Thursday, November 6, 2014

WHATSAPP SASA KUWABAINI WAONGO



Picha na Salim Kikeke
 
Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kudai kuwa ujumbe haujafika utakuwa unaongopa mchana kweupe.

  • Huduma hiyo inapatikana kupitia Whatsapp katika simu zote za mkononi zenye uwezo wa kuitumia 
  • Tick ya kijivu ina maana kuwa ujumbe umetumwa, tick mbili za kijivu zina maana ujumbe umemfikia mlengwa, na tick mbili za blue zina maana kuwa mlengwa ameusoma ujumbe uliotumwa
  • Ukibonyeza na kushikilia ujumbe uliotuma inatokea Pressing and holding an individual message shows the Message Info option
  • Ukibofya utaona muda kamili ambao ujumbe huo ulisomwa
  • Maoni kuhusu mabadiliko hayo yamepokelewa tofauti katika mitandao ya kijamii, wapo ambao hawajafurahishwa
whatsapp
Whatsapp haijatoa sababu za kufanya mabadiliko hayo ambayo yamewakera baadhi ya watumiaji.

Kuanzia jana huduma hiyo inayomilikiwa na Facebook- itakuwa ikionyesha tick mbili za rangi ya blue upande wa chini kulia katika kila ujumbe unaotuma kubainisha kuwa umesomwa.

Na ukibofya ujumbe wenyewe utaona muda kamili ambao mlengwa alifungua na kuusoma ujumbe husika.

Kabla ya hapo WhatsApp imekuwa ikionesha muda wa mwisho wa mtumiaji aliokuwa kwenye mtandao huo. 

Saturday, November 1, 2014

JIFUNZE MASOMO YA SEKONDARI KUPITIA SHULE DIRECT KATIKA Internet.org

 
 
 
Kwa mara ya kwanza, wanafunzi Tanzania wanaweza kujipatia nyenzo za kujifunzia masomo ya sekondari bila gharama yoyote kupitia mpango wa Facebook wa Internet.org. 

Mfumo wa masomo ya dijitali wa Shule Direct ni mpango wa kwanza wa aina yake Tanzania, mfumo huu unawapatia wanafunzi na walimu nyenzo za masomo zenye ubora wa hali ya juu zilizotengenezwa kufuata mfumo wa elimu ya Sekondari ya Tanzania.

Watengenezaji wa nyenzo zinazopatikana Shule Direct ni mabingwa katika fani ya elimu, hii inahakikisha kuwa nyenzo zipatikanazo Shule Direct ni sahihi, zinapitiwa na kuhakikiwa mara kwa mara kwa ajili ya maboresho, hivyo zina ubora wa hali ya juu.

Mfumo wa masomo wa kidigitali wa Shule Direct unampa mwanafunzi uhuru wa kujisomea, kujadiliana na kubadilishana mawazo na wanafunzi wenzake wakati wowote na mahali popote.


Kupitia Shule Direct wanafunzi wanaweza kujisomea matini (“notes”), kujibu maswali ya majaribio, pia wanaweza kushiriki mijadala mbali mbali na wanafunzi wenzao na walimu. Mijadala hii inasimamiwa na msimamizi kutoka Shule Direct kuhakiki matumizi salama ya mtandao wa Intaneti na kuwa haki za wanafunzi na watu chini ya umri wa miaka 18 zinahifadhiwa.

Ushirikiano wa Shule Direct na Internet.org ni hatua madhubuti katika kuhakikisha teknolojia iliyopo inatumika kuboresha elimu Tanzania. Ushirikiano huu umekuja wakati muafaka, na ni faida kubwa kwa Shule Direct kwa vile kwa mpango huu nyenzo zetu sasa zitawafikia wanafunzi wengi zaidi. 

Internet.org ni mpango wa Facebook ambao unalenga kuwezesha watu wengi zaidi ambao hawana namba ya kuunganishwa na Intaneti, kuweza kupata namna ya kutumia Intaneti, na kujipatia huduma mbali mbali muhimi k.v. tovutu ya Shule Direct na nyinginezo nyingi zipatikanazo kupitia Intaneti.

Mpango huu wa Internet.org unapatikana kwa watumiaji wa mtandao wa Tigo kwa sasa.

www.shuledirect.co.tz Jifunze. Jadiliana. Wakati wowote. Mahali Popote.
 

KUNUNUA KOMPYUTA MSIMU WA SIKUKUU 2014

 
 laptop images png
Tokea LAPTOP zimeanza kuingia sokoni zimekua sehemu ya maisha yetu ya kila siku . Mwanzoni hazikua zinapendeza sana , Kubwa na Gharama . Lakini siku hizi katika dunia ya ushindani mambo yamebadilika kwa sababu kuna kampuni nyingi zinazotengeneza Laptop kwahiyo zimekua na gharama nafuu na mtu anaweza kuchagua aina anayotaka kulingana na viwango au uwezo wake .

Kuna kampuni nyingi zinazotengeneza Laptop lakini kwa zinazouza sana ni hizi , DELL , ASUS , LENOVO , IBM , HP , SAMSUNG , APPLE , ACER ,CHILLBLAST , ALIENWARE , TOSHIBA ,SCHENKER , MSI , GIGABYTE ,SONY , SCAN .

Kama unataka kununua laptop msimu huu wa sikukuu za mwaka 2014 , huu ni muongozo unaoweza kukufaa katika kuchagua laptop , ingawa baadhi ya vitu vinaweza kubadilika kutokana na nchi na soko kwa ujumla .
Ukienda kwenye Maduka utakuta kuna laptop aina 3 , zile zenye Operating System haswa windows , ambazo hazina kabisa , na ambazo zimewekwa lakini za majaribio ukiingia kwenye mtandao unatakiwa kununua .

Bei za laptop zinategemea moja ya mambo hayo 3 ukiacha mengine yote , laptop ambazo hazina kitu kabisa bei yake ni ndogo inapungua zaidi ya dola 200 kuliko zile ambazo zimeshawekwa Programu kama ni za majaribio au ambazo zimeshasajiliwa kabisa .

Sasa hivi kuna Preview ya Windows 10 , unaweza kuingia dukani ukaambiwa ndio toleo jipya wewe ukakubali kuitumia kumbe ni preview tu baada ya muda itaweza kukusumbua , kwa sasa usitumie windows 10 , tafuta windows 7 au 8 .

Kabla ya kuamua kununua laptop hakikisha unajua kile unachotaka kufanya na laptop husika , kama ni kwa masuala binafsi tu madogo au ya kitaaluma ( kutegemea na taaluma ) . mfano kama unataka kununua ya kuchezea Michezo (Games ) unatakiwa kuchagua yenye viwango na uwezo mkubwa , kama CPU , RAM , zaidi hapo andaa bajeti kubwa .
Kama ni kwa ajili ya Kuandika vitu vyako tu , kutembelea tovuti mbalimbali unaweza kununua laptop ya viwango vidogo na utatumia gharama ndogo .
CPU ndio muendeshaji mkubwa wa Laptop yako kwa ujumla , udogo au ukubwa wa CPU ndio utaamua kasi ya laptop yako kutokana na matumizi . Kuna Kampuni nyingi zinazotengeneza CPU Kama Intel , AMD , Motorola na nyingine nyingi lakini INTEL na AMD ndio zinazonunuliwa zaidi sokoni na kutumika zaidi kwenye laptop , mwendo wake au Spidi inatakiwa iwe kuanzia 3.4 Ghz , Core i5 or i7 M .

Uwezo na Ukubwa wa kuhifadhi vitu wa Laptop yako ni muhimu sana , hii nayo inategemea na aina ya shuguli unazofanya na vitu vyako , kama unavideo nyingi , nyaraka , picha na vitu kama hivyo unashauriwa kua na laptop yenye uwezo na eneo kubwa la kuhifadhia vitu vyako hii inaitwa HDD – Hard Disk Drive , inatakiwa iwe na angalau GB 250 , iwe na mfumo wa SATA .

HDD Kubwa inaendana na RAM wengine huita Memory kubwa , hii inatakiwa kuanzia GB 4 na kuendelea , kutegemeana pia na shuguli unazofanya , laptop inapofanya kazi vitu vyote huhifadhiwa kwenye hii RAM .

Kwa watu wanaopenda michezo ya Kompyuta , kuchora , kutengeneza filamu kutumia Kompyuta , suala la VGA , GPU au Graphic Card ni muhimu sana , uzuri wa Video unayoiona kwenye kioo unategemea sana hii kadi , Kuna kampuni nyingi zinazotegeneza hizi kadi kwa ukubwa na viwango tofauti .

Huwezi kutumia laptop bila ulinzi dhidi ya mashambulio kutoka nje labda kwenye internet au vitu unavyochomeka kama flash , au unavyoingiza kama CD/DVD , hapo ndio tunakuja kwenye suala zima la ANTIVIRUS .Mpaka sasa hivi kampuni nyingi zimeshatoa matoleo mapya ya ANTIVIRUS Zao , kama Kaspersky 2015 , AVIRA , AVG 2015 , AVAST 9.0 , NORTON , SYMANTEC , MCAFEE na Nyingine nyingi . 

Ufanyaji mzuri wa ANTIVIRUS unategemea sana ukubwa na uwezo wa LAPTOP yako na zaidi ni jinsi unavyoiboresha kwa kuingiza kwenye internet kwa ajili ya kufanya updates ( boresha )

Kwa wale wanaopenda kusafiri au sehemu zenye shida ya umeme suala la betri ni muhimu sana kwenye laptop mpaka mwaka mmoja uliopita betri zilikua zinadumu kwa saa 4 lakini sasa hivi kuna mpaka saa 8 kutegemea na aina ya Laptop na Ukubwa wake , betri inayokaa muda mrefu itaweza kukusaidia kwa muda mrefu zaidi .

Screen au Kioo ni muhimu kwa watumiaji wa laptop hili nalo hutegemea shuguli unazofanya , kwa mtumiaji wa kawaida anaweza kuamua kutumia kioo cha kawaida ila kwa mchoraji wa ramani yeye atahitaji laptop yenye kioo kikubwa ili aweze kuona kazi zake na kuchora vizuri zaidi .

Kwenye laptop zote za sasa hivi zinavitu ambavyo ni lazima kama NIC (Sehemu ya Kuchomeka waya wa Mawasiliano ) , WIFI ( Wireless ) , USB , Speaker na Mic , Cardreader , webcam , FingerPrint .

Warranty ni kitu muhimu sana kwenye bidhaa yoyote unayonunua sio kwenye Laptop tu , hii ndio inaeleza jinsi utakavyorudisha laptop dukani kama imeharibika ndani ya muda Fulani na kitu gani kikiharibika ndio urudishe .

Kwenye Laptop na Vifaa vingi warranty inakua ndani ya miaka 3 lakini kwa nchi nyingi za afrika , Tanzania ikiwemo ni mwaka mmoja .

Mwisho kabisa ni kuongea na muuzaji wa bidhaa kuhusu shuguli unayoenda kufanya na kifaa chako kabla ya kununua , ataweza kukushauri zaidi na hata kukuonyesha bidhaa zilizopo ili uweze kuchagua ili usije kupata taabu baada ya kununua .
Na:Yona Maro

Friday, October 31, 2014

TIGO NA FACEBOOK WAZINDUA PROGRAM TUMISHI YA INTERNET.ORG NCHINI TANZANIA

Tanzania
(Picha na:Facebook)
Program tumishi ya Internet.org imezinduliwa jijini Dar es salaam ikiwa ni sehemu ya mpango mpya kati ya mtandao wa kijamii wa Facebook kutoka Marekani na kampuni ya Simu ya  Tigo ya Tanzania ,ambayo inawawezesha wateja wa Tigo kutumia baadhi ya tovuti bila gharama.

Internet.org  iliyozinduliwa Oktober 29 mwaka huu ni mpango wa kimataifa unaoyashirikisha miongoni mwa makampuni makubwa ya teknolojia, taasisi zisizo za kibiashara zinazofanya kazi pamoja kufikisha huduma ya internet kwa mabilioni ya watu duniani ambao hawapati huduma ya internet.

 Kampuni ya mtandao wa kijamii ya Facebook yenye makao yake nchini Marekani ni waanzilishi wa program tumishi ya internet.org ambayo ilianza  kutumika barani Afrika katika nchi ya Zambia julai mwaka huu kwa wateja wa mtandao wa Airtel inawezesha mtumiaji wa simu za viganjani kupata taarifa za Afya,Elimu,Uchumi,ajira,mawasiliano bila ya kutozwa gharama za kimtandao.

Taarifa ya hivi karibuni kutoka mamlaka ya mawasiliano Tanzania - TCRA, ilionyesha kuwa idadi ya watu wanaotumia internet iliongezeka kutoka milioni saba na nusu mwaka 2012 mpaka kufikia milioni tisa nukta tatu mwaka huu 2014.

Taarifa ya Facebook  imeeleza kuwa huduma zinazokuwa zikipatikana bure kwa wateja wa Tigo ni  katika program tumishi ya Internet.org ni
  • AccuWeather
  • BabyCenter & MAMA
  • BBC News & BBC Swahili
  • BrighterMonday
  • The Citizen
  • Facebook
  • Facts for Life
  • Girl Effect
  • Messenger
  • Mwananchi
  • Mwanaspoti
  • OLX
  • Shule Direct
  • SuperSport
  • Tanzania Today
  • Wikipedia
 Hata hivyo wachambuzi wa maswala ya teknolojia wanasema lengo la kuchochea na kuwafikishia watu wengi zaidi huduma ya internet bado litakutana na ugumu mwingine hasa kutokana na gharama za kununulia simu zenye uwezo wa kutumia internet kuwa kubwa na upatinaji wa umeme wa uhakika katika baadhi ya maeneo ya vijijini, japokuwa umeme wa jua umeanza kutumika kwa wingi.

Tuesday, October 21, 2014

FACEBOOK KUTUMIKA KUFUNZA USALAMA BARABARANI


DSC_0135
Naibu Kamishna wa Polisi  na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa la Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga (wa pili kushoto) akifurahi jambo na baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini. Kushoto ni Mratibu wa Mradi wa kuboresha Demokrasia na Amani (DEP) kutoka ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Bi. Beatrice Stephano, Afisa Mfawidhi Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kanda ya ziwa Mwanza, Bw. Ludovick Ringia (wa pili kulia) nje ya ukumbi wa mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu mara baada ya kuwasili katika warsha ya siku nne ya wadau wa utekelezaji wa mradi wa uchaguzi unaolenga kuboresha Demokrasia na Amani nchini (DEP) kuelekea uchaguzi mkuu ujao iliyoandaliwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kufadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo (UNDP). (Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).
Na mwandishi wetu, Dodoma 
Naibu Kamishna wa Polisi  na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa la Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, amekubaliana na haja ya kuanzisha mafunzo katika vyombo vya habari vya kijamii kama facebook ili kutanua uwanja zaidi wa elimu ya usalama barabarani hasa kwa vijana ambao ndio waathirika wakubwa wa ajali.

Aidha amesema Polisi wanafikiriia kuanzisha mfuko wa kielektroniki wa ulipaji wa faini kwa makosa ya barabarani ili kuongeza kasi ya udhibiti na kuondoa tuhuma za rushwa.

Kauli hiyo ameitoa mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na wanahabari na watendaji kutoka redio za jamii nchini mjini Dodoma, katika warsha ya siku nne ya wadau wa utekelezaji wa mradi wa uchaguzi unaolenga kuboresha Demokrasia na Amani nchini (DEP) kuelekea uchaguzi mkuu ujao iliyoandaliwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kufadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo (UNDP).

washa ya siku nne ya wadau wa utekelezaji wa mradi wa uchaguzi unaolenga kuboresha demokrasia na amani nchini kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
DSC_0141
Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Unesco , Bw. Al Amin Yusuph, akisalimiana na Naibu Kamishna wa  Polisi  na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa la Usalama Barabarani, Mohamed Mpingamara baada ya kuwasili kwenye warsha hiyo iliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
Kauli yake hiyo ilifuatia hoja iliyotolewa na Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO), Bw. Al Amin Yusuph, ambaye aligusia redio za jamii katika kusambaza habari zenye kulenga kuokoa maisha na mali kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Mpinga ambaye pia ni kamanda wa kikosi cha usalama barabarani  alisema katika mada yake kwamba changamoto kubwa ni kutekeleza sera ya kuhakikisha kwamba hakuna kifo wala majeruhi katika ajali za usalama barabarani.

Akielezea hali halisi ya ajali barabarani huku akikariri takwimu za Benki ya Dunia na Shirika la Afya Duniani (WHO) kamanda Mpinga alisema kwamba utafiti unaonesha katika kila wakazi 100,000 duniani 24 hufa katika ajali za barabarani ambapo vijana na watu maskini ndio wapo katika hatari kubwa zaidi.

Aidha alisema takwimu zaidi kutoka WHO zinasema kwamba watu million 1 na laki tatu hufa kila mwaka duniani  hapa kwa ajali huku ikibainisha kwamba asilimia 75 ya watu wanaojeruhiwa na kufa wanatoka katika nchi maskini ambazo hazina magari mengi kama zile zilizoendelea.
DSC_0171
Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Unesco , Bw. Al Amin Yusuph (kushoto) akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Naibu Kamishna wa Polisi  na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa la Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, kutoa mada kwa watendaji wa redio za jamii nchini. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa mtandao wa redio za jamii nchini (COMNETA) ambaye pia ni Meneja wa redio jamii Sengerema FM ya mkoani Mwanza  Bw. Felician Ncheye.

Alisema pamoja na takwimu hizo za kutisha za duniani, nchini kwetu pekee watu 4000 hufa kila mwaka kutokana na ajali na mwaka uliopita walikufa watu 4002.

Akitoa mada katika mafunzo hayo alisema kwamba ajali nyingi zinazotokea zinasababishwa na binadamu ambapo asilimia 75 za ajali zote husababishwa na makosa ya kibinadamu.

Alisema utafiti unaonesha kwamba makosa hayo chanzo chake ni uzembe, ulevi, mwendo kasi, kutozingatia sheria, uchovu wa madereva na matumizi ya vyombo vya moto.

Aidha uzembe wa waendesha pikipiki ndio unabeba asilimia 20 hadi 30 ya ajali zote.

Alisema kufunguliwa kwa biashara ya pikipiki kubeba abiria kumewaingiza vijana wengi ambao wengi wao si wataalamu wakikosa sifa ya kuendesha vyombo hivyo vya moto huku wakiwa vinara wa kuvunja sheria barabarani kwa vitendo.

DSC_0212
Naibu Kamishna wa Polisi  na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa la Usalama Barabarani, Mohamed Mpingaakiwasilisha mada kwa watendaji wa redio jamii nchini (hawapo pichani)  waliokuwa wakihudhuria warsha ya siku nne ya wadau wa utekelezaji wa mradi wa uchaguzi unaolenga kuboresha Demokrasia na Amani nchini (DEP) kuelekea uchaguzi mkuu ujao iliyoandaliwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kufadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo (UNDP) iliyoamlizika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma. Kushoto ni Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Unesco , Bw. Al Amin Yusuph na Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa mtandao wa redio za jamii nchini (COMNETA) ambaye pia ni Meneja wa redio jamii Sengerema FM ya mkoani Mwanza  Bw. Felician Ncheye.
Madereva hao alisema wanaendesha kasi, hawavai kofia ngumu na kubeba abiria kwa mtindo wa mishikaki.

Akifafanua zaidi amesema kwamba pamoja na madereva wa pikipiki kuongoza kwa kuvunja sheria hali za barabara kama kukosekana kwa alama, muundo wa barabara zenyewe, utelezi , uchakavu wa vyombo na hali ya hewa vimekuwa visababishi vya ajali.

Kamanda alitaka vyombo vya habari vya redio za jamii kuelimisha madereva matumizi sahihi ya barabara kwa kuwaita wataalamu kuelezea mambo hayo bila chumvi wala kuharibu nidhamu na maisha .

 Alisema mathalani maeneo ya mnadani madereva wamekuwa wakivunja sheria hasa upakiaji wa mizigo isiyozingatia usalama wa abiria waliomo.

Alisema jeshi la polisi limechukua mikakati kadhaa kuwezesha kukabiliana na hali ya usalama barabarani hasa kwa kuanzisha ukamataji wa makosa hatarishi katika usalama wa barabara.

Makosa hayo ni mwendokasi, ulevi, uendeshaji wa hatari na uzidishaji wa abiria alisema faini zinazotolewa zimefanya kupungua kwa ajali kutoka elfu 17 hadi elfu 11.

Alisema mikakati mingine ni utoaji wa elimu kwa kupitia vyombo vya habari na kushukuru kwamba elimu hiyo anaona inasaidia. Alisema wanatoa elimu kupitia televisheni , redio na vyombo vya habari vya kijamii.
DSC_0196
Aidha wamekuwa wakishiriki kutoa mafunzo wakishirikiana na wadau wengine.

Pia aliutaja mkakati mwingine ni kuboresha mifumo ya utendaji kwa kuainisha maeneo yanayotokea ajali mara kwa mara, ukusanyaji wa takwimu na kubadili mfumo wa ukaguzi barabarani kwa kuanzisha maeneo maalumu ya kukagulia magari kwa undani.

Pia kunatengenezwa mfumo wa nukta ambapo dereva anapofanya makosa pointi zinaondolewa na zikimalizika anapokonywa leseni.

Kuhusu ulipaji wa faini kupitia benki na njia nyingine za elektroniki alisema zitarahisha utendaji wa polisi na kuondoa tuhuma za rushwa na pia kuwafanya watu kuwa waangalifu zaidi.

Aidha amesema wanatengeneza utaratibu kwa kushirikiana na wadau wengi kutengenezwa kanuni ya ulazima wa madereva kurejea shule kwa mafunzo hasa kutokana na kubadilika mara kwa mara kwa miundombinu ya barabara na teknolojia ya magari.
DSC_0200
 Sehemu ya wadau/watendaji wa redio jamii wa utekelezaji wa mradi wa uchaguzi unaolenga kuboresha Demokrasia na Amani nchini (DEP) kuelekea uchaguzi mkuu ujao wakifuatilia kwa umakini mada iliyowasilishwa na Kamanda Mpinga kwenye warsha hiyo.
Hata hivyo alisema pamoja na mikakati hiyo na mingine Jeshi la Polisi linakabiliwa na changamoto zinazoambatana na bajeti ndogo ya kuiwezesha kununulia vifaa vya kazi kama speed radar za kisasa na mifumo muafaka ya kusimamia usalama barabarani ambapo kwa sasa kila tatizo wanasukumiziwa polisi iwe ni taa mbovu za barabarani au mashimo.

Changamoto nyingine ni wananchi wenyewe kukosa utamaduni wa kuheshimu sheria mpaka waone polisi.

Alivitaka vyombo vya redio jamii kufundisha wananchi na wala sio kuchochea wao wazidi kuvunja sheria na kuitoa mfano wa matuta barabarani ambayo yanadaiwa na wananchi na kusema hiyo si dawa bali elimu kwa wananchi kuhusu usalama barabarani na namna ya kudhibiti ajali.

Naye Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Unesco , Bw. Al Amin Yusuph akimkaribisha Kamanda Mpinga azungumze alisema mafunzo hayo yameandaliwa kwa ajili redio za jamii kujiuza kw apamoja katika kuhudumia umma na kujiendeleza.

Alisema redio ndio njia pekee ya kuwafikia watanzania wengi hasa kwa kuzingatia kwamba watumiaji wa vyombo vingine ni wachache hasa kutokana na kukosekana kwa nishati na pia kuwa mbali na maeneo yanayotangaza habari.
DSC_0221
Wasaidizi wa Kamanda Mpinga wakigawa machapisho mbalimbali yanayotoa elimu ya usalama barabarani kwa washiriki wa warsha hiyo iliyomalizika mwishoni mwa juma mjini Dodoma.
DSC_0244
DSC_0240
Reportuer wa warsha ya wadau wanaotekeleza mradi wa uchaguzi iliyomalizikia mwishoni mwa juma mjini Dodoma Mchungaji Privatus Karugendo akihoji suala la baadhi ya watumiaji wa vyombo vya moto wanaotumia simu za viganjani pindi wawapo barabarani kitu ambacho ni hatari kwa usalama wao.
DSC_0268
Baadhi ya machapisho yaliyogawiwa kwa watendaji wa redio jamii nchini yanayotoa elimu ya usalama barabarani.
DSC_0255
Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wakipitia machapisho hayo yaliyotolewa na Kitengo cha Polisi Usalama Barabarani kwenye warsha hiyo.
DSC_0259
DSC_0287
Naibu Kamishna wa Polisi  na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa la Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, akipata picha ya kumbukumbu na Mshiriki wa warsha hiyo Prosper Kwigize.
DSC_0292
Naibu Kamishna wa Polisi  na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa la Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, akifurahi jambo na Mkurugenzi wa redio jamii Uvinza Fm, Alhaji Ayubu Kalufya.

Saturday, October 18, 2014

KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO LAKANUSHA UVUMI WA UJUMBE MFUPI WA MANENO

Kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Tanzania limekanusha uvumi wa ujumbe mfupi wa maneno unaoendelea kusambazwa kwenye simu na mitandao ya kijamii kuhusiana na Papa kumtaka Rais Barack Obama wa Marekani kupitisha sheria ya kuabudu siku ya jumapili mwezi huu.

Akizungumza katika kipindi cha Kanisani jumahili kupitia Morning Star Radio ambacho huwapatia nafasi Viongozi mbalimbali wa Kanisa hilo kutoa mada na kuulizwa maswali na wasikilizaji Katibu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato katika Unioni ya Kusini mwa Tanzania Mchungaji James Machage amesema kuwa ujumbe huo ni uvumi na wa uongo ambao hauhusiana na kanisa hilo,kwani kanisa lina utaratibu maalum wa kutoa matamko yanayolihusu na sio katika ujumbe wa maneno katika simu ama kwenye mitandao ya kijamii.

Toka jumatano iliyopita blog hii imekuwa ikitumiwa na kushuhudia ujumbe huo ambao mwanzoni ulikuwa kwa lugha ya kiingereza na ijumaa ukawa umetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili hali ambayo imeleta sintofahamu miongoni mwa waumini wa kanisa la Waadventista Wa Sabato

Ujumbe wenyewe wa kiingereza "Doreen Emmau: The Pope urging US President Barrack Obama to pass the National Sunday Law this month,SDA President Ted Wilson is appealing to all SDA members around the world to pray and have a personal consecration and revival and reformation of Godliness for 7 days either 7 am or 7 pm for the outcome of the Holy Spirit in the form of the latter rain.Plse send to all SDA members.Many will be cold in faith,a prophecy that will go back to the fold of the Beast the pope itself.Be Watchful my friend,Jesus is at the Door....He is coming be Ready....Harry Coombs" 

Wa kiswahili  "Papa amwomba rais wa marekani Barack Obama atangaze sheria ya taifa ya jumapil mwisho wa mwezi huu, rais wa wasabato Ted wilson anawaomba waadventista wasabato duniani kote kufanya maombi na matengenezo kwa siku saba kwa ajili ya utauwa wa kweli muda wa maombi ni saa 1 asbh au 1 jioni kwa kumwagwa roho mtakatifu kwa namna ya mvua.Tafadhali tuma sms kwa waadventista wasabato.Rafiki yangu kesha na uwe tayari YESU anakuja yuko mlangoni"

Naye Katibu Mkuu wa Konferensi ya Mashariki mwa Tanzania Mchungaji Sadock Butoke amesema jana kuwa kanisa hilo halina taarifa hizo na ujumbe huo unapaswa kupuuzwa. 
  

Tuesday, October 14, 2014

CHRISTIANO RONALDO AONGOZA KWA KUWA NA MASHABIKI WENGI KWENYE FACEBOOK,AFIKISHA MILIONI 100

Cristiano Ronaldo, akicheza wakati wa mechi kati ya Ureno na Ufaransa.
 Mchezaji nyota wa timu ya soka ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo,amefanikiwa kuwa mwanamichezo wa kwanza kuwa na mashabiki milioni 100 wanaomfuatilia kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook.

Takwimu hizi zinamfanya Mchezaji huyo ambaye pia huichezea timu ya soka ya nchi yake ya Ureno kufikia kiwango cha zaidi ya takribani mashabiki milioni 30 kwenye mtandao huo ya wale wanaomfuatilia Mchezaji bora wa mpira wa miguu Duniani  Lionel Messi toka Argentina ambaye huchezea timu ya FC Barcelona ya Hispania.

Takwimu hizi ambazo huenda zikamwongezea thamani ya kibiashara mchezaji huyo ikiwemo kupata matangazo ya makampuni mbalimbali ambaye pia ana mashabiki milioni 30.5 wanaomfuatilia kwenye mtandao wa kijamii wa twitter,kwanitukio la hivi karibuni ambapo Christian Ronaldo kwa siku mbili aliandika mapachiko sita kwa muda wa siku mbili akitangaza saa aina ya TagHeuer, tangazo ambalo lilitazamwa mara milioni 34.9 kwenye facebook na kupata likes milioni 2.4 kwenye mtandao huo na kuipatia kampuni ya kutengeneza saa hizo  thamani ya paundi 300,000.

Christian Ronaldo katika tangazo la saa za Tag Heuer

Mwanzoni mwa mwezi huu Mchezaji wa Manchester United Wayne Rooney alikuwa mchezaji wa Kwanza wa Ligi ya Uingereza -PLF kufikisha mashabiki milioni 10 wanaomfuatilia kwenye mtandao wa Twitter.

Saturday, October 11, 2014

BAADHI YA PICHA JINSI WAADVENTISTA WA SABATO WALIVYOUNGANA KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII KUOMBEA TATIZO LA EBOLA

 
 


 

 



Oktoba 11,2014 ilikuwa ni siku maalum kwa waumini wa  Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani kwa ajili ya kuombea waathirika  wa ugonjwa wa ebola,tukio hilo liliwashirikisha watu wote duniani kwa kushiriki kwa kutumia mitandao ya kijamii wa twitter na facebook kwa kutumia #UnitedinPrayer for #EbolaCrisis


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani Mchungaji Ted Wilson hivi karibuni  ambaye anaongoza kanisa hilo lenye waumini milioni 18 katika nchi 215 kutoka divisheni 13 za kanisa hilo duniani amesema ameguswa sana na tatizo la Ebola lililowakumba watu kutoka nchi za Afrika magharibi hasa nchi za Guinea,Siera Leone, Liberia ,Senegal na Nigeria.


Octoba mosi mwaka huu kanisa la waadventista wa sabato kupitia  chama cha wachungaji lilianzisha mkakati wa kufanya maombi duniani kote kwa kutumia mitandao ya kijamii kuombea tatizo la ugonjwa wa ebola  kwa watu waliokumbwa na ugonjwa huo,mkakati ambao umehitimishwa oktoba  11,2014 kwenye makao makuu ya kanisa hilo na viongozi wa ngazi za juu toka sehemu mbalimbali duniani waliokutana yalipo makao makuu ya kanisa hilo Maryland nchini Marekani


Popular Posts

Labels