi huu wenye thamani ya Dola bilioni kumi na nne na nusu upo chini ya mpango wa Wizara ya Habari na Mawasiliano.Mradi huo unasemekana kutoa nafasi zaidi ya 100,000 za ajira ifikapo mwaka 2030 pamoja na kuendelea kudumisha ukuaji wa pato la nchi la jumla ya aslimia 10 katika kipindi cha miaka 18 ijayo.
Popular Posts
-
Wadau mbalimbali wa mitandao ya kijamii jijini Arusha wameeleza kuwa, Elimu duni kuhusu matumizi ya mtandao ndio chanzo cha matum...
-
AT&T Inc. blasted the Federal Communications Commission on Thursday for compiling what it called an unfair and biased report on what...
-
Almost everyone takes lots of pictures and posts some of them online. With a little more planning of shots and editing, these pictures can ...
-
Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 inakadiliwa kuwa jumla ya program tumishi kwenye simu zitakazo kuwa zimepakuliwa duniani zitakuwa ni bi...
-
Mwishoni mwa juma lililopita pamegundulika hali mbaya ya kiusalama mtandao itakayo waathiri watumiaji wa kivinjari kijulikanacho kama...
-
Baadhi ya washiriki wa semina ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano iliyofanyika jana katika ukumbi wa Tume ya Sayansi na Tekno...
-
Tahadhari ya utapeli: Wizi wa fedha kupitia "mobile banking" “Ujumbe ufuatao nimeupokea kwenye e-mail kutoka kwa mtu ninayefaham...
-
Serikali ya Tanzania imewataka wananchi kutoa maoni yatakayoiboresha sheria ya makosa ya mitandao ya mwaka 2015 iliyosainiwa hivi kar...