Nchi ya Kenya imechukua hatua ya kwanza katika ujenzi wa kile kinachotarajiwa utakuwa mradi mkubwa zaidi barani Afrika wa mji wa kiteknolojia (Silicon Valley) au unaotegemea sana vifaa vya electroniki katika kuendeleza teknolojia ya habari na mawasiliano.
Rais Mwai Kibaki alizindua rasmi mradi huo katika eneo la Konza,mtaa mdogo kusini mwa Nairobi,ambako mji huo mpya wa kiteknolojia utajengwa katika muda wa miaka 20 ijayo.Rais Kibaki ambaye alizindua mradi huo muda mfupi kabla ya kuondoka madarakani mwezi machi alieleza mji wa Konza utasaidia kubadili uchumi wa Kenya kwa kiasi kikubwa.
Mradi huu wenye thamani ya Dola bilioni kumi na nne na nusu upo chini ya mpango wa Wizara ya Habari na Mawasiliano.Mradi huo unasemekana kutoa nafasi zaidi ya 100,000 za ajira ifikapo mwaka 2030 pamoja na kuendelea kudumisha ukuaji wa pato la nchi la jumla ya aslimia 10 katika kipindi cha miaka 18 ijayo.
Popular Posts
-
Mamlaka ya Mawasilino Tanzania, TCRA, imesema watumiaji wa namba za simu ambazo hazikusajiliwa, watakatiwa mawasiliano ifikapo Juni M...
-
Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam wamezungumzia utapeli unaofanywa kwa kutumia simu za mkononi na kusema wengi wanaofanya hivyo husajili...
-
Google I/O ni kongamano linalofanyika kila mwaka California kwa kuwakutanisha Developers wa bidhaa za Google kama Android , Chrome , Chrom...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Mwezeshaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama cha Morning Star Radio,Johnson Mziray akichangia jambo kwenye warsha hiyo,pembeni yake mweny...
-
Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini Tanzania imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu mili...
-
Masomo kwa njia ya mtandao(Online Studies) kwa miaka ya hivi karibuni yamekuwa yakitolewa bure na baadhi ya Vyuo Duniani. Mfano katika...